PROX  WAR  au Proxy Warfare ni vita inayopiganwa kwa kupitia sehemu 
nyingine. Katika vita 'ya kawaida' mapigano huwa kati ya nchi na 
nchi.Kwa mfano, Vita ya Kagera ilkuwa kati ya Tanzania na Uganda, na 
mapambano yalitokea katika nch zote mbili.
Katika
 proxy war hali ni tofauti. Nchi A inaweza kupigana vita na nchi B 
katika nchi C.Yaani kwa ufasaha zaidi, kwa mfano, kuna mapambano katika 
nchi C kati ya jeshi la nchi hiyo na waasi, kisha nchi A inapeleka 
askari wake kuilisaidia jeshi la serikali la nchi C, na nchi B inapeleka
 askari wake (au inasaidia kwa siri) kusaidia waasi wanaopigana na 
serikali ya nchi C.
Naomba ieleweke kuwa mie 
sio nabii wa waangamizi, kwa kimombo 'prophet of doom.' Ninachoongelea 
hapa kinatokana tu na hali halisi ilivyo kwenye mapigano yanayoendelea 
nchi DRC kati ya jeshi la Serikali ya nchi hiyo na kikundi cha waasi cha
 M23.
Nchi yetu imetoa wanajeshi kadhaa 
kushirikiana na Malawi na Afrika Kusini kuunda kikosi cha kulinda amani 
nchini DRC. Lakini kuna taarifa kuwa waasi wa M23 wanapewa sapoti na 
Rwanda (kama ni kweli au la,mie sina hakika...lakini lisemwalo 
lipo...kwanini Rwanda ituhumiwe na si Kenya au Msumbiji?)
Sasa
 tukiangalia hali ya uhusinao kati ya Tanzania na Rwanda katika siku za 
hivi karibuni, na tukijikumbusha kauli ya Rais Paul Kagame kuwa 
"atamsbiri (Rais Jakaya) Kikwete mahala mwafaka kisha amtandike" kuna 
uwezekano "mahala hapo mwafaka" kuwa ni DRC. 
Kwanini
 ninasema hivyo? Uwezekano wa Rwanda kuivamia Tanzania au Tanzania 
kuivamia Rwanda ni mdogo sana,kutokana na sababu mbalimbali. Lakini nchi
 hizo mbili zinaweza 'kupigana vita kirahisi' kupitia mapigano 
yanayoendelea kati ya Jeshi la DRC linalosaidiwa na 'Kikosi cha 
Kimataifa' (kinachojumuisha Jeshi la Tanzania) na waasi wa M23 
(wanaodaiwa kusaidiwa na Rwanda.)
Vyovyote
 itakavyokuwa, vita ni kitu kibaya, natunapaswa kuombea kistokee kwa 
gharama yoyote ile.Mwanafalsafa mahiri wa 'Sanaa ya Vita' (Art of War), 
Mchina SUN TZU anatahadharisha kuwa "vita ni suala la uhai na kifo, 
barabara inayoelekea kwenye usalama au maangamizi..."
Kuna
 wanaojidanganya kuwa Rwanda "ni kijinchi kidogo kisicho na uwezo wa 
kupambana na Tanzania." I wish wangekuwa sahihi.Kwa mujibu wa SUN TZU, 
ushindi katika vita yoyote ile unategemea sana matumizi ya mashushushu 
(wapelelezi) wa ndani na wa nje.
Hivi tunafahamu kuwa tuna Wanyarwanda 
wangapi Tanzania ambao wapo mahsusi katika kufanikisha azma yoyote ile 
ya nchi yao?Kwa maafisa wetu uhamiaji ambao bia mbili tatu tu wapo 
tayari kumpa mtu passport ya Kitanzania, tuna maadui wangapi 
wanaotengeneza idadi yetu kukaribia milioni 50? 
Soma hapa http://suntzusaid.com/book/13 kufahamu
 zaidi kuhusu matumizi ya mashushushu katika vita, kwa mujibu wa SUN 
TZU.(na jaribu kupigia mstari uhusiano wetu wa Malawi na uwezekano wao 
kuwa mojawapo ya aina hizo za mashushushu)
Anyway,
 kama nilivyobainisha hapo awali, mie sio nabii wa majanga.Ningependa 
sana askari wetu waliokwenda huko DRC watimize jukumu lao haraka na 
kurejea nyumbani wakiwa salama WOTE. Nilichoeleza kuhusu PROXY WAR ni 
uchambuzi tu unaozingatia hali halisi.

No comments:
Post a Comment