Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, January 24, 2011

Misri yalaumu jeshi la kiislamu

Maandamano ya Wakristo, Misri
Misri imesema ina ushahidi kuwa kundi la wapiganaji la Kipalestina huko Gaza ambalo lina uhusiano na al-Qaeda lilihusika katika shambulio la bomu kwenye kanisa mjini Alexandria, ambapo watu ishirini na mmoja waliuawa katika mkesha wa mwaka mpya.
Waziri wa mambo ya ndani wa Misri, Habib al-Adly, amesema kundi liitwalo 'jeshi la Kiislamu' lilipanga na kutekeleza shambulio hilo.
Shambulio hilo ni baya zaidi kutokea dhidi ya Wakristo nchini Misri katika kipindi cha karibu muongo mmoja.
Kundi hilo la Gaza limekanusha kuhusika na shambulio hilo na maafisa nchini Misri hawajatoa maelezo zaidi kuhusu shambulio hilo.
Kutokana na shambulio hilo kumekuwa na ghasia baina ya polisi na Wakristo wa madhehebu ya kicopti.
'tuna ushahidi wa kutosha kuwa 'jeshi lao la Kiislamu ' wamehusika katika kupanga na kutekeleza shambulio hili la kigaidi,' Bw Adli alisema katika maadhimisho siku ya Polisi nchini Misri.
Rais Hosni Mubarak aliwasifu polisi akisema kupatikana ushahidi huo kutasaidia kutuliza roho za raia wa Misri.
Shambulio la Alexandria lilisababisha Wakristo ambao ni wachache zaidi nchini humo kuandamana na kuilaumu serikali kwa kutowajali.
Msemaji wa kundi hilo la 'jeshi la Kiislamu' amesema kuwa kundi lao halikuhusika katika shambulio la Kanisa nchini Misri.
Lakini aliongezea kuwa : 'Tunawasifu wale waliotekeleza shambulio hilo'.
'Jeshi la Kiislamu' limelaumiwa kwa utekaji nyara na vurugu huko Gaza.

Saturday, January 22, 2011

SITTA,MWAKYEMBE KUITAWANYA CCM


UPO mpasuko wa wazi ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kama ambavyo vikao na matamko mbalimbali yanayotoka kwenye chama hicho yanavyoonyesha, hasa kuhusu sakata la serikali kulipa mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya Dowans.
Baada ya kauli ya Umoja wa Vijana wa CCM juzi kumtaka mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete, achukue maamuzi magumu kukinusuru chama, hasa kwa kuwachukulia hatua kali vigogo wawili, Waziri wa Ushrikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, Kamati Kuu ya chama hicho imetoa tamko la onyo kwa vijana hao.
Katibu Mwenezi John Chiligati aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ‘amri’ ya vijana hao kwa Rais Kikwete kwamba awachukulie hatua Sitta na Mwakyembe ni suala la serikali na si la chama.
Alisema kufanya hivyo ni kuingilia mamlaka ya Rais iliyowekwa kwa mujibu wa sheria ambayo hutumika kuongoza nchi na kwamba Kamati Kuu inaiachia serikali kuliangalia hilo.
Huku akisisitiza kwamba tamko la UVCCM ni haki ya kitengo hicho cha chama, alisema Kamati Kuu itawaelimisha zaidi vijana hao na akasisitiza: “Ni lazima maamuzi ya chama yaheshimiwe.”
Alisema maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu iliyokutana Januari 20, mwaka huu, imejadili masuala mbalimbali ikiwemo hali ya siasa nchini na kusema kuwa ni lazima serikali iheshimu maamuzi ya mahakama ya kimataifa ya biashara kuhusu mgogoro wake na TANESCO, unaolazimu serikali kuilipa Dowans fidia ya sh 94 bilioni.
Alisema hukumu hiyo ni funzo tosha kwa serikali, hasa katika kuingia mikataba ya miradi ya maendeleo na hata inapotaka kuivunja ni lazima ifuate sheria zilizopo, ikiwa ni pamoja na kufanya makubaliano yenye tija kwa taifa.
“Tunajua hili lililotokea hasa kutokana hukumu ya TANESCO kwa Dowans, tunajua kila Mtanzania ana haki ya kutoa maoni lakini kubwa ni uamuzi wa kisheria na hatuna budi kuuheshimu; kwanza tusubiri uamuzi wa pingamizi lililowekwa Mahakama Kuu ndipo taratibu nyingine zifuatwe na hata tamko la UVCCM ni maoni yao tutakaa nao sisi kama chama na kuwaelekeza taratibu za chama, “ alisema Chiligati.
Alisema TANESCO ilifanya kosa, na Kamati Kuu inaisisitizia serikali umuhimu wa kuzingatia na kuheshimu sheria, ikiwamo maamuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Biashara (ICC).
Hata hivyo, alisema pamoja na hukumu hiyo, ni vema serikali ikasubiri uamuzi wa mahakama kuhusu pingamizi lililofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binaadamu (LHRC) juu ya malipo hayo.
Sakata ya Dowans
Chiligati, alisema Kamati Kuu imeona ni vema kuheshimu maamuzi ya Mahakama na hakuna budi kutekeleza hukumu hiyo ila ni busara kwa serikali kutolipa malipo hayo ya bilioni 94 hadi uamuzi wa Mahakama Kuu kuhusu pingamizi lililowekwa na Kituo cha Haki za Binaadamu liamuliwe ndipo taratibu nyingene zifuate kwa mujibu wa sheria.
Migomo ya Wanafunzi, Wahadhiri wa Vyuo Vikuu nchini
Alisema ni vema serikali ifuatilie kwa makini suala hilo na kulipatia ufumbuzi wa haraka na kama kuna tatizo la malipo ilitakiwa kulipwa kwa wahusika ili kuondokana na hali ya migomo ya kila mara.
Alisema ufuatiliaji wa karibu utasaidia kubaini matatizo na hata kupata suluhu ya kudumu kwa haraka na ikiwezekana kumaliza hali hiyo.
Ila ni muhimu kwa wanafunzi na wahadhiri kuwa na utaratibu wa kutoa matatizo yao kabla na kuacha utaratibu hadi mambo yanapoharibika.
Aidha alisema kukaa meza moja mara kwa mara baina ya serikali na wahadhiri kutasaidia kujadiliana kwa kina na kugundua matatizo na kuyapatia ufumbuzi kwa wakati.
Vurugu za Arusha
Katibu Mwenezi huyo wa CCM, alisema kamwe chama chake hakiko tayari kurudia uchaguzi wa Meya kwani uchaguzi ulifuata taratibu zote za kisheria mbali ya CHADEMA kususia uchaguzi huo.
Alisema katika tatizo hilo ni vizuri CHADEMA wakawa wakweli kwani waliweka pingamizi dhidi ya Mbunge wa Viti Maalum, Mary Chatanda na kusahau kuwa CCM ina wajumbe 16, huku wao wakiwa na wajumbe 14 na TLP mmoja.
Alisema kitendo kilichotokea Kamati Kuu imekijadili kwa kina na kusikitishwa na vurugu hizo zilizopelekea kupoteza maisha ya watu watatu na wengine kujeruhiwa kutokana na kadhia hiyo.
“Ni vizuri CHADEMA wakawa wakweli wamesahau Mbunge wa Viti Maalum hupangiwa eneo la kazi na chama chake, kama wao walivyofanya kwa wabunge wao wawili hali ya kuwa wanaishi Moshi mjini lakini wakapelekwa wilayani Hai na wakashiriki kupiga kura, sasa tatizo liko wapi mbona sisi hatujalalamika ila wao tu ndio wafanye hivyo!?” alisema Chiligati.
Maadhimisho ya miaka 34 ya CCM
Kada na kiongozi huyo wa CCM, alisema Febreuari 5, mwaka huu, CCM itatimiza miaka 34 ya kuzaliwa kwake ambapo sherehe za maadhimisho hayo zitazinduliwa jijini Dar es Salaam Februari Mosi, mwaka huu na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Amani Abeid Karume.
Alisema kuwa katika maadhimisho hayo wameyataka matawi ya CCM nchi nzima kufanya mikutano mikuu na kufanya tathmini ya kina namna ya walivyoshinda uchaguzi na hata maeneo waliyoshidwa kuwa wakweli.
Alisema maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na mikutano ya hadhara kwa nchi nzima kwa kuwashukuru wananchi kwa kuichagua CCM katika Uchaguzi Mkuu uliopita na Februari 5, kilele chake kufanyika mkoani Dodoma na kuhitimishwa na Rais Kikwete kwa kupokea maandamano ya mshikamano.
Semina kwa wabunge wa CCM
Alisema CCM itafanya semina kwa wabunge wake 260 leo katika Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam ili kuwapa uelewa wa namna ya Bunge na kanuni zake kwa mujibu wa sheria.
Alisema Uchaguzi uliopita zaidi ya asilimia 60 ya wabunge wake ni wapya na 40 ni wa zamani hivyo ugeni wao CCM imeona ni muhimu kuwafanyia mafunzo hayo ili kwenda sambamba na kasi na viwango vya wabunge wa Chama cha Mapinduzi.


Korea kusini yawaokoa mateka baharini

Choi Young
Choi Young
Makamanda wa jeshi la wanamaji la Korea kusini wamevamia meli ya mizigo iliyokuwa imetekwa na maharamia katika bahari ya Arabia.
Lt Jenerali Lee Sung-ho alisema mabaharia wote 21 wa meli ya Samho-Jewelry inayomilikiwa na Korea kusini wameokoloewa.
Jeshi hilo la majini limesema wanane miongoni mwa maharamia waliuawa na watano wamekamatwa.
Korea kusini hufanya doria ikiwa ni sehemu inayohusisha mataifa mengi ya kupinga uharamia eneo hilo- ambapo ilipeleka meli ya kivita baada ya meli hiyo kutekwa siku ya Jumamosi.
Shughuli hiyo ya uokoaji ilifanyika takriban kilomita 1,300 kutoka pwani ya Somalia na imeelezwa na Lt Jenerali Lee kama "shughuli ya kijeshi iliyo bora".
Samho Jewelry yenye tani 11,500 ilikuwa imebeba kemikali kutoka muungano wa Imarati kuelekea Sri Lanka ilipotekwa baina ya maji ya Oman na India.
Mapema wiki hii, Rais Lee Myung-Bak aliliambia jeshi hilo kuchukua "hatua zozote ziwezekanazo" ili kuwaokoa Wakorea kusini wanane, Waindonesia wawili na raia wa Burma 11 waliokuwa kwenye meli hiyo.
Manowari ya Choi Young ilikuwa ikiilinda hiyo meli kwa takriban wiki nzima, na jeshi hilo limesema maharamia hao walionekana kupunguzwa nguvu na muda wote wa kukimbizana.


NI KAMA WANAONGEA ..CHEKI JISTORI lenyewe  SASA...yaliyomo yamo??...yamooo

KIJANA: dada mambo vipi mi ni handsome unanionaje..?    BINTI: : yaa...unavutia hasa msuko.. balaa....

KIJANA: hata..wewe una mvuto sana..    BINTI:  mmmh... siamini kweli ??..
KIJANA: aaah nipatie namba yako kiganjani...siunajua mi sibipu natwangaga kotekote   BINTI: ok usijali..

 KIJANA: asante kwa namba ntakupigia 29t...!!  BINTI: ntashukuru kuskia sauti yako..lakin....lakini.... usimwambi mtu eti....


PAUL LUVINGA ATWAA TUZO YA SHUJAA SAFARI LAGER


                                    Mshindi wa SHUJAA wa SAFARI LAGER  bwana paul luvinga
                                Washiriki watatu waliokuwa wanawania nafasi ya shujaa wa safari lager
                                            Bendi ya MJOMBA ikitumbuiza
                              Mkurugenzi wa masoko wa TBL DAVID MINJA wakati wa kutangaza mshindi wa SHUJAA wa SAFARI LAGER.

Majaji wa shindano la SHUJAA wamemchagua PAUL LUVINGA kuwa shujaa wa tuzo hiyo ambaye ameshinda baada ya kuanzisha MAKTABA ya bure ya mtaani na kusaidia zaidi ya wanafunzi 200.

PAUL ambaye amejishindia kitita cha shilingi MILIONI SABA amewashinda washiriki wengine wawili ambao ni MERCY SHAYO na LEONARD MTEPA ambao wamepata shilingi MILIONI MOJA kila mmoja.

Naibu waziri wa kazi na ajira DOKTA MAKONGORO MAHANGA amesema wakati akitoa zawadi kwa mshindi huyo kuwa shindano hilo ni moja ya ukuzaji wa ajira hapa nchini.

Mshindi PAUL mbali na kujinyakulia shilingi milioni saba pia kampuni ya bia ya TBL imempa kiasi cha shilingi MILIONI TATU ili aweze kuboresha wazo lake katika kusaidia jamii inayomzunguka.

Barmasai ashinda Dubai Marathon

David Barmasai Tumo
Barmasai ni bingwa wa Dubai Marathon
Mwanariadha wa Kenya, David Barmasai siku ya Ijumaa aliibuka bingwa wa mbio za Dubai Marathon, baada ya kujiandikishia muda wake bora zaidi katika mashindano hayo, saa 2, dakika 7 na sekunde 18.
Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa mwanariadha huyo, mwenye umri wa miaka 22, kupata ushindi.
Mwaka jana Barmasai alikuwa ni mshindi wa mbio za marathon za Nairobi.
Akizungumza kwa Kiingereza na mwandishi wa BBC Andy Edwards, Barmasai alielezea kwamba mashindano hayo yalikuwa magumu mno, na hakutazamia kuwa mshindi.
"Kwa kweli ilikuwa vigumu mno kushinda mashindano haya. Sikufikiria ningeliweza kupata ushindi katika mashindano haya. Nimefurahi sana kuwatangulia wanariadha wote. Nilishangazwa sana wakati Eliud Kiptanui aliposhindwa kuendelea baada ya kilomita 30", alielezea Barmasai.
Barmasai amesema sasa anafikiria kujiandaa vyema kwa mashindano ya Tokyo Marathon nchini Japan, na kujaribu kuimarisha muda wake.
Mkenya Evans Cheruiyot alimaliza katika nafasi ya pili, na Eshetu Wendimu wa Ethiopia katika nafasi ya tatu.
Kwa upande wa kina dada, Aselefech Medessa wa Ethiopia alikuwa mshindi, kwa kumaliza katika muda wa saa 2, dakika 22, na sekunde 45, sekunde tatu tu kufikia muda bora zaidi wa mashindano hayo.
Lydia Cheromei wa Kenya alikuwa wa pili, na Isabella Andersson kutoka Sweden akamaliza katika nafasi ya tatu.

Afisa wa Congo akamatwa juu ya ubakaji

Maafisa na Umoja wa Mataifa umesema, serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imemkamata afisa wa jeshi juu ya tuhuma za ubakaji wa raia wengi uliofanyika Januari 1 mashariki mwa nchi hiyo.
Lt Kanali Kibibi Mutware anashutumiwa kwa kuongoza ubakaji wa zaidi ya wanawake 50 huko Fizi, jimbo la Kivu ya kaskazini.
Kanali Kibibi ameyatupilia madai hayo na kusema ni uvumi.
Kumekuwa na matukio mengi ya ubakaji wa wanawake wengi mashariki mwa Congo, lakini hili limekuwa tukio kubwa la mara moja kutokea ambalo limehusisha jeshi.
Tahirou Diao, msemaji wa umoja wa mataifa huko Uvira karibu na Fizi, alisema maafisa wa kijeshi wa Congo walimkamata walipotembelea Fizi.

Wanawake wa Congo wakipinga ubakaji dhidi ya wanawake na watoto
Maso'a Mwenembuka, mkuu wa manispaa ya Fizi, alithibitisha kumwona Kanali Kibibi akiwa amefungwa pingu na kuondoshwa, pamoja na takriban wanajeshi wengine 10 waliokamatwa wakihusishwa na ghasia hizo zilizotokea siku ya mwaka mpya.
Vyanzo vya kijeshi na mashirika ya kutetea haki za binadamu vimesema matukio hayo ya mwaka mpya yalianza wakati kundi la watu lilipomvamia askari ambaye alimpiga risasi raia- ikidaiwa kuwa walikuwa wakigombania mwanamke.
Baada ya hapo kundi la wanajeshi likaamua kulipiza kisasi kwa watu wa Fizi.
Ofisi ya umoja wa mataifa ilisema wanajeshi waliwapiga kisu watu 26, akiwemo mtoto mwenye umri wa miaka minne, kuharibu zaidi ya nyumba 200 na kubaka idadi kubwa ya wanawake.
Wakaazi wengi wa Fizi na muathirika wa madai hayo ya ubakaji wameshutumu Kanali Kibibi, afisa kamanda wa eneo hilo, kwa kuongoza vurugu hizo.
Lakini katika mahojiano na BBC wiki hii, alikana madai hayo na kusema wanajeshi waliofanya uhalifu huo walikiuka amri yake.
Ghasia za miaka 16 mashariki mwa Congo zimekithiri kwa udhalilishaji wa wanawake na watoto wa kike.
Zaidi ya wanawake 300, wanaume na watoto walibakwa na muungano wa makundi ya waasi katika mji wa Luvungi na vijiji jirani kaskazini mwa Kivu kilomita kadhaa kutoka kituo cha umoja wa mataifa mwezi Agosti.


                                                       **************************

                               JE DULLY SYKES ALIMTENDEA HAKI BOB JUNIOR?

  Jina la shalobalo alilopewa msaani chipukizi bob junior na dully sykes kiutani lilikuwa lina maana hiyo mama alikuwa anamkejeli akalipokea bila kujua maana akashindwa kulikataa wakati limeshavumaa.
  Maana halisi ya shalobalo kwa kimombo ni sehemu nyeti katika makalio ya nyani...je alijua kama dully alikuwa anamkejeli namna na shalobalo alitaka sana kujua maana yake dully akamwambia ipo siku atamwambia...lakini baadae dully alimwambia maana yake ni mtanashati...kweli?

Djaaka was founded in Beira, Mozambique in 2001 by members from the big traditional music and dance company “Companhia de música e dança traditional da Beira”. Not long after their formation they won the regional young musicians’ festival Music Crossroads in 2002. It was here that they gained substantial regional exposure, winning several prizes, one of which was a visit to Fallun, the folk music festival in Sweden.

Their music reflects various traditions from central Mozambique. Djaaka’s sound can be identified largely by their use of marimba which comes from one area of central Mozambique called “Timbila” is heard on many of their songs. The music is contemporary with a strong traditional touch, both funky and deeply rooted. Djaaka sing in a dialect called Massena, which is not far removed from languages of Zambia, like Bemba and Njanja.

Djaaka is a true live band, skilled musician and good dancers, with outstanding outfits. Their live performance has impressed not only their home audience; it has brought them to festivals in Reunion, Mauritius, South Africa, Zimbabwe, Italy and United Kingdom. They have won the “best Mozambican band” award three times at TOP-Ngoma, held by Radio Mozambique.

MODEL OF A WEEK 
Candice swanipoel,

 This South African model and Victoria Secret Angel was discovered at a flea market when she was 15.  I wonder how easy it is for creepy men to “discover” models.  Anyway, enjoy the week of pictures

Friday, January 21, 2011

Mawaziri Tunisia wajitoa chama cha RCD

Televisheni ya taifa imeripoti, mawaziri wote katika serikali ya mpito ya Tunisia ambao walikuwa katika chama cha Rais aliyekimbia, RCD, wamejitoa kwenye chama hicho.
Hata hivyo, mawaziri hao wataendelea kushikilia nafasi zao za uwaziri katika serikali ya umoja wa kitaifa.
Hapo awali, ilitangazwa kuwa zaidi ya wanachama 30 wa familia ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo walikamatwa.
Maandamano Tunisia
Maandamano Tunisia
Wakati hali Tunisia ikizidi kuwa tete, majeshi yalifyatua risasi za kutoa tahadhari wakati waandamanaji walipoendelea kuzunguka mjini Tunis.
Taarifa kutoka eneo hilo zinaeleza kwamba baadhi ya waandamanaji walijaribu kupanda ukuta wa makao makuu ya RCD.
Majaji wa Tunisia nao waliandamana Tunis wakitaka majaji wote waliofanya kazi chini ya Rais aliyekimbia wajiuzulu.
Vile vile kumekuwa na taarifa za kuwepo maandamano siku ya Alhamis katika miji ya Gafsa na Kef.
Rais Zine al-Abidine Ben Ali alikimbilia Saudi Arabia wiki iliyopita baada ya kufanyika maandamano makubwa ya kupinga ukosefu wa ajira, umaskini na rushwa.
Licha ya kuondoka, maandamano yamekuwa yakiendelea, huku waandamanji wakitaka wanachama wote wa RCD waondoshwe madarakani.
Mawaziri wanne kutoka upinzani wameng'atuka kutoka baraza la mawaziri la serikali ya mpito siku moja baada ya kuundwa, wakitaka mawaziri kutoka chama cha RCD wasihusishwe.
Waziri mkuu Mohammed Ghannouchi na Rais wa serikali ya mpito Fouad Mebazaa- aliyekuwa spika wa bunge dogo- nao wamejiondoa kwenye chama cha RCD ili kujaribu kujiweka mbali na Bw Ben Ali.

Muuaji wa wanawake afungwa Afrika kusini

Thozamile Taki
Thozamile Taki
Muuaji kutoka Afrika kusini amehukumiwa kifungo cha maisha kwa kosa la kuua wanawake 13.
Thozamile Taki, mwenye umri wa miaka 40, anayejulikana kama 'sugarcane killer' kutokana na kutupa miili ya wanawake hao kwenye mashamba ya miwa, na kuwalagahi kwa kuwaahidi kuwatafutia kazi.
Akimhukumu Taki kifungo cha maisha kwa kila kesi, Jaji King Ndlovu amemwelezea kama "mbweha kwenye ngozi ya kondoo."
Raia wa Afrika kusini wamefurahishwa na hukumu hiyo na kusifu jitihada za polisi.
Ndugu wa marehemu- baadhi ambao walikuwa wakimjua Taki binafsi-walilia na kushangilia wakati Jaji Ndlovu alipokuwa akisoma hukumu hiyo katika mahakama kuu ya Durban siku ya Jumatano mchana.
Jaji Ndlovu alisema, jinsi Taki alivyokuwa wakati wa kesi hiyo imechangia katika kutoa uamuzi wa kifungo hicho.
Alisema, " Hata waathiriwa walipolia hadharani wakati wa kutoa ushahidi, ulitabasamu tu."
Zaidi ya watu 100 walitoa ushahidi dhidi ya Taki wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa mwaka 2009.
Miili ya wanawake hao iliyokuwa imeoza ilipatikana kwenye mashamba makubwa ya miwa na chai huko Umzinto, KwaZulu-Natal na Port St Johns mwaka 2007.
Taki amenyimwa haki ya kukata rufaa dhidi ya hukumu yake hiyo na anatarajiwa kupelekwa kwenye gereza lenye ulinzi wa hali ya juu huko KwaZulu-Natal.


 WANANCHI WA  MBEYA WATEKETEZA BASI KWA MOTO

               IGP Mwema
Wananchi wanao daiwa kuwa na hasira kali wakazi wa wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya wameteketeza basi kwa moto baada ya basi hilo kumgonga mtembea kwa miguu.
Akizungumza kwa njia ya Simu Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advotece Nyombi, alisema kuwa pamoja na wananchi hao kuchoma moto basi hilo bado wameweza kufunga barabara na kupelekea msongamano mkubwa wa magari katika eneo hilo la tukio.
Alisema kuwa tukio hilo limetokea leo na kuwa hadi sasa jeshi la polisi linaendelea na jitihada za kuwasihi wananchi hao kutuliza jazba ili kufungua barabara hiyo.
Kamanda huyo alisema mbali ya mtu mmoja huyo aliyegongwa na basi hakuna mtu mwingine ambaye amepata kufa wala kujeruhiwa katika tukio hilo.

Blacks and greys dominate Milan men's catwalks

 Greys and blacks dominated the catwalks Tuesday as Giorgio Armani, DSquared2 and Neil Barrett wound up the fourth and last day of the Milan's men fashion shows for autumn-winter 2011-2012.

Armani presented grey in all its incarnations -- stone coal, blue-grey, greyish-green, with jackets with strong shoulders and clean silhouettes.
Overcoats and fur-lined leather coats, coloured shirts in violet, pink and orange, and buckskin shoes rounded out the collection.
As was to be expected, the twin stylists of DSquared2 put on a spectacular show, complete with a "Little House on the Prairie"-style covered wagon.
The Wild West atmosphere was reflected in the mainly black clothes, with black Wyatt Earp hats and leather braces.
The duo's jackets were very long and tied at the waist with a belt, or very short and hyper-cinched.
Jeans were worn low on the waist, while for nights out there were little waistcoats with khaki on the front and tartan in the back.
In terms of materials, flannel, wool and leather dominated.


USAWA WA KIJINSIA UTAFIKIA HAPA SASA...!!!
Kelele za wanajinsia kutaka usawa wa 50 kwa 50 kati ya mwanamke na mwanaume unaendelea kupata mafanikio makubwa lakini itafika siku wanawaqke wadai haki zote za matendo ya mwanaume mfano kamili ni hapa juu...cheki mdada anavyoinjoi kutoa taka mwili as man....teh  teh...malengo ya milenia ..to empower women.......,vijimamboz 


PRECISION AIR KULETA MAPINDUZI YA BEI ZA NAULI YA NDEGE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNfKuxAlj3p5EUm-YHVdS-W4RY6e5MGrcVCTBlEVjHyN454XQLHGU9_rsPiCdfeHmgG2gh7I9zsyEZO_qoDP9OssjOFwSeQ6sT_wfRSo3qzwLHH-9nIgptbSOUfBlQxr6Nu2maphsGWUo_/s1600/mwaki.jpg  Nauli ya kwenda Zanzibar kuwa 35,000/=, na ukikata ya kwenda na kurudi 60,0000/= Kwa muda wa miezi mitano,akizungumza na waadnishi wa habari mkurugenzi biashara phili mwakitawa 

Thursday, January 20, 2011

MSECHU AZAWADIWA BIMA YA AFYA JIJINI DAR

Msanii wa bongo flava na mshindi wa pili waq mashindano ya bongo star search na Tusker project  SEASON 4 PETER MSECHU amezawadiwa bima ya ya afya ya kiwango cha primier plan na kampuni ya soluhealth,pichani meneja mkuu osca osir akimkabidhi msechu zawadi hiyo jijin Dar es salaam.




Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager na ushirikiano wa kituo cha televisheni cha ITV leo wameweka bayana ukumbi ambapo fainali ya Tuzo ya heshima ya “Shujaa wa Safari lager” itafanyika. Ukumbi huo uko katika Hoteli maarufu na ya kisasa Paradise City Hotel.

Akizungumzia fainali hiyo ya aina yake, Meneja wa Bia ya Safari lager Fimbo Butallah (pichani juu) alisema; Maandalizi yote yameshakamilika, na washiriki wote watatu walioingia fainali watakuwepo katika hafla hiyo ambapo mshindi atatwaa tuzo hiyo ya heshima ikiambatana na kitita cha pesa shilingi milioni saba, pia washiriki wawili waliobaki watapata zawadi ya shilingi milioni moja kila mmoja.

Pia katika fainali hizo zitakazofanyika siku ya Ijumaa tarehe 21 Januari, kutakuwa na burudani toka kwa msanii bingwa wa kughani mashairi Tanzania Mrisho Mpoto, maarufu kama “Mjomba” akiwa ameongozana na bendi yake.

Bw. Butallah pia alitumia nafasi hiyo kutaja jopo la majaji wanaoendesha mchakato mzima wa “Tuzo ya Shujaa wa Safari Lager” ambao ni;-

Bw. Richard Magongo – Mkaguzi mkuu wa Mahesabu, TBL

Bw. Deogratius Rweyunga – Mkurugenzi wa Redio One Stereo na

Bw. Alex Mgongolwa – Mwanasheria na Wakili aliyebobea.

Butallah pia, alitumia muda huo kuwapongeza wananchi kwa kuweza kuonesha ushirikiano wa hali ya juu kuanzia hatua za mwanzo za kupendekeza mashujaa na hadi hivi sasa tukiwa katika mchakato wa kuwapigia kura washiriki watatu walioingia finali ili hatimaye tupate mshindi. Mashujaa walioingia fainali ni:
Ms. Mercy Shayo wa Bomang’ombe – KilimanjaroBw. Paul Luvinga wa Sinza – Dar Es Salaam.Bw. Leonard Mtepa wa Mwananyamala – Dar Es Salaam


KANUMBA KUTEKA SOKO LA FILAMU TANZANIA...KUSHUSHA  VIFAA VYA FILAMU VYA MAMILIONI 
duka linaloitwa B&H.huko new york cityAikitizama taa nzuri kwa production
Akiwa makini kuchagua ili mashabiki wake wa ukweli nwawe nawapa vitu vyenye quality

Hapa ni sehemu za BOOM MIC pesa yako tu hapo kuna kila aina ya mic kwa ajili ya production napo akichukua mojawapo ili sauti iwe nzuri katika movie zake.
  

*WAZIRI NCHIMBI AKUTANA NA WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI LEO

Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mukajanga akimuonyesha jarida la Baraza Waziri wa Habari, vijana, utamaduni na michezo Dr. Emmanuel Nchimbi (kulia ). Wamiliki wa vyombo vya habari nchini (MOAT) na viongozi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) walikuwa na mazungumzo ya kujadili mambo mbalimbali kuhusiana na taaluma ya habari na waziri Dr. Nchimbi leo katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo. Picha na Anna Nkinda - Maelezo
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo) Raphael Hokororo, akifafanua jambo kuhusu sera ya habari wakati wa mazungumzo kati ya wamiliki wa vyombo vya habari nchini (MOAT), na viongozi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Waziri wa Habari, vijana, utamaduni na michezo Dr. Emmanuel Nchimbi katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mukajanga. Mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari nchini Reginald Mengi (kulia) akizungumza jambo wakati wa mkutano huo leo. Kushoto ni Waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo. Anayemsikiliza ni Waziri wa Habari, vijana, utamaduni na michezo Dr. Emmanuel Nchimbi .Waziri wa Habari, vijana, utamaduni na michezo Dr. Emmanuel Nchimbi (wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wamiliki wa vyombo vya habari nchini (MOAT) na viongozi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) mara baada ya kumalizika kwa mkutano wao ulioganyika leo katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo.


WANARIADHA WAPATA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO

                                     Mwanariadha MASUMBUKO akikabidhiwa vifaa vya michezo
                                                          SARAH akikabidhiwa vifaa vya michezo na NCHIMBI
wanariadha wataowakilisha nchi
Hapo jana Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo amekipazia sauti chama cha riadha Tanzania akiwaomba wadhamini binafsi kujitokeza kuusaidia mchezo huo.

Waziri NCHIMBI ametuma maombi haya kwa wadauwakati akikabidhi vifaa vya michezo kwa wanariadha wawili wa Tanzania watakaoshiriki kwenye mashindano ya riadha ya kimataifa yatakayofanyika huko BAMAKO MALI baadae mwezi huu.

JEASHI LA CONGO 'LILIONGOZA UBAKAJI'

Kamanda wa jeshi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameshutumiwa kwa kuongoza ubakaji wa wanawake takriban 50 uliofanyika hivi karibuni.Kumekuwa na ripoti nyingi za ubakaji huko Congo lakini tukio hili linaaminiwa kuwa la kwanza kwa idadi kubwa ya wanawake kubakwa likihusishwa jeshi. Mmoja wa waliobakwa, pamoja na vyanzo vilivyonukuliwa katika ripoti ya umoja wa mataifa, wote wanamshutumu Lt Col Kibibi Mutware kwa kuhusika na ubakaji huo uliofanyika mwaka mpya mjini Fizi.

Dr Faise Chacha, mkuu wa hospitali ya Fizi ameeleza, " Askari mmoja aliuawa hapa karibu kabisa na hospitali hii." "Hiyo ilisababisha wasiwasi na wagonjwa wetu wote wakakimbia. Tulirudi siku ya pili asubuhi na tukaanza kuwapokea watu waliokuwa wamepigwa kisu na wengine- wanawake- waliobakwa." Dr huyo na shirika la kitabibu la kutoa msaada Medecins Sans Frontieres wamewatibu waathirika 51 waliobakwa mpaka sasa.

Kama ilivyo kwa matukio ya awali huko Congo, wengi wanatarajiwa kuficha yaliyowasibu kuepuka kuachwa na waume na familia zao. Wawili miongoni mwa wanawake hao walikubali kuzungumza na BBC ilimradi tu wasitajwe majina yao.

Mmoja aliiambia BBC, " Nilibakwa mbele ya watoto wangu wanne." "Ninaona aibu, ninaona aibu sana. Nikikutana na watu wawili au watatu ambao wanajadili jambo, naanza kuhisi tu kuwa wananizungumzia mimi, hata kama si kuhusu mie."

Mwanamke huyo mwengine alifanikiwa kumtambua aliyembaka. "Ilikuwa jioni na walionibaka walikuwa wanajeshi," alisema kwa sauti ndogo, mwili wake ukiwa umefunikwa na khanga yenye rangi za kuvutia. nakuongeza kwa kusema " Walikuwa wanne- Kibibi na walinzi wake. Wameiba vitu vyetu vyote pamoja na pesa."


TAIFA STARS YALAMBA MILIONI 75

WAANDAAJI wa michuano ya soka kwa Nchi za Bonde la Mto Nile wameipa timu ya soka ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' sh.milioni 75, ingawa ilivurunda.

Taifa Stars ilishika nafasi ya sita kati ya timu saba zilizoshiriki mashindano hayo ya kwanza ambayo yameandaliwa na Misri,huku Burundi ikiwa ndiyo ya mwisho na Sudani imeshika nafasi ya tano, baada ya Jumapili kuifunga Taifa Stars mabao 2-0 katikamechi ya kuwania nafasi ya tano.Lakini juzi Taifa Stars, Sudani na Burundi timu vibonde katika mashindano hayo zilitangazwa kila moja kupewa dola za Marekani50,000 sawa na sh. milioni 75 za Tanzania. Mashindano yaliandaliwa na Chama cha Soka cha Misri (EFA).

Fedha hizo ziliztangazwa baada ya mchezo wa fainali ya michuano hiyo Uwanja wa Jeshi mjini hapa ambapo Misri iliibuka naushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Uganda na kuibuka bingwa.

Kwa kutwaa ubingwa huo ambao unaifanya Misri kuwa bingwa wa kwanza ilizawadiwa dola 150,000 za Marekani sawa na sh. milioni225 za Tanzania, wakati Uganda iliyoshika nafasi ya pili ilizawadiwa dola za Marekani 120,000 sawa na sh.milioni 180 zaTanzania.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambayo juzi iliifunga Kenya baop 1-0 ma kushika nafasi ya tatu, yenyewe ililamba dolaza Marekani 100,000 sawa na sh. milioni 150 za Tanzania, huku Kenya yenyewe ikitia kibindoni dola 60,000 sawa na sh.milioni90 za Tanzania.

Dola moja ya Marekani kwa sasa ni kati ya sh.1460 hadi 1500 hivyo kuifanya angalau Taifa Stars nayo kupoza machungu ya kukosazawadi kubwa za mshindi wa kwanza hadi wa tatu.

Taifa Stars ambayo haikushinda mechi katika mechi ilitarajiwa kuondoka jana usiku na kufika Dar es Salaam leo alfajiri ikiwa,ikiwa imefungwa mechi mbili na kutoka sare mbili Ilifungwa na Misri mabao 5-1, ilifungwa na Sudani mabao 2-0 na ilitoka sare ya bao 1-1 na Uganda na sare kama hiyo na timuiliyoshika nafasi ya mwisho Burundi, ambayo ilipata pointi moja tu ya Stars.

Wakati huohuo, kipa Kidiaba wa DRC alitangazwa kuwa Kipa Bora wa Mashindano, huku mshambuliaji Said Khamdi wa Misri ambayemechi ya fainali alifunga mabao mawili alitangazwa kuwa Mfungaji Bora baada ya kufunga mabao sita na Ahned Said Faraj pia waMisri aliibuka Mchez
aji Bora.

Pongezi wakati wa uzinduzi wa Kilimanjaro Tanzamia Music Award's 2011 usiku huu katika hoteli ya Double Tree jijini Dar.
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja akizungumza katika uzinduzi wa tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Award's 2011 uliofanyika usiku huu katika hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar.
Meneja wa bia ya Kilimanjaro,George Kavishe akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika usiku huu katika hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar.
Katibu Mkuu wa BASATA,Gonche Materego akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika usiku huu katika hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar.

Muwakilishi wa Wasanii wa Music nchini,Luiza Mbuttu akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake wote.
Msanii wa muziki wa Bongo Freva,Marlow akifanya vitu vyake katika uzinduzi huo.
Msanii wa Muziki wa kizazi kipya,Mataluma akikamua usiku huu katika uzinduzi wa tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Award's 2011 uliofanyika usiku huu katika hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar.
MC wa shughuli hiyo,Gardiner Habash akiwajibika ipasavyo katika uzinduzi huo.Ankal akiwa na Wadau wa TBL,Shoto ni Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja na kulia ni Meneja wa bia ya Kilimanjaro,George Kavishe.
Mbunifu wa Mavazi na Mwanamitindo mkongwe hapa nchini,Khadija Mwanamboka akijadiliana jambo na Mrembo Jokate Mwegelo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kilimanjaro Tanzania Music Award's 2011 uliofanyika usiku huu katika hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar.
Wakali wa Bongo Flava.
Miamba ya Kaskazini ikiwakilisha kama kawa.
Amini na Linah wakiwa katika mazungumzo ya hapa na pale.
toka kulia ni Giver Meena,Martin na Mdau.
Wadau wa TBL wakiwakilisha katika uzinduzi huo.
Ma DJ's wa Ukweli kutoka katika familia moja,toka shoto ni Dj Bon Lov,Dj Mackay na Dj Venture.
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja akiwa na Mdau Ben Kisaka pamoja na Miss Tanzania 2010,Genevive Emmanuel katika hafla hiyo ya uzinduzi wa Kilimanjaro Tanzania Music Award's 2011 uliofanyika usiku huu katika hotel ya Double Tree Hilton,Masaki jijini Dar.
Wadau,toka shoto ni Hud,Sylvia Sharry,Martin pamoja na Jamillah.
Msanii wa Bongo Freva,Mwasiti (shoto) akila na Richard,Hamis B 12 na Linda.
Aunt Ezekiel Wadau wenzake katika nyanja ya Filamu.
Wasanii wa Bongo Freva wakiimba wimbo wa pamoja unaohusu Kilimanjaro Tanzania Music Award's usiku huu.
Mamaa wa 8020 Fashions,Shamim Mwasha akiwaonyesha taswirazz kwa warembo mara baada ya kuipata kupitia kamera yake.
Mtu mzima Bon Lov na Banana Zorro pamoja na C Pwaa.
Wadau.
Benjamin wa Mambo Jambo (shoto) akiwa na washkaji wengine wakifuatilia shughuli nzima ya uzinduzi huo usiku huu.
Temba na Chegge wakishow love na mdada wa Double Tree Hilton usiku huu.
toka shoto ni Ahmad Michuzi,Abraham Mossi na Mdau.
Wadau wa TBL wakibadilishana mawazo wakati wa hafla hiyo usiku huu.

Wadau wa Taarab pia walikuwepo.
Wafanyakazi wa TBL.
Wadau