Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Sunday, June 24, 2012

MISS LAKE ZONE HIGHE LEANING HUYU HAPA

Mshindi wa Miss Lake Zone Inter-College 2012 ni Migeshi john na wapili(kushoto)Josephin Winfred(kushoto)ambae ni mshindi wa pili na mshindi wa  tatu Enfilda Clemence (kulia).
Top 5 katika picha ya pamoja mara tu baada ya Josephin kutangazwa mshindi.
 Josephine katika kivazi la ufukweni.

MISS TOURISM KUJA KIVINGINE MWAKA HUU


MISS TOURISM TANZANIA - AT UDIZUNGWA NATIONAL PARKS,MAJEMBE KIBAO YAINGIA KATIKA BODI YA MISS UTALII KUIMARISHA SHINDANO NA KURUDISHA RADHA YA MISS TOURISM TANZANIA.

HILDA EDWARD AWA MISS DAR INTER COLLEGE 2012


Miss Dar Inter College 2012, Hilda Edward akiwa washindi wake wa pili Jamila Hassan kulia na Rose Muchunguzi kushoto, baada ya shindano hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa Makumbusho, katikati ya Jiji la Dar es Salaam 









Hilda akipigana busu moto moto la pongezi na Miss Dar Inter College aliyevua taji Blessing Ngowi


TOP 5; Kutoka kulia Veronica Yole, Sada Suleiman, Rose Muchunguzi, Jamila Hassan na Hilda Edward

DIAMOND PLATINUM;  Nassib Abdul akitumbuiza kwa hisia, kibao Wema Wangu mbele ya jaji Wema Sepetu, ilikuwa tamuuu

Wednesday, June 20, 2012

AZAM MARINE KUMALIZA TATIZO ZANZIBAR

a
 Meli hiyo inavyoonekana kwa Nje
 Meli hiyo inavyoonekana kwa ndani.
Meli hiyo inavyoonekana kwa Ujumla
Azam yaamua kufanya kweli na hivi karibuni meli ya kisasa iko mbioni  kuzinduliwa ambayo ikawezesha watu kwenda na magari yao Zanzibar. Meli hiyo inauwezo kubeba magari 200, abiria 1500 na Mizigo tani 500.KAMPUNI ya Usafiri wa baharini ya Azam Marine inatarajia kuzindua meli kubwa ya kisasa kwaajili ya abiria waendao Dar es Salaam, Pemba na Unguja. Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Hussein Mohamed Said, amesema Julai 15 mwaka huu meli hiyo yenye urefu wa mita 100 itazinduliwa. 
 Mohamedi alisema shida ya usafiri itapungua kwa asilimia kubwa kutokana na meli hiyo kuwa na uwezo wa kubeba abiria 1500, Mizigo tani 500 na magari 200 ambapo abiria atakae jisikia kwenda na gari lake Zanzibar, Pemba au Dar es Salaam ataweza kufanya hivyo.
Waziri Mwenye dhamana ya Mawasiliano na Miundombinu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hamadi Masoud, alithibitisha kwamba anataaarifa za ujio wa meli hiyo ambayo alisema kwa kiasi kikubwa itakuwa ni ya kutoa huduma tu na siyakutengeneza faida. Meli hiyo inauwezo wa kwenda kasi ya notkomail 20.

Monday, June 18, 2012

DIAMOND PLATINUM KUPAMBA MISS DAR INTERCOLLEGE 2012

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Nasib Abdul ‘Diamond’ anatarajiwa kupamba shindano la kumsaka Miss dar Intercollege 2012 linalotarajiwa kufanyika Juni 22 kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa , uliopo mkabala na chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM). 
Mratibu wa shindano hilo Dina Ismail amesema kwamba mbali na Diamond, onyesho hilo pia litapambwa na burudani kutoka bendi ya Skylight iliyopo chini ya mshiriki wa Tusker Project Fame mwaka juzi, Anneth Kushaba.
 Alisema maandalizi ya shindano hilo yanakwenda vema ambapo warembo 14 watakaosghiriki  wanaendelea na mazoezi katika hoteli ya  The Grand Villa iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam 
 “Mwaka huu tumejipanga vema kuhakikisha mmoja ya warembo kutoka Miss Dar Intercollege anafanya vema katika fainali za Miss Tanzania ,”alisema Dina.
 Warembo watakaoshiriki shindano hilo  wanatoka vyuo vya  Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time,  Ustawi wa Jamii,  Usimamizi wa Fedha (IFM)  na Chuo Kikuu huria (OUT ambapo taji linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM, huku mshindi wa pili wa mwaka jana, Blessing Ngowi alitinga fainali za Miss Tanzania. 
Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Veronica Ngota, Rose Muchunguzi, Nancy Maganga, Hilda  Edward, Diana Nyakisinda, Neema Michael, Veronica Yollla, Jacquiline Cliff, Sharifa Ibrahim, Natasha Deo, Saada Suleiman, Rose Masanja na Jamila Hassan. 
Shindano hilo limedhaminiwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s,Dodoma Wine, Ndege Insurance, Skylight Band,Lamada Hotel, Screen Masters,Makumbusho ya Taifa, Mustafa Hassanali, Shear Illusions, Lamada Hotel,Grand Villa Hotel, Sporti Kizaa zaa, Clouds Fm na blog za Michuzi, Mamapipiro, Bin Zubeiry,Mtaa kwa Mtaa na Fullshangwe.

MATRIDA MARTIN AWA MISS DAR CITY CENTER 2012


Redd’s  Miss Dar City Center 2012, Matilda Martin (katikati) akiwa na mshindi wa  pili, Magdalena Munisi (kushoto) na  Mshindi wa tatu, Witness  Michael.


LISSA JENSEN NDIYE MISS WORLD TANZANIA 2012

 Redds Miss Tanzania, Lisa Jensen ambaye atawaiwakilisha Tanzania katika shindano la Miss World 2012 akiwa amepozi kwa picha mara baada ya kuvishwa taji hilo katika shindano lilofanyika katika ukumbi wa 327 Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 Redds Miss World akitoa mada wakati wa shindano hilo.
Washiriki walioingia katika hatua za tano bora

Sunday, June 17, 2012

EDDA MISS KIGAMBONI CITY 2012


Redds Miss Kigamboni City  2012 , Edda Sylvester (21) akipunga mono kwa furaha mara baada ya kutangazwa mshindi na kuvikwa taji la Kigamboni City katika shindano lililofanyika katika Ukumbi wa Navy Kigamboni jijini Dar es Salaam jana. 
Warembo walioingia hatua ya tano bora ya Miss Kigamboni 2012, kutoka kulia Elizabeth Boniface, Ester Albert, Edna Sylvester, Hadija Kombo na Agnes Goodluck wakipozi kwa picha jukwaani baada ya kutajwa kuvuka nafasi hiyo na kupata tiketi ya kushiriki shindano la Miss Temeke 2012 baadea mwaka huu.
Warembo waliokuwa wakiwania taji la Miss Kigamboni City 2012 wakicheza show ya ufunguzi jukwaani.
Redds Miss Kigamboni City  2012 , Edda Sylvester (katikati) akiwa na mshindi wa pili Agnes Goodluck (kushoto) na mshindi wa tatu Elizabeth Boniphace mara baada ya kutangwazwa washindi. Edda aliwashinda warembo wengine 9 katika shindano hilo. (Picha zote na Mroki Mroki) 

MWANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Mlimani jijini Dar es Salaam, Edda Silyvester, 21, usiku wa kuamkia juzi alifanikiwa kutangazwa kuwa mshindi wa taji la kitongoji cha Kigamboni 'Redd's Miss Kigamboni 2012' katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Navy Beach.
Kutokana na ushindi huo Edda alizawadiwa kitita cha Sh. 500,000 taslimu na mgeni rasmi katika shindano hilo, diwani wa Kata ya Kigamboni, Dotto Msawa.
Nafasi ya pili katika shindano hilo lililopambwa na burudani safi kutoka katika bendi ya FM Academia maarufu Wazee wa Ngwasuma ilichukuliwa na Agnes Goodluck ambaye naye alipata zawadi ya Sh. 350,000.
Elizabeth Boniface alichaguliwa kuwa mshindi wa tatu na kupata zawadi ya Sh. 300,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Esther Albert na mshindi watano akiwa ni Khadija Kombo. Elizabeth na Khadija kila mmoja alipata zawadi ya Sh. 200,000.
Jaji Mkuu wa shindano hilo, Benny Kisaka, alitangaza kuwa badala ya warembo watatu atachukua warembo wote watano kwenda kushiriki katika shindano la Kanda ya Temeke baadaye mwaka huu.
Warembo wengine walioshiriki shindano hilo walikuwa ni Sophia Martin, Rosemary Peter, Doreen Kweka na Linnah David waliambulia kitita cha Sh. 150,000 kila mmoja.
Waratibu wa shindano hilo, kampuni ya K& L Media Solutions wanawashukuru wadau wote waliosaidia kufanikisha shindano hilo
Kwa kufanikisha onyesho hilo ambalo lilikuwa ni la mwisho kwenye kanda ya Temeke

Friday, June 15, 2012

NYUMBA YA WEMA SEPETU YENYE THAMANI YA 400ML

Nyumba Ina sebule mbili, Moja ni TV Room na ya pili ni Sitting Room. Hii juu (pichani)ni TV Room na chini (pichani) ni Sitting Room

Hiki ni chumba cha Wema Sepetu, kina Dressing Table mbili, Massage Chair pamoja na Mini Saloon.
Anachumba pembeni ambacho ni kwa ajili ya viatu na nguo.
Hapa ni sehemu maalum ya kufanyia interviews mbalimbali.

Sehemu ya Dining

Wema akiwa amepozi kwenye TV Room
`

MISS DAR CITY CENTER LEO


 Washiriki wa kinyanganyiro cha Redds Miss Dar City Centre wakiwa kwenye mazoezi ya mwisho kwenye kambi yao Kiromo Hotel mjini Bagamoyo.Fainali hiyo itafanyika kwenye Hotel ya Golden Tulip leo Juni 15, 2012.
Warembo hao wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazoezi yao.

MISS DAR INTER COLLEGE KUTEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA J'MOSI


WAREMBO wanaotarajiwa kushiriki shindano la Miss Dar Intercollege 2012  jumamosi  hii wanatarajiwa kutembelea makumbusho ya Taifa kwa ajili ya kujifunza. 
Shindano hilo linatarajiwa kufanyika katika ukumbi huo wa Makumbusho ya Taifa uliopo mkatabala na chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) Juni, 22 mwaka huu. 
Mratibu wa shindano hilo Dina Ismail, alisema ziara hiyo itawasaidia sana warembo hao katika harakati zao za kielimu. 
Alisema Makumbusho ya Taifa ni sehemu muhimu kwa kila Mtanzania kufahamu kutokana na kuwepo vitu vingi vya kihistoria vilivyopata kutokea katika karne zilizopita. 
Kama mjuavyo kule kuna kuna fuvu la mtu wa kwanza duniani (zinjathropas), vyombo, magari na vitu vingine vya kwanza kuanza kutumika,”alisema. 
Dina aliongeza kuwa maandalizi kwa ajili ya shindano hilo yanakwenda vema ambapo washiriki 13 kutoka vyuo vya IFM, Ustawi wa Jamii, Chuo Cha Biashara (CBE), uandishi wa Habari (DSJ) na Huria (OUT) wanaendelea na mazoezi kwenye hoteli ya The Grand Villa iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam. 
Warembo hao ambao wapo chini ya ukufunzi Marlydia Boniface na Bob Rich ni  pamoja na Veronica Ngota, Rose Muchunguzi, Nancy Maganga, Hilda  Edward, Diana Nyakisinda, Neema Michael, Veronica Yollla, Jacquiline Cliff, Sharifa Ibrahim, Natasha Deo, Saada Suleiman, Rose Masanja na Jamila Hassan. 
Shindano hilo limedhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji cha Redd’s Original, Dodoma Wine, Ndege Insurance, Shear Illusions, Skylight Band, Lamada Hotel, Screen Masters, Makumbusho ya Taifa, Mustafa Hassanali, Grand Villa Hotel, Clouds Fm na blog za Michuzi, Mamapipiro, Bin Zubeiry, Mtaa kwa Mtaa na Full Shangwe.

Monday, June 11, 2012

BOB MAKANI AANGWA LEO JIJI DAR ES SALAAM

Waombolezaji mabo wengi wao ni makada wa CHADEMA wakiwa wamebeba sanduku lililohifadhi mwili wa Marehemu Bob Makani wakati mwili huo ulipofikishwa katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam kwaajili ya kutolewaheshima za Mwisho.
Vioongozi wa juu wa Serikali akiwepo Rais Jakaya Kikwete (watatu kuli) Makamu wa Rais, Dk. Gharib Bilali(wapili kulia) Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe (wa nne kulia) walihudhuria.

rais Kikwete akishiriki kubeba sanduku hilo.



CSTHERINE NDIYE REDDS MISS CHANG'OMBE 2012

Redds Miss Chang’ombe 2012, Catherine Masumbigana 21, akipunga mkono mara baada ya kusimikwa rasmi kuwa mshindi wa taji hilo ambapo aliwashinda warembo wengine 13 waliokuwa wakiwania taji la Chang’ombe na tiketi ya kushiriki Miss Temeke 2012.

Redds Miss Chang’ombe 2012, Catherine Masumbigana 21, (katikati) akipunga mkono mara baada ya kusimikwa rasmi kuwa mshindi wa taji hilo. Kulia ni mmshindi wa pili, Jesca Haule (18) na Mshindi wa tatu Zulfa Bundala. Masumbigana aliwashinda warembo wengine 13 katika shindano hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Quality Center jijini Dar es Salaam Juni 10, 2012.
 Tano bora ya Miss Chang’ombe 2012 ambao wote wamepata tiketi ya kushiriki shindano la Miss Temeke 2012 wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka Kushoto ni Zulfa Bundala (21), Jesca Haule (18), Catherine Masumbigana (21), Miriam Nkisigwa (20) na Flora Kazungu.
 Warembo wakicheza show maalum ya ufunguzi
 Warembo wakipita na mavazi ya ubunifu. Kutoka kulia ni Debora Nyakisinda, Like Abraham na Jesca Haule.
 Ilifika zamu ya waarembo wakupita na vazi la ufukweni mbele ya majaji na wapenzi wa sanaa ya urembo nchini waliokuwapo ukumbini hapo. Kutoka kulia ni Debora Nyakisinda, Like Abraham na Jesca Haule.
 Vazi la ufukwenu, Kutoka kulia ni Restituta Faustiney, Wensley Mabula na Clara Diu.
 Miss Chang'ombe 2012, Catherine Masumbigana alivyojinadi na vazi la ufukweni
 Warembo Flora Mayasa (kulia) Catherine Masumbigana (katikati) na Elizabeth Mushi wakiwinda point na vazi la ufukweni.
 Kila mmoja alirusha kete yake, Latifa Mabewa (kulia) akijinadi na Zulfa Bundala
Mkali wa Bongo Fleva Nassib Abdul 'Diamond' na vijana wake walisindikiza show hiyo kwa kutoa burudani kali jukwaani.
 Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Vijana (Mb) Amos Makala akizungumza jukwaani.
 Waratibu wa shindano hilo kutoka King Promotors wakifuatilia onesho. Kushoto ni Tom Chilala.
 Mgeni Rasmi Amos Makala  (kushoto) akimpongeza Mshindi Miss Chang'ombe, Catherine Masumbigana kwa kutwaa taji hilo. Kulia ni Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe.
 Amos Makala (kushoto) akizungumza na Viongozi Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga (kulia) na Prashant Patel.
 Wapenzi wa urembo kutoka Chuo Kikuu cha Kampala tawi la Dar es Salaam nao walikuwepo.
 Washiriki wa Miss Ilala 2012 kutoka Kitongoji cha Tabata jijini Dar es Salaam nao hawakukosekana
 Familia ya Miss Tanzania 2011, nayo ilikuwepo ni mama yake na mdogo wake.
 Vimwana wa Kurasini ambao pia wamepata tiketi ya kushiriki Miss Temeke 2012 wakiwa ukumbini kushuhudia wapinzani wao wapya walioingia kushiriki nao.
 Wadau kutoka Kampumi ya NeXus walidhamini shindano hilo na kulifuatilia kwa ukaribu zaidi.
 Vijana wa Mapacha watatu walikuwepo jukwaani na kutoa burudani kali.