Pages
BRAND NEW MUSIC
metty magese
Listen & Download
http://mdundo.com/a/32626
Friday, February 15, 2013
UNIQUE MODEL CATHERINE ALIVYONG'ARA ONYESHO LA LADY IN RED 2013
Mshindi wa shindano la Unique model 2012Catherine Masumbigana akionyesha mavazi katika onyesho la mavazi la Lady in Red,onyesho hili lilifanyika Serena hotel jijini dar mwishoni mwa wiki iliyopita.
Monday, February 11, 2013
PENZI LA DIAMOND NA PENNIEL LAPAMBA MOTO!

Uvumi ulionea kuhusiana na muunganiko wa mapenzi kati ya Diamond Platnum na DTV VJ Penniel kua ni wapenzi baada ya kusambaa kwa picha kwenye mitandao ya kijamii inayowaonesha wakiwa pamoja kitandani na kula bata sehemu mbalimbali.
Juzi Diamond alithibitisha rasmi kuwa kwa sasa anajivinjari shuka moja na mdada huy huyo kwa kupost picha ya Penny kwenye mtandao wa Instagram na kuandika:.
#MaBabyMama #De’MumOfMyBlood #MamaYounDiamond #YounPlatnumz #YoungPrezident…..
Mwenye macho haambiwi tizama,pia penniel amekuwa karibu sana na mama Diamond kwa kipindi hiki ambapo wachambuzi wa mambo ya kichokonozi wanadai ni katika hali ya kuweka mazingira ya kukubalika ukweni.
WEMA ATOKA NA MBABA
STAA wa filamu mwenye jina kubwa Bongo, Wema Abraham Sepetu, juzikati alitupia picha yake akiwa kimahaba zaidi na mwanaume aliyedai kuwa ni ‘mume’ wake.
Baada ya kuitupia picha hiyo, Wema aliandika: ‘Miss you mume wangu, wewe ndio kila kitu katika maisha yangu, watasema sana lakini mambo yetu yanatuendea vizuri.”
Maneno hayo yanaashiria kuwa Wema anampenda sana mwanaume huyo ambaye siyo Diamond.
RED CARPET YA GRAMMY AWARDS 2013

The Roots arrive at the 55th Annual Grammy Awards at the Staples Center in Los Angeles, CA on February 10, 2013.

Alicia Keys.

Rihanna.
Kelly Rowland.
Beyonce.
Jennifer Lopez.
Adelle.
Janelle Monae.
Ashanti.
Tamia.
Taylor Swift.
Chrissy
Teigen and John Legend arrive at the 55th Annual Grammy Awards at the
Staples Center in Los Angeles, CA on February 10, 2013.
LL Cool J and wife Simone Johnson.
Faith Hill and Tim McGraw.
Jack Antonoff, Nate Ruess, and Andrew Dost.
Justin Timberlake.
Drake.
Chris Brown.
Nas.
Neyo.

Wiz Khalifa and Amber Rose.

Rick Ross.
Jennifer Lopez and Casper Smart.
Friday, February 8, 2013
MSANII MATUMAINI HOI KWA MARADHI ATUA JIJINI TOKA MSUMBIJI
MSANII wa vichekesho ambaye alikuwa nchini Msumbiji, Tumaini
Mwakibibi ‘Matumaini’ jana alipokelewa na wasanii wenzake kibao baada ya
kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar
akiwa hoi kutokana na kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.
Matumaini alitua uwanjani hapo jana majira ya saa 9:30 alasiri ambapo kutokana na hali yake kuwa mbaya wasanii walimbeba mgongoni na kumfikisha kwenye gari ambapo walimpeleka moja kwa moja hospitali ya Amana alikolazwa mpaka sasa akiendelea kupatiwa matibabu.
Matumaini alitua uwanjani hapo jana majira ya saa 9:30 alasiri ambapo kutokana na hali yake kuwa mbaya wasanii walimbeba mgongoni na kumfikisha kwenye gari ambapo walimpeleka moja kwa moja hospitali ya Amana alikolazwa mpaka sasa akiendelea kupatiwa matibabu.
Thursday, February 7, 2013
MTOTO MCHANGA ATUPWA KWENYE DAMBO BAADA YA KUZALIWA
(Tunaomba radhi kwa picha hii si nzuri,ila tunaiweka kukemea matendo ya kinyama dhidi ya watoto)
ZIKIWA zimepita siku takriban tano toka kukutwa kwa mwili wa mtoto mchanga katika eneo la Semtema jirani na makazi ya wanafunzi wa chuo kimoja cha dini mkoani Iringa, simanzi na majonzi zimeendelea kutanda katika Manispaa hiyo baada ya mtoto mwingine wa jinsi ya kike kutupwa katika dampo la taka eneo la Stendi ya M.R mjini Iringa.
Wakizungumzia matukio hayo ya wanawake wasiofahamika kufanya vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto wanaowazaa, baadhi ya akina mama wamelitaka jeshi la polisi na jamii nzima kusaidiana kuendesha misako dhidi ya wanawake wanaofanya vitendo hivyo vya kikatili.
Sarah Sanga, mkazi wa Miyomboni mjini hapa alisema kuwa matukio ya wanawake kutoa mimba na kutupa watoto yameendelea na kuwa ni tishio katika Manispaa ya Iringa.
Bwana Said alishauri wanawake kuwafichua wenzao ambao siku za karibuni walionekana na mimba na ghafla mimba hizo kutoweka kwani wanaweza kuwa wahusika lakini akawalaumu wanaume kwamba wanaweza kuwa chanzo cha tatizo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk. Leticia Warioba akizungumzia tukio hilo amewataka mabinti na vijana wilayani hapo kuepuka kupeana mimba bila kuwa na uhakika wa ndoa.
“Serikali ya wilaya itaendelea kutoa elimu zaidi kwa vijana ili kupunguza tatizo la watoto kutupwa katika wilaya ya Iringa,” alisema
Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa, limethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuahidi kuendelea na msako mkali ili kuwakamata wahusika.
Mpekuzi.
ZIKIWA zimepita siku takriban tano toka kukutwa kwa mwili wa mtoto mchanga katika eneo la Semtema jirani na makazi ya wanafunzi wa chuo kimoja cha dini mkoani Iringa, simanzi na majonzi zimeendelea kutanda katika Manispaa hiyo baada ya mtoto mwingine wa jinsi ya kike kutupwa katika dampo la taka eneo la Stendi ya M.R mjini Iringa.
Wakizungumzia matukio hayo ya wanawake wasiofahamika kufanya vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto wanaowazaa, baadhi ya akina mama wamelitaka jeshi la polisi na jamii nzima kusaidiana kuendesha misako dhidi ya wanawake wanaofanya vitendo hivyo vya kikatili.
Sarah Sanga, mkazi wa Miyomboni mjini hapa alisema kuwa matukio ya wanawake kutoa mimba na kutupa watoto yameendelea na kuwa ni tishio katika Manispaa ya Iringa.
Bwana Said alishauri wanawake kuwafichua wenzao ambao siku za karibuni walionekana na mimba na ghafla mimba hizo kutoweka kwani wanaweza kuwa wahusika lakini akawalaumu wanaume kwamba wanaweza kuwa chanzo cha tatizo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dk. Leticia Warioba akizungumzia tukio hilo amewataka mabinti na vijana wilayani hapo kuepuka kupeana mimba bila kuwa na uhakika wa ndoa.
“Serikali ya wilaya itaendelea kutoa elimu zaidi kwa vijana ili kupunguza tatizo la watoto kutupwa katika wilaya ya Iringa,” alisema
Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa, limethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuahidi kuendelea na msako mkali ili kuwakamata wahusika.
Mpekuzi.
FLAVIAN MATATA ABANGUA DILI LA DIESEL+EDUN
Mwanamitindo wa kimataifa kutoka nchini Tanzania Flaviana Matata ameshiriki katika kampeni za matangazo makubwa ya makampuni ya nguo ya DIESELna EDUN.
Kampeni ya DIESEL + EDUN ilianzishwa mwaka jana mwezi wa kwanza ambapo muanzilishi wa kampuni ya DIESEL – Renzo Rosso – na waanzalishi wa kampuni ya EDUN – Ali Hewson na Bono walisafiri hadi nchi za Uganda na Mali na kukutana na wakulima wa pamba barani Africa.
Waliingia makubaliano ya kutengeneza nguo maalum zitakazotokana na pamba ya wakulima hawa wa Afrika na hivyo kuwanufaisha moja kwa moja. Hivyo basi nguo hizi zinatangazwa kama kampeni ili kunufaisha bara la Afrika.
Nguo hizo zitaanza kupatikana mwanzoni mwa mwezi wa tatu katika maduka mbalimbali nchini Marekani na duniani. Pia nguo za DIESEL + EDUN zitauzwa kupitia mitandao mbalimbali.
Wednesday, February 6, 2013
KAULI YA SPIKA ANNA MAKINDA KUHUSU VURUGU ZA FEB 4 BUNGENI
Spika wa bunge Anne Makinda
amesema taasisi ya bunge inalaani vurugu zilizojitokeza bungeni february
4 2013 na kusababisha kuahirishwa kwa kikao cha bunge wakati wa mjadala
wa mbunge wa Ubungo John Mnyika (Chadema) kuhusu upatikanaji maji
katika jiji la Dar es salaam.Baada ya kipindi cha maswali na majibu february 5 2013 Spika Makinda kasema katika kikao cha dharura cha kamati ya uongozi kilichofanyika feb 4, kimelaani hizo vurugu na kuamua kupeleka hiyo ishu kwenye kamati ya haki, kinga na madaraka ya bunge ili kufanya uchunguzi na kuwasilisha bungeni matokeo ya uchunguzi huo.
Jingine lililojadiliwa na kufanyiwa maamuzi ni kamati kusitisha uwasilishwaji wa hoja zote binafsi za wabunge zilizotakiwa kuwasilishwa katika mkutano huu wa bunge ili kuepuka vurugu zinazoweza kutokea tena.
Baada ya hayo maelezo wabunge kadhaa walisimama na kuomba muongozo wa spika akiwemo mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari aliyehoji kuenguliwa kwa hoja yake, pia mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu aliyetaka kujua hatua zilizofikiwa katika rufaa za wabunge zilizokatwa kupinga maamuzi mbalimbali ya spika.
Namkariri mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari akisema “sasa kama fujo zinatokea bungeni na kupelekea hoja yangu kuondolewa, kamati iliyopaswa kukaa kuzungumza ni kamati ya maadili sio kamati ya uongozi, kamati ya uongozi kimsingi haina mamlaka ya kuondoa hoja yangu kwenye ratiba ya shughuli za leo, mh Spika naomba muongozo wako”
Mbunge Tundu Lissu alisema “kwa taratibu za kanuni za bunge, mbunge ambae haridhiki na uamuzi wa spika anatakiwa akate rufaa na naomba muongozo wako, rufaa zaidi ya 10 ambazo zimekatwa dhidi ya maamuzi ya kwako spika na muheshimiwa naibu spika… za tangu mwaka 1011, za mwaka jana,
RAPPER PREZZO KUFUNGA NDOA NA GOLDIE JUMAMOSI HII
Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali nchini Nigeria, rapper Jackson Makini aka Prezzo anatarajia kufunga ndoa na mwanamuziki wa Nigeria Goldie February 9.
Habari hiyo pia imeandikwa na website ya Big Brother Africa. Harusi hiyo itafanyika jijini Lagos, Nigeria.
Katika hatua nyingine mwakilishi wa mwaka jana wa Nigeria kwenye shindano la Big Brother Africa, anatarajia kuanzisha Reality TV show yake.Goldie anaanzisha show hiyo iitwayo ‘Tru Friendship’. ‘Tru Friendship’ itaonesha maisha ya kila siku ya muimbaji huyo wa Skibobo, Goldie, yote kama mtu maarufu na kama Susan Harvey.
Tuesday, February 5, 2013
KITALE ATWAA JIKO PEUPEE!
Msanii wa Filamu za kuchekesha hapa nchini maarufu kama Kitale, jana amesherehekea siku yake muhim, kwa kufunga ndoa na mpenzi wake, ambae leo hii tunamuongelea kama mkewe, Bi Fatma Salum.
Ndoa hiyo ilifungwa majira ya Saa nane mchana maeneo ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na watu kibao wakiwemo marafiki, ndugu na jamaa.
Friday, February 1, 2013
MAMA SHARO MILIONEA AMTOSA MTOTO ANAEDAIWA NI WA SHARO
MAMA wa aliyekuwa msanii wa muziki na filamu Bongo, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ amefungukia gari aliloacha mwanaye pamoja na mimba ambayo inadaiwa ni yake.
“Kwa upande wa Marry Lucas wa Sumbawanga msichana aliyejitokeza baada ya Sharo kufariki na kusema ana ujauzito wake, siwezi kumtambua kwa sababu enzi za uhai Sharo hakuniambia kuwa ana mchumba wala mpenzi.”
Sharo Milionea alifariki dunia Nov 26, mwaka jana kwa ajali ya gari iliyotokea mkoani Tanga.
Siku chache baadaye, Marry aliibuka na kudai alikuwa mpenzi wa Sharo na ana ujauzito wake.
Thursday, January 31, 2013
UNIQUE MODEL CATHERINE AKIWA NA JUDIE SANGU
Unique model Catherine akiwa katika pozi na Judie Sangu kipindi cha kambi ya shindano la unique model 2012.
Mandhali tulivu katika fukwe za hoteli ya Giraffe ocean view iliyopo jiini Dar es salaam.
Mandhali tulivu katika fukwe za hoteli ya Giraffe ocean view iliyopo jiini Dar es salaam.
WEMA SEPETU ALIVYOJIMWAGA KWA SERENGETI BOY WAKE
Wema Sepetu ameamua kuhamishia majeshi yake kwa kiserengeti boy ili kulipiza kiasi kwa X wake wa zamani, DIAMOND.....
Huyu ni Haidary Cavilla ambaye ni mchumba wa miss Tanzania namba 2 ,mwaka 2000, aitwaye Mercy Galabawa....
Kama kawaida, jamaa ni mdogo kiumri akilinganishwa na Wema, lakini inasemekana kwama Haidary anamiliki mkwanja mrefu ulioichanganya akili ya Wema Sepetu hasa baada ya kununuliwa gari aina ya Audi Q7.....
Picha hizi zilipigwa nyumbani kwa wema sepetu na hatimaye kuvuja mitandaoni,hali inayoashiria kulipiza kisasi kwa Diamond baada ya kunaswa akiwa na Penny....
Wema sepetu ni mrembo anayekabiliwa na skendo chafu ya kubadiliwanaume kama nguo.Alianza na..
Huyu ni Haidary Cavilla ambaye ni mchumba wa miss Tanzania namba 2 ,mwaka 2000, aitwaye Mercy Galabawa....
Kama kawaida, jamaa ni mdogo kiumri akilinganishwa na Wema, lakini inasemekana kwama Haidary anamiliki mkwanja mrefu ulioichanganya akili ya Wema Sepetu hasa baada ya kununuliwa gari aina ya Audi Q7.....
Picha hizi zilipigwa nyumbani kwa wema sepetu na hatimaye kuvuja mitandaoni,hali inayoashiria kulipiza kisasi kwa Diamond baada ya kunaswa akiwa na Penny....
Wema sepetu ni mrembo anayekabiliwa na skendo chafu ya kubadiliwanaume kama nguo.Alianza na..
KITALE KUFUNGA PINGU ZA MAISHA JUMAPILI HII

Kwa mujibu wa Kitale alisema japokuwa amepitia katika changamoto mbalimbali za ki maisha na amejifunza mengi na ndiyo sababu ya kuvuta jiko.
Wednesday, January 30, 2013
Tuesday, January 29, 2013
MAITI YA KICHANGA YAGEUKA JOGOO HOSPITALI YA MWANANYAMALA
BADO tupo mwanzoni mwa mwaka lakini tukio la maiti ya kichanga kugeuka jogoo ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam linaweza kuongoza mengine yote ya ajabu yanayoweza kujiri ndani ya 2013.
Asubuhi ya Jumatano iliyopita, ilikuwa kizaazaa pale jokofu lililotumika kuhifadhi maiti ya kichanga cha mtoto, kukutwa kuna jogoo.
Mshangao zaidi ni kwamba ndani ya lile jokofu, pembeni ya yule jogoo, kulikuwa na hirizi pamoja na tunguri.
Habari kutoka vyanzo vyetu, zimewekwa wazi kuwa Jumanne iliyopita, saa 7 mchana, polisi walipigiwa simu, wakataarifiwa kuhusu maiti ya mtoto iliyokuwa imetelekezwa eneo la Kigogo, Mbuyuni, Dar es Salaam.
Vyanzo vyetu vimebainisha kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kukuta maiti hiyo ya kichanga ikiwa imefunikwa kwa kuzungushiwa sanda.
Kwa mujibu wa Moses Madilu, mkazi wa Kigogo, aliyedai kushuhudia tukio hilo, polisi walipofika eneo la tukio waliikagua maiti hiyo na kubaini kwamba ni ya kike.
Chanzo chetu kikaeleza kuwa baadhi ya mashuhuda, hususan wanawake, walitokwa na machozi kwa masikitiko kwamba itakuwa mtu alijifungua halafu akakinyonga kichanga hicho kabla ya kukitelekeza eneo hilo.
“Baada ya kujiridhisha kwa kazi yao, polisi waliichukua maiti hiyo ya kichanga, wakaipakia kwenye ‘difenda’, wakaipeleka Hospitali ya Mwananyamala,” kilieleza chanzo chetu.
HOSPITALI YA MWANANYAMALA
Ndani ya hospitali hiyo, mwandishi wetu alielezwa kuwa polisi walipofika, walishusha maiti hiyo na kumkabidhi mganga wa zamu aliyejulikana kwa jina moja la Dk. Liwa.
“Dk. Liwa aliwaambia wale polisi wapeleke maiti hiyo mochwari.
“Polisi walifanya hivyo lakini kule mochwari walimkuta msimamizi mkuu, Omar Buyoya aliyekataa kuipokea kwa vile daktari hakuthibitisha kama kile kichanga kilikufa au kilikuwa hai.
“Polisi na Buyoya walivutana kwa muda mrefu, alitokea mhudumu mwingine wa mochwari aliyekuwa akijuana na polisi mmoja aliyebeba ile maiti, alikubali kuupokea mwili huo na kuingiza ndani kwenye jokofu la kuhifadhia maiti.”
Muuguzi huyo aliendelea kusema kuwa siku iliyofuata, Dk. Liwa alifika mochwari na alipofungua jokofu na kufunua sanda, badala ya kukuta maiti ya kichanga, alikuta jogoo, tunguri na hirizi.
“Dk.Liwa alipatwa na mshangao mkubwa huku jasho likimtoka kutokana na uoga, aliwaita wafanyakazi ambao walijazana hapo mochwari kushuhudia.
“Baadhi ya wafanyakazi walipigwa na butwaa huku wengine wakicheka hadi kudondoka chini na wakawa wanajiuliza kama kweli polisi wanaweza kupeleka jogoo hospitali au ni mambo ya kishirikina,” alisema muuguzi huyo.
Dk. Liwa na wafanyakazi wenzake waliondoka mochwari na kuacha hilo jogoo katika chumba cha maiti huku wakishindwa la kufanya.
KAULI YA MGANGA MKUU.....
Uwazi ilimtafuta Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani ambaye alikiri kuonekana kwa jogoo badala ya maiti ya kichanga.
“Polisi walituletea kifurushi wakiamini kuwa ni maiti ya kitoto kichanga ambapo tulikipokea lakini ilipotazamwa na daktari, tulikuta jogoo, hirizi na tunguri, tuliamua kumchoma moto kwa sababu kile ni chumba cha kuhifadhi maiti siyo cha kuhifadhia mizoga ya kuku, ng’ombe au mbwa,” alisema Dk. Ngonyani.
KAULI YA POLISI ...
Naye Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alipoulizwa juu ya sakata hilo alisema kwamba wao kama jeshi la polisi walipigiwa simu na raia mwema kuwa kuna maiti ya kichanga ambapo askari waliondoka hadi eneo la tukio na kuichukua mpaka Hospitali ya Mwananyamala.
“Polisi waliichukua hadi Hospitali ya Mwananyamala kwa wataalamu na baada ya kuikabidhi waliondoka na kuendelea na shughuli nyingine, nami nashangaa kusikia kwamba madaktari walikuta jogoo,” alisema Kenyela.
MASWALI MATANO
Je, ni kweli polisi waliikagua maiti na kugundua ni kichanga cha kike?
Kama ndiyo, ilikuwaje kikageuka jogoo?
Kwa nini daktari hakuipima ile maiti, badala yake akaelekeza ipelekwe mochwari?
Je, au polisi walibeba mzoga wa jogoo, wakampakia kwenye difenda wakidhani ni maiti ya kichanga?
Mkweli nani, polisi wanaodai kupeleka maiti ya kichanga, au hospitali wanaosema walipelekewa mzoga wa kuku, tunguri na hirizi?
Na Mpekuzi
RICK ROSE ANUSURIKA KUPIGWA RISASI ZA TUMBO
Imeripotiwa kwamba nyota Rick Ross, anusurika kujeruhiwa baada ya mtu mmoja aliyekuwa na silaha kurusha risasi kadhaa kwenye gari yake aina ya Rolls Roys
Ndani ya gari hilo aliyekuwemo yeye na msichana mmoja na kusababisha kugonga nyumba akijaribu kuongeza mwendo,taarifa zilizotolewa na mashahidi
Taarifa za polisi zinasema kuwa asubuhi ya leo (jumatatu) wamepokea simu nyingi kutoka kwa wakazi ambao wanaishi maeneo ya Las Olas baada ya kusikia mlio wa risasi
polisi wanasema gari lingine lilisimama karibu na gari la nyota huyo na mtu mmoja aliekuwa ndani ya gari hilo kuanza kurusha risasi kwenye gari la Ross
Nyota huyo hakupatwa na risasi hata moja wakati wa tukio hilo na hakuna mtu yoyote aliyejeruhiwa ndani ya gari hilo.
Mpaka sasa hakuna alietuhumiwa, kugundulika wala kushikiliwa juu ya tukio hilo, polisi wanaendelea kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo
Thursday, January 24, 2013
WANANCHI WACHOMA NYUMBA ZA ASKARI POLISI MKOANI PWANI

KUNDI
la wananchi wanaodaiwa kuwa na hasira, wamevamia kituo cha Polisi cha
Kibiti Wilayani Rufiji na kufanya vurugu kubwa baada ya raia mmoja kufa
kwa kile kilichodaiwa kipigo cha Polisi.
Chanzo
chetu cha Habari kutoka Kibiti kinaipasha kuwa kijana aliyefariki
kutokana na kipigo hicho ni Hamis Mpondi, ambaye mauti yamemfika wakati
akipatiwa matibabu Hospitali ya Muhimbili.
Habari
zaidi zinapasha kuwa hivi sasa wananchi hao wanaendelea kuteketeza
nyumba za Askari Polisi hao zilizopo jirani na kituo hicho, licha ya
Polisi kuendelea kufanya juhudi za kuwatawanya kwa mabomu katika eneo
hilo.
Aidha
wananchi hao wameanza kufunga barabara kuu ya Kilwa iendayo Mikoa ya
Kusini, Lindi na Mtwara kwa mawe, magogo na kuchoma matairi ikiwa ni
umbali wa kama kilometa moja kutoka kituo cha Polisi Kibiti.
Hali
inaelezwa kuwa inazidi kuwa tete huku Polisi wa Kibiti wakiendelea na
jitihada za kudhibiti hali hiyo kwa kufyatua mabomu hewani kujaribu
kutawanya umati huo wa watu. Vurugu zinaendelea, Habari kwa hisani ya
Father Kidevu.
Subscribe to:
Posts (Atom)




































