Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Sunday, November 24, 2013

MFANYAKAZI WA GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL ASHEREKEA BIRTHDAY NA WASHIRIKI WA TANZANIA TOP MODEL 2013

 Mfanyakazi wa Hotel ya Giraffe Ocean View jioni ya jana alisherekea siku yake ya kuzaliwa akiwa kazini kwake,wafanyakazi wenzake na washiriki wa shindano la Tanzania Top model 2013 walijumuika kuila keki ya Birthday,Glady anasherekea kufikisha miaka 40.
(Rose akimlisha keki Gladys Msia kama picha inavyozungumza).
 Gladys akilishwa keki na Bi. Hellen.
 Gladys akiwa na wafanyakazi wenzake Hellen,Martha Mkololo na Gladys kwenye picha ya pamoja.
Mambo ya ku-pop campaign yaliendelea.Thomas Fusi akifungua campaign kimadaha.
 Hapa wimbo wa Hapy birthay to you ukiimbwa....
 Washiriki wa Tanzania Top Model wakishiriki birthday ya Gladys.

Wednesday, November 20, 2013

WASHIRIKI WA TANZANIA TOP MODEL KUPIGA KAMBI GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL

 Mkurugenzi Tanzania Top model Ysufu George akiongea na wanahabari kuhusu ujio wa kuweka kambi ya siku 17 ya wanamitindo hao katika Hoteli ya Giraffe ocean view iliyomo Frikana jijini Dar.
 Wanamitindo wakiwasili leo mapema Giraffe Ocean View Hotel wakitokea Tamar Hotel walikokuwa wameweka kambi ya siku mbili baada ya kutokea hotel ja Jb Bekmont.
Giraffe ocean View Hotel ,hoteli yenye hadhi ya nyota nne,karibu Giraffe upate huduma zilizo sawa na thamani ya pesa zako,inasifika kwa ukarimu uliopita kiwango.

AFANDE SELE APOKELEWA KWA SHANGWE BAADA YA KUJIUNGA CHADEMA






Mwanamziki mashuhuri Tanzania, anayejulikana kama Afande Sele Amejiunga na M4C, kwa kuingia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo. Mji wa morogoro ulirindima vifijo wakati Afande akizunguka na Msafara wa Piki Piki kuwaaga rasmi wale wasio na misimamo thabiti Kisiasa, kama inavyoonekana katika picha. 

kwa upande mwingine wapenzi wa CCM walionekana kuwa nahofu na uchungu, na walihisi sasa mambo yanazidi kuwa magumu sana kwao.

Kata ya mafiga wa upande wake ilionekana kutekwa kabisa na CHADEMA, huku katika mkutano wa Ndani Afande Sele alichaguliwa kushika nafasi ya Uenyekiti wa kata hiyo, katika kipindi hiki cha kushusha chama kwa wananchi (Program ya Chadema ni msingi), ambayo imekuwa mwiba mkali kwa CCM.

NDOA YA PACHA WA P-SQUARE YAINGIA DOSARI

Jumapili ya November 17, 2013, jiji la Lagos, Nigeria lilishuhudia harusi kubwa ya kitamaduni kati ya muimbaji wa kundi la P-Square, Peter Okoye na mchumba wake Lola Omotayo, lakini cha ajabu, kaka yake mkubwa, Jude Okoye hakuwepo.
 
Msemaji wa kundi hilo Bayo Adetu alisema Jude hakuwepo kwenye harusi kwakuwa alikwama nchini Ghana.
Jude_okoye-2 Jude Okoye
P-Square walikuwa wametumbuiza jijini Accra, Ghana kwenye show ya ‘Glo and Bounce Slide‘ siku moja kabla ya harusi na hivyo Adetu akadai kuwa Jude alikosa ndege na hivyo kushindwa kurejea Lagos kushuhudia harusi hiyo iliyohudhuriwa na mastaa kibao akiwemo Diamond Platnumz.
 
Lakini chanzo cha sehemu ya kundi la wasanii wengine walioenda Ghana kwenye show hiyo kilisema Jude hakwenda Ghana. 
 
‘Hatukumuona, mapacha hao walikuwa hapa na bendi yao lakini hatukumuona Jude‘, chanzo hicho kilisema.
 
Vyanzo vya ndani kwenye familia ya Okoye vimedai kuwa Jude Okoye na wanafamilia wengine hawakuiunga mkono ndoa ya Peter na mama wa mwanae Lola Omotayo. Vyanzo vingine vimedai kuwa marehemu mama yao naye hakuwa akiuunga mkono uhusiano huo.
dc6c29ec506111e387720e8e429886c3_8 Lola
‘Jude na wengine hawampendi. Hawakutoa baraka zao kwa ndoa hiyo. Hata Paul pia, lakini ni pacha wake. Hata ndugu wengine walikuwepo pale walikuwa wagumu pia kuhudhuria. Jude hakwenda kwasababu hakuwa ameliunga mkono wazo hilo tangu siku ya kwanza,’ chanzo cha familia hiyo kilisema.
LolaOmotayoMakeupLook2_that1960chickdotcom  Lola ni mrembo haswaa
Baadhi ya wanafamilia wa Okoye walienda mbali zaidi na kudai kuwa Lola Omotayo anadaiwa kumsaliti Peter Okoye mara kwa mara. Inadaiwa kuwa walikuwa wanadai vifanyike vipimo vya DNA kubaini kama kweli Cameron na Aliona ni wa Peter kweli ama kashikishwa tu.

Peterrrr 
Peter akiwa na mwanae Cameron
‘Ni serious kabisa, wanadai kuwa Lola hulala na wale anaowaita ‘wajomba’ na wanataka vifanyike vipimo vya DNA, wanataka kumlinda kaka yao.’
   
 
Hata hivyo madai hayo hayajathibitishwa bado.

WASHIRIKI WA TANZANIA TOP MODEL KUPIGA KAMBI GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL

 Mkurugenzi Tanzania Top model Ysufu George akiongea na wanahabari kuhusu ujio wa kuweka kambi ya siku 17 ya wanamitindo hao katika Hoteli ya Giraffe ocean view iliyomo Frikana jijini Dar.
 Wanamitindo wakiwasili leo mapema Giraffe Ocean View Hotel wakitokea Tamar Hotel walikokuwa wameweka kambi ya siku mbili baada ya kutokea hotel ja Jb Bekmont.
Giraffe ocean View Hotel ,hoteli yenye hadhi ya nyota nne,karibu Giraffe upate huduma zilizo sawa na thamani ya pesa zako,inasifika kwa ukarimu uliopita kiwango.

TANZANIA TOP MODEL WAFUNGUA RASMI ZOEZI LA UPIGAJI KURA KWA WASHIRIKI

  Mkurugenzi wa shindano la Tanzania Top Model 2013 Bw. Jackson Kalikumtima akitangaza rasmi namba ya kupiga kura ili kumchagua mshiriki umpendae kushinda taji la Princess of Tanzania.
  Bwana Kalikumtima aliyasema hayo keo katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanika katika hoteli ya Tamar iliyopo mwenge jijini Dar.
Namba iliyotangazwa ni 15564 ikiwa ni namba maalumu unatuma ujumbe mfupi wa maneno Mfano :  TM Nyanjige kwenda 15564 hapo utakuwa umemwezesha mshiriki umpendae kushinda taji. hilo.
 Baadhi ya vionjo vya vipindi vya televisheni vitakavyoruka Clouds Tv kila siku kuanzia leo usiku saa tatu hadi siku ya fainali vilioneshwa kwa waandishi wa habari hii leo
 Huu ndiyo mfumo mpya wa kumchagua mshiriki umpendae.
 Washiriki wa Tanzania Top model wakiwa katika mkutano na waandishi wa Habari hii leo.