Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam
imesema itawachukulia hatua za kisheria wamiliki wa klabu za usiku
zinazokiuka maadili kwa kuruhusu klabu zao kupiga ngoma ya
‘bunyerobunyero’.
Ngoma hiyo iliibuka na kuwa maarufu hasa
jijini Dar es Salaam baada ya Polisi kupiga marufuku ngoma ya
‘kantangaze-kigodoro’ na ‘khanga moko’.
Onyo hilo lilitolewa jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Kanda hiyo, Suleiman Kova wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema ngoma hiyo imeibuka karibuni na inaenda kinyume na maadili ya Kitanzania.
No comments:
Post a Comment