Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, August 31, 2011

REDDS KUANDAA ONYESHO KUBWA LA MAVAZI NA WASHIRIKI WA MISS TANZANIA 2011 KUSHEHEREKEA MIAKA 50 YA UHURU.



Victoria Kimaro

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original imeandaa maonesho makubwa ya mavazi yatakayowashirikisha warembo wa Miss Tanzania 2011 yenye kaulimbiu ya kusheherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.
Redd’s ambayo ni kinywaji rasmi cha shindano la Miss Tanzania 2011 wamedhamiria kutumia maonesho haya kama chachu ya kuwapatia washiriki nafasi ya kuonesha vipaji vyao katika sanaa ya mitindo.na kuwakutanisha na wadau wa fani ya mitindo ili waweze kujipatia njia mbadala ya kujiendeleza  baada ya mashindano.
                                      
Akiwa anaongea kuhusiana na onesho hili meneja wa kinywaji cha Redds Bi. Victoria Kimaro alisema “Redds kama mdhamini aliyeshiriki kikamilifu kwenye mashindano haya ya urembo toka kwenye ngazi za chini za vitongoji imetambua kuwa kuna umuhimu wa kuwapatia washiriki nafasi za ziada za kuonesha vipaji vyao kwenye fani mbalimbali ikiwemo ya ulimbwende na mitindo ili kuwawezesha kuwa na njia mbalimbali za kujipatia mafanikio ya kimaisha. Maonesho haya ya mavazi yatawakutanisha warembo na wadau mbalimbali wa mitindo kama wabunifu wa mavazi, taasisi za walimbwende na makampuni ya matangazo ili waweze kugundua vipaji vipya na kuvipatia nafasi ya kuviendeleza.” Bi. Kimaro aliendelea kwa kusema kuwa “Tasnia ya urembo ina mchango mkubwa kwenye jamii yetu sio tu kwa upande wa burudani bali inawapatia nafasi warembo mbalimbali Tanzania kukuza vipaji vyao na kuwekea msingi ambao wakijipanga vizuri utawajenga na kuwaletea mafanikio mbalimbali kweye maisha yao.  Maonesho haya ya mavazi ni mojawapo ya fursa ambayo Redds inayowapatia warembo wakuze vipaji vyao kama njia mbadala ya kujipatia maendeleo na mafanikio baada ya shindano la kitaifa.”

Maonesho hayo ambayo yatafanyika siku ya Ijumaa ya tarehe 2 Mwezi wa 8 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam yatajumuisha wadau mbalimbali wa mitindo, burudani kutoka kwa Banana Zorro na B Band pamoja na mwanadada mkali wa mziki wa kizazi kipya Shaa. Warembo wa Miss Tanzania siku ya onyesho watavaa nguo zilizobuniwa na wanamitindo mbalimbali kama Binti Africa,, Kijo na Franco. Onyesho hili pia limemshirikisha mwanamitindo maarufu kutoka mji wa New York ambaye pia amefanya kazi na wabunifu mbalimbali wa kimataifa na nyota mbalimbali wa nchini Marekani Bi. Rosemary Kokuhilwa ajulikanaye kama Fashion Junkii.

Siku ya onesho warembo wataanza na safari ya kutembelea  kiwanda cha Bia Tanzania  (TBL) kilichopo Ilala Dar es Salaam ambapo watashuhudia mtiririko mzima wa upikaji wa bia na kujumuika na wafanyakazi wa kiwandani hapo kwenye chakula cha mchana.

Redd’s Original imeshiriki kikamilifu kwenye mashindano ya Miss Tanzania 2011 ambapo imefadhili zaidi ya vitongoji 35 na pia kama mdhamini mkuu wa Redds Miss Ilala, Redds Miss Temeke na Redds Miss Kinondoni.


SHABA YA WIZI YA MILIONI 400 YANASWA DAR
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limewataka wezi wa madini ya shaba na wasafirishaji wa bidhaa kinyume cha sheria wajisalimishe wao wenyewe.  Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini hapa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova alisema kuwa ameweka mtandao wenye vikosi maalum kwa ajili ya kuwashughulikia wezi hao. Kamanda Kova alisema mpaka sasa wanamshikilia mfanyabiashara mmoja (jina limehifadhiwa) kwa uchunguzi zaidi) baada ya kukamatwa na madini ya shaba yenye thamani ya Sh. milioni 400 ambayo yalikuwa yanasafirishwa kutoka Zambia kwenda katia bandari ya Dar es Salaam. Aidha, Kova alisema wizi huo unahatarisha uchumi wa nchi na kusababisha serikali kukosa mapato.

         SWALA YA IDD EL FITRI BUKOBA
Wakazi wa mkoa wa Kagera wakiswali swala ya Idd El fitri leo asubuhi mjini bukoba.

BREAKING NEWS: BASI LA CHAMPION LAPINDUKA LAUWA WATU 8,68 WAJERUHIWA

 Basi la champion likionekana katika picha namna lilivyopinduka matairi juu.
 Kamanda Zerote steven alifika eneo la ajali na kutoa ufafanuzi wakati akihojiwa na vyombo vya habari.
 Ajali hiyo ilitokea mnamo saa 8:00 mchana, katika kijiji cha Nala wakati basi hilo likitoka Mwanza kuelekea jijini Dar es Salaam na kwamba, majeruhi 53 wamelazwa katika hospitali ya mkoa Dodoma.
  Eneo hilo la ajali ni kilomita 15 kutoka Dodoma mjini na Kamanda wa Polisi mkoani hapa Zelothe Stephen amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, lakini akasema, uchunguzi kuhusu chanzo cha ajali hiyo unaendelea.
  Hata hivyo, kamanda Stephen alisema taarifa za awali kutoka kwa mashuhuda zinaeleza chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva ambaye alishindwa kulimudu gari hilo baada ya kukutana na tuta ghafla.



STELLA MBUGE KURUDISHA HESHIMA YA KINONDONI!?!
 Stella mbugi katika pozi.Miss Kinondoni 2011 mwenye ari ya kurudisha record ya Miss Kinondoni kuchukua Taji la Miss Tanzania enzi za akina Richa Adhia,wema sepetu,Nancy Sumary nk.
                                               
Hamisa Hassan.
       
Husna maulid nae yumo,anatishia amani upade wa vipaji.
Msoimi wa chuo kikuu naye yupo kuwaonyesha namna gani atawafunika  warembo wenzake.
    Kitu cha Tabora hiki...kazi ipo mwaka huu...!
Ushindani ni mkali sana mwaka huu kwani mamiss wengi kama wanafanana sana vigezo,kazi kwa majaji.


BEIBER APATA AJALI
0830_justin_bieber_car_arrow_EXP
Justin Bieber and his super-expensive Ferrari are both doing OK after the singer was involved in a minor fender bender in L.A. today ... this according to the LAPD.
According to police, a driver in a Honda collided with a Ferrari driven by Bieber.
Sources on the scene tell UNIQUEENTERTZ ... the Honda "tapped" Biebs so gently he didn't exchange info with the other driver.
But we're told one of Justin's peeps decided ... better safe than sorry ... and called police -- who showed up and said there wasn't enough damage to even take a report.
The good news is no one was injured. Even better news ... we're told Bieber doesn't own the Ferrari.




     LEO NI EID EL FITR

Leo ni sikukuu ya Eid El Fitr ambapo waislamu kote duniani wamekusanyika katika misikiti na kuswali mara baada ya kumaliza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, ikiwa ni moja ya nguzo tano za dini ya kiislamu. mara baada ya kumalizika mfungo wa mwezi wa ramadhan waislamu hufanya ibada na kusherehekea kwa mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukumbushana mambo muhimu yanayohusu dini ya kiislamu. Kama wanavyoonekana katika picha ni waumini wa dini ya kiislamu wakiswali katika msikiti wa Mtoni kwa Kabuma wilayani Temeke jijini Dar es salaam.


KARIBU TANZANIA(SERENGETI NATIONAL PARK)
                            Tembo na misafara yao,inasemekana tembo huwa na kilo zaidi ya 11,000 akikomaa.               Twiga  a.k.a Girafe.            Kiboko na wenzie' basi tuwaite Viboko kwasababu wako wengiau vibokoz wakifurahia mbugani humo.                      Swala.               Ukungu, umande ni hali ambazo ni kivutio kikubwa maeneo ya mbugani               Katika eneo hili la Hotel ya Serena iliyozungukwa na maadhari ya aina yake ya kuvutia, kila utakachokitizama kitakuwa na mvuto kwa macho yako, ardhi, nyasi, miti, utunzaji wa mazingira ololooo!                The Ngorongoro Crater and the Ngorongoro Conservation Area are without a doubt some of the most beautiful parts of Tanzania, steeped in history and teeming with wildlife. Lango kuu kuingia Hifadhi ya Taifa Serengeti National Park A Word heritage Site.


CHRISS BROWN SPOTTED KISSING!




Did the media forget that Chris Brown has a girlfriend? He may want to bring her out more often.

Yesterday, he was spotted enjoying downtime in West Hollywood with Bow Wow, while kissing on what the media has pegged, ‘a mystery girl’, however it looks as though the mystery girl is actually his girlfriend ‘Karrueche’, sans her highlights and make up.

Tuesday, August 30, 2011

BREAKING NEWZ:AUWAWA KIKATILI BAADA YA KUKAMATWA KAIBA KUKU

                                           
  Marehemu NASIB pamoja na Kuku waliodaiwa kuwaiba na kumsababishia kifo
 Jeshi la Polisi likiwa limefika eneo la Tukio kuuchukua Mwili wa marehemu na kuupeleka katika hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya.


LELYA JUMA : MIMI NDIYE MISS TANZANIA
 Mrembo mwenye haiba ya pekee toka mkoa wa Rukwa Nyanda juu kusini amethubutu kusema yeye ndiye mshiriki mwenye vigezo zaidi kwani haoni upinzani wowote kambini hapo.
   Mrembo Leyla ana umri wa miaka 19 tu,ana elimu ya chuo akichukua masomo ya biashara,anapendelea kuogelea,kucheza muziki na kubadilishana mawazo na watu mbalimbali,
   Mbali na fani ya Urembo Leyla ana kipaji kikubwa cha kusakata kabumbu(soka),
   Namba yake ya ushiriki ni 1 mpigie kadri utakavojisikia kwani nia yake ni kuja na mambo mapya endapo atashinda taji la Miss Tanzania 2011.



KANDA YA ILALA YATISHIA MISS TANZANIA
                                                                                                                                           
Jennifer kaolaki(kushoto),Alexia William(kati) na Salha Israel(kulia)
Washiriki wanaowania taji la Miss Tanzania 2011 tokea kanda ya Ilala wakionyesha makali yao katika picha kuwa hawana mpinzani katika shindano hilo.
 Tunampongeza Jackson Kalikumtima (mwaandaji wa Ilala zone) kuleta warembo wakali wenye vigezo vinavyotishia amani kwa warembo wengine katika kinyang'anyiro hiko ambacho fainali zake ni tarehe 10.


MCHEZA KIKAPU AKAMATWA AIRPORT
Former NBA player Javaris Crittenton has been arrested after trying to board an airplane in Orange County, CA.
Crittenton had checked in for a flight to Atlanta last night, where his lawyer said he was going to surrender in a murder case. He was taken to an L.A. police station and booked on suspicion of being a fugitive from justice, the FBI confirms to the
Washington Post.
Javaris, who played for the Washington Wizards, was wanted for murder in the shooting death of 22-year-old Julian Jones.

BREAKING NEWS: MAUGO ATANGAZA KIFO CHA CHEKA


   Bondia Adam Maugo amejitapa kumtoa roho bondia mwenzake Fransis Cheka ulingoni Idd pili y a kesho kutwa.
     Maogo amekuwa akijitapa mara kadhaa kwenye vyombo vya habari kuwa haendi kupigana bali anaenda kumuua Cheka ulingoni.
         Mbali na hivyo Maugo ambe ni mwanajeshi mstaafu amepewa ma MP toka JWTZ  ambao watampa ulinzi siku hiyo ambayo atamfirigisa cheka ulingoni.


MISS LINDI AWA VODACOM MISS SPORTS LADY 2011 
Vodacom Miss Sports Lady, Loveness Flavian akipongezwa na warembo wenzake wa Vodacom Miss Tanzania waliofanikiwa kuingia tano bora ya kuwania taji hilo la michezo baada ya mwenzao huyo kutajwa kuwa ndiye mshindi na anakuwa mtrembo  wa tatu kuingia katika hatua ya Nusu fainali
Vodacom Miss Top Model, Mwajabu Juma (katikati) ambaye alikuwa mrembo wa kwanza kuingia hatua ya Nusu Fainali ya Vodacom Miss Tanzania 2011.


NDOA YA BEENIE MAN NA D'ANGEL'S VIPANDEVIPANDE
beenie_man_divorce_split_d_angel_marriage_photos.jpgWell-renowned Dancehall power couple, Moses "Beenie Man" Davis and Michelle "D'Angel" Downer seem to be heading their separate ways after Beenie revealed on TVJ's Entertainment Report this past weekend that divorce papers have indeed been sent out and that the two are separating.
The couple's marriage has endured various trials and tribulations and endless speculation regarding possible infidelity by both parties amongst other rumors. Beenie and D'Angel previously separated in 2007 but reconciled shortly thereafter and all seemed normal within the Davis household. However, the "King of the Dancehall" now insists that their most recent break-up could be permanent. "Yeah, divorce papers send, mi nuh kno if it sign.” Additionally, he claimed that D'Angel told him to disappear from her life and intimated that the two haven't spoken within the last two weeks. "Divorce a divorce man, that how it goes man, you move on. In life, you have to adapt and adjust, when yuh adjust in life, yuh haffi jus move on, yuh a big man," he intimated.


 
BOBY WINE AFUNGA NDOA

 Msanii Robert Kyagulanyi a.k.a Bobi Wine kwa sasa ni husband halali wa Barbara Itungo, ndoa yao ilifungwa weekend hii ilyopita nchini uganda. 

Monday, August 29, 2011

REDD'S YATOA ZAWADI EL-FITRI KWA AKINA MAMA WAZAZI HOSPITALI YA MWANANYAMALA

Jenifer kakolaki,mshiriki wa Miss tanzania akimbembeleza mtoto
 Warembo wakimsikiliza Mganga mkuu katika hospitali ya mwananyamala jijini Dar.
Mrembo akisaini kitabu cha wageni kwa niaba ya warembo wenzake.
 Miche ya sabuni na nepi kwaajili ya watoto wachanga waliozaliwa, zawadi hizo zilikabidhiwa hospitalini hapo na warembo kupitia kinywaji cha REDD'S.
Mrembo akionyesha upendo kwa mama na mtoto.
Salha Israel akimbeba mtoto mchanga kwa furaha wodini hapo.
Ni upendo wa hali ya juu sana kwa warembo wa Miss Tanzania kuonyesha ushirikiano na watu tofautitofauti katika jamii yetu,hii imekuwa ikiwezeshwa na Redd's kinywaji murua.
Mrembo toka Tanga akishangaa mtoto alietoka kuzaliwa kama dakika kumi zilizopita,mi kupita REDD'S utatambua haya.
Brand Manager wa REDD'S ,Victoria akiongea na waandishi wa habari nia ya kutoa zawadi hizi kwa wamama waliojifungua miche ya sabuni na nepi kwaajili ya watoto wao wachanga.
Miss tanzania Geneviev Mpangala akiongoza warembo hao ambao walikuwa katika picha ya pamoja na madaktari wa hospitali ya Mwananyamala jijiniDar.
Ziara ilisitishwa kwa picha hii,pongezi REDD'S kuwafikia akina mama waliojifungua kipindi hiki cha Idd.


MAAZIMISHO YA MIAKA 47 YA JESHI LA WANAMAJI
 Wanajeshi wakionyesha wananchi namna ya kujiokoa na boya.
 Jinsi ya kuokoa mtu aliezama katika maji mengi.
Tukio hili lilikuwa likifanyika maeeneo ya kivuko cha kigamboni ambapo wakazi na wavuka boti walipata elimu hii leo.



NAIBU SPIKA MH. JOB NDUGAI AONGELEA UVUMI AMBAO UMEZAGAA KUHUSU KUTOFAUTIANA NA SPIKA WAKE

Mh. Anna Makinda (Spika)
Mh. Job Ndugai (Naibu Spika)
     Taarifa ambayo imeibuka kuhusu Spika na Naibu Spika kutofautiana kuhusu maamuzi ya kuunda Kamati maalum ya kumchunguza Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Ndg. David Jairo si ya kweli.
     Mh. Job Ndugai ameyaongea haya katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM cha leo na amekana huo ni uvumi tu wa watu ambao wasiolitakia mema taifa letu na wasioutakia mema ushirikiano wao mzuri ambao wanao yeye na Mh. Spika Anna Makinda, na vile vile Mh. Ndugai alilielezea pia uvumi ambao watu wameuzusha kuhusu yeye kuonekana ana nguvu zaidi ya Spika Anna Makinda; Mh. Ndugai amekana hilo na kusema ni maneno tu yale yale! ambayo watu wasioutakia mema ushirikiano wao na kusema kwamba Mh. Spika Anna Makinda anamuamini sana na anamtuma katika shughuli nyingi tu ambazo ni muhimu lakini anaenda yeye Mh. Job Ndugai.     Clouds Fm walimuuliza maswali mawili matatu naye akayaongelea kwa ufasaha na kutaka wananchi waelewe hivyo anavyosema yeye, kuliko kusikiliza watu ambao wanazusha tu mambo ambayo sio mazuri.




AMBER ROSE NA WIZ KHALIFA WALIVYOTINGA MTV AWARDS

Wiz Khalifa and Amber Rose were the perfect couple on the Black Carpet at the 2011 MTV VMAs held at the Nokia Center in California.
Amber Rose told the world that the only thing she's looking forward to is her man Wiz Khalifa winning Best New Artist!


Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala akimsikiliza Bibi Mawazia Kibwana , mkazi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, akitoa malalamiko kwa Mbunge wake juu ya kitendo cha kubomolewa choo chake na Mwekezaji Raia wa kigeni na kuzungusha uzio uliofikia  upenuni mwa makazi yake. Mbunge huyo alitembelea kitongoji hicho mwishoni mwa wiki kujionea hali halisi ya mgogoro wa ardhi uliopo kijijini hapo.
 Makala akiongozwa kuangalia uzio uliowekwa na muwekezaji huyo na kuzua mgogoro wa ardhi wa kugombea mipaka na wanakijiji. Kushoto ni walinzi wa mwekezaji huyo.