Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, August 15, 2011

BREAKING NEWS: JOSE CHAMELIONE ABADILI DINI AITWA GADHAFFI

Chamelione akibatizwa jina la Gaddafi

    Msanni toka Uganda Joseph Mayanja  a.k.a Jose Chameleone ameonekana msikiti wa Kibuli Ijumaa ya August 12,2011 akiwa amevaa mavazi ya dini ya kiislam na kubadadili dini
Chameleone alifuatana na  wanachama toka Eagles Production members Haruna Mubiru na Grace Sekamate na baada ya kuingia kwenye dini ya Kiislam ametaka atambuliwe kama Gadhaffi Chameleone na si Jose Chameleone kama alivyojulikana awali na baadaye alisali sala ya Ijumaa na waumini wengine.


SUPER D IN STORE NOW!
DVD ZA MAPAMBANO YA NGUMI KIMATAIFA SASA ZINAPATIKANA KWA WINGI BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM.



WATU 18 WAJERUHIWA AJALI YA LOLI NA BASI HUKO LINDI
Zaidi ya abiria 18 walikuwa wakisafiri kwa basi la kampuni ya Country Express lenye namba za usajili T 806 AVM wamejeruhiwa vibaya na kunusurika kifo baada ya basi hilo kugongana uso kwa uso na Lori katika eneo la kijiji cha Mnimbila, wilaya ya Lindi vijijini, mkoani Lindi.
Ajali hiyo imetokea jioni ya leo Jumapili na majeruhi wote wa ajali hiyo hali zao ni mbaya na wameondolewa katika hospitali ya mkoa wa Lindi na kupelekwa Hospital ya Rufaa ya Nyangao kwa matibabu zaidi.

 KUCHELEWA KUWALIPA MAPEMA NASRI NA FABREGAS ITAWAGHARIMU ARSENAL

Alex Song akiwania mpira na Gabriel Obertan
Huku wakiwa na mengi ya kuyafanyia kazi ili kufikia pale ambapo mashabiki wao wanatamani kuona timu yao ikifika, Arsenal walijikuta wakianza kwa kasi ndogo baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Newcastle United .
Siyo vigumu kuona Arsenal walipojikwaa na kushindwa kupata ushindi mbele ya Newcastle Utd.Moja kwa moja mzigo wa lawama hauna budi kubebwa na Arsene Wenger.

No comments: