Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, November 27, 2013

MKURUGENZI WA GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL ASHUHUDIA MAZOEZI YA WASHIRIKI WA TTM

Mkurugenzi wa Giraffe Ocean View Hotel Bw. Dr.Charles Bekoni(katikati) akishudia mazoezi ya washiriki wa Tanzania Top Model 2013 pindi alipotembelea sehemu wanapofanyia mazoezi wanamitindo hao ndani ya hoteli hiyo.
washirki wakipiga jalamba la mazoezi ya nguvu kujinoa na fainali zitakazofanyika hivi punde.

...Video: Justin Bieber – ‘All That Matters’ [Teaser]...

Justin Bieber
Justin Bieber lowers the lights and goes in for a kiss in the steamy video for “All That Matters,” the second release in his #MusicMondays series. The 19-year-old heartthrob makes out with his sexy co-star in the clip, which was shot earlier this month in L.A.
“What’s a king bed without a queen?” he asks. “You’re all that matters to me.”
The full video will premiere on December 2, while his Believe movie hits theaters on Christmas Day.
Watch the Biebs serenade his lady in the teaser below.
 VIDEO

TLC and Lil Mama Perform ‘No Scrubs’ on ‘Dancing With the Stars’...

TLC and Lil Mama
A day after their return to the American Music Awards, TLC took over the ballroom on “Dancing With the Stars.” Standing on a glittery platform, T-Boz and Chilli performed their 1999 hit “No Scrubs” while the finalists danced the samba. They were once again joined by Lil Mama, who rocked green hair and stepped in sync with her idols.
TLC is working on a new album for release in 2014 featuring contributions from Lady Gaga and Dallas Austin.
 video

steve RnB amvisha pete ya uchumba mpenzi wake

steve rnb engaged 2Ni jambo la kawaida kwa wasanii wa bongoflava hasa wakubwa kama steve RnB kutembea na kila demu mzuri hapa bongo.lakini kwa steve ni tofauti kabisa kwani amefanikiwa kumvisha pete ya uchumba high school sweetheart wake.Rumour has it kwamba steve RnB na huyu mrembo wametoka mbali na wamekuwa wapenzi wa
muda mrefu hadi wameshawahi kufukuzwa shule pamoja.tunamtakia Steve RnB safari njema ya kuelekea katika ndoa

Mabomu, risasi vyarindima Kivule"ILALA"


Waendesha bodaboda 13 wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kuendesha mauaji dhidi ya watu wanaodaiwa kuwa ni wezi wa pikipiki katika mtaa wa Kivule Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Mbali ya waendesha bodaboda hao, pia pikipiki 17 zilikamatwa na polisi kwa tuhuma kama hizo jana.

Hata hivyo, kazi hiyo haikuwa rahisi kwani polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi pamoja na risasi za moto kukabiliana na waendesha pikipiki zaidi ya 100, hali iliyozua mtafaruku mkubwa kwa wakazi wa mtaa huo na viunga vya jirani.


Kabla ya  tukio hilo, madereva wa bodaboda walijikusanya kwa ajili ya kuendesha msako wa nyumba kwa nyumba baada ya kupata majina ya mtandao wa wezi wa pikipiki katika mtaa huo na maeneo ya jirani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Marietha Minangi, alisema kuwa hatua kali zimechukuliwa na jeshi hilo baada ya waendesha bodaboda hao kujichukulia sheria mkononi ya  kuwaua watu waliokuwa wakiwakamata.

Kamanda Minangi alisema msako huo utaendelea kwa kuwa waliojitokeza katika mauaji hayo ya kinyama walikuwa ni wengi.

“Nawasihi waendesha pikipiki kama wanahitaji biashara wafanye biashara, vinginevyo waache mara moja vitendo vya kihalifu kwa kuwa tunaendelea kuwasaka hadi kieleweke,” alisisitiza Kamanda Minangi.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule, Joseph Gassaya, alisema kuwa mtaa wake ulivamiwa na vitendo vya uhalifu yakiwamo mauaji ya vijana wawili.Gassaya alifafanua kuwa vijana hao waliuawa na madereva wa bodaboda kutokana na kuwahisi kuwa ni wezi.

"Nikiwa kiongozi wa mtaa huo, nafahamu kuwa matukio ya mauaji yamekuwa yakitokea mara kwa mara ikiwamo waendesha bodaboda wanne kuuawa na kuporwa pikipiki zao na taarifa zinatolewa polisi," alisema.

“Pengine vijana hao wameamua kuchukua sheria mkononi baada ya kuona taarifa zao hazifanyiwi kazi ipasavyo, bila kujua kuwa jeshi hilo linachukua hatua baada ya kuthibitisha,” alisema.

Naye mmoja wa waendesha bodaboda hao ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema kuwa wameshangazwa na kitendo cha polisi kutumia nguvu kupita kiasi.

Alisema taarifa za kuporwa pikipiki na kunyongwa kwa wenzao wanne, alitoa taarifa katika kituo cha Polisi Stakishari, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa kuwasaka wahalifu hao.

“Sielewi kama waendesha pikipiki waliokufa hawakuwa watu. Kwa nini hao wezi waonekane kuwa wana haki zaidi...Jeshi lipo kwa ajili ya raia wote si kwa baadhi ya watu,” alisema.

Alisema kabla ya kutekeleza zoezi hilo, waliweka mtego kwa mtu waliyemhisi kuwa ni mwizi na aliponaswa mmoja wao, aliwataja wenzake wote aliokuwa akishirikiana nao kuiba pikipiki.

Aliongeza kuwa Jeshi la Polisi halipendi kutoa ushirikiano kwa kuwa matukio ya mauaji yameripotiwa lakini hakuna hatua zilizochukuliwa, jambo lililowaudhi na kuamua kujichukulia sheria mkononi ili kujihami.

Sunday, November 24, 2013

BACK TO BACK MAZOEZI YA TANZANIA TOP MODELS 2013

Mazoezi haya yanafanyika katika Hoteli ya Giraffe Ocean view iliyopo Jijini Dar.

CIARA ALIVYOTOKELEZEA KWENYE GQ

Ciara
Ciara is bringing her “Body Party” to the pages of GQ. Future’s fiancée flaunts her smoking-hot body in a series of provocative photos for the men’s magazine. In the black-and-white images shot by Gomillion & Leupold, the 28-year-old singer sports a fishnet top with nothing underneath, clenching her breasts with her hands. She shows off her glistening legs and exposes some boob in a white crop top and cutoff denim shorts.
In the interview, CiCi chats about her new single “Overdose” and offers some dancing and style tips to the fellas.
On “Overdose”: “The song’s got a throwback ’80s vibe with a modern twist; I think that’s unexpected. It’s more a product of my experimentation—it has a vintage-y feel, but I feel like everyone can love it.”
On dancing: “Go with the flow; don’t overthink it. If you’re a head-nod kind of guy, nod your head. If you’re a guy who likes to coast out and rock or sway, just do that. Whatever you do, don’t get out there and try do something you haven’t practiced. Do what shows your style and vibe—let me catch that without you trying to show me anything.”
On her style advice for guys: “I love when people have their own creative vision, when a person stands out and tries different things. I also think less is more. A T-shirt and some Balmain jeans or even just simple jeans can still look nice—it can be powerful, too.”
See more photos from her stunning shoot below.

Ciara
Ciara

JACKY WA MAISHA PLUS AHUSISHWA NA MAPENZI YA JINSIA MOJA

MREMBO aliyeshiriki Shindano la Maisha Plus Season 2, Jacqueline Dunstan ‘Jack wa Maisha Plus’ amezua jambo katika mtandao baada ya kutundika picha akiwa anabusiana na mwanamke mwenzake.
Jack ambaye kwa sasa yupo nchini Dubai, aliweka picha hiyo katika mtandao wa Instagram hali ambayo iliwashangaza wadau wengi waliopo kwenye mtandao huo ambapo walimchana kuwa aache vitendo vya kisagaji lakini mwenyewe hakujibu.
Jack baada ya kuweka picha hiyo aliandika maneno haya; ‘mwaaah’ ndipo wadau walipoanza kumshambulia na kumtaka aondoe picha hiyo chafu.

P SQUARE WATEMBELEA WATOTO WENYE ULEMAVU JIJINI DAR

Mkuu wa Kitengo cha Vodacom Foundation, Yesaya Mwakifulefule wakipeana mikono na wasanii kutoka nchini Nigeria maarufu kwa jina la P Square (Peter na Paul Okoye), wakati walipotembelea kituo cha watoto wenye ulemavu wa Utindio wa Ubongo cha Msimbazi Mseto jijini Dar es Salaam, ambapo wasanii hao walitoa msaada kwa watoto hao wenye ulemavu huku ikiwa ni njia moja ya kushiriki kazi ya kijamii.

Rais JOYCE BANDA wa Malawi aanzisha tena chokochoko na Tanzania...Sasa adai kuwa Mkoa wa RUVUMA na wananchi wake wote ni Mali yake


RAIS wa Malawi, Joyce Banda ametajwa kuendeleza chokochoko baina ya nchi yake na Tanzania, huku sasa akidaiwa kutumia redio na runinga za nchini mwake kutangaza kuwa mkoa wa Ruvuma, viongozi na wananchi wa ukanda wa Ziwa Nyasa ni mali yake.
Aidha, amesitisha safari za meli ya mv Ilala iliyokuwa ikifanya safari kwenye Ziwa Nyasa kusafirisha mazao na wananchi wa ukanda huo upande wa Tanzania.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa soka wa Mbambabay jana, Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba, alisema Rais Banda ambaye aliibua upya mzozo wa mpaka baina ya nchi hizi mbili, kuwa ni mkorofi kutokana na kufanya vitendo vinavyoonesha uhusiano baina ya nchi hizi mbili kuzorota.
Komba alibainisha vitendo hivyo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akisema imefika mahali Rais Banda anapotosha ukweli kuhusu mpaka kati ya nchi hizo mbili na kudai sehemu ya mwambao wa Ziwa upande wa Tanzania ni yake.
Mbunge huyo alisema jimbo la Mbinga Magharibi ambalo ni Wilaya ya Nyasa, wanasikiliza matangazo ya redio za Malawi, na anazitumia kupotosha umma kuwa ukanda wa Ziwa Nyasa ni mali yake na wananchi wanaamini hivyo.
Rais Banda anatangaza kupitia vyombo vya habari vya nchi yake ambavyo vinasikika vizuri katika wilaya hiyo kutokana na wilaya ya Nyasa kutopata mawasiliano ya redio na runinga za nchini.

 Komba alisema kutokana na wilaya hiyo kukosa mawasiliano ya vyombo vya habari, wananchi wake wanakosa kusikiliza matangazo zikiwamo hotuba za viongozi wa Taifa.

Wananchi wanakosa kusikiliza matangazo zikiwamo hotuba ya Rais Kikwete ya kila mwezi na hotuba za viongozi wengine wa kitaifa wakiwamo Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.
“Kutokana na kukosekana usikivu huo, Rais Banda anatumia nafasi hiyo kutangaza kuwa viongozi wote wa wilaya na mkoa na eneo lote ni mali yake,” alisisitiza Komba.

  Aliongeza kwamba watu wote walioko kwenye mkutano huo isipokuwa Katibu Mkuu Kinana, akiwamo Dk Asha-Rose Migiro ambaye alizaliwa Mbambabay wote ni mali ya Rais Banda.

Mbunge huyo alisema wananchi wa eneo hili nao ni Watanzania wanaostahili kusikia na kupata habari za nchi yao, badala ya kusikiliza nyimbo na matangazo ya Malawi ambayo yanakuwa na ajenda zake.
Mbunge Komba alimwomba Katibu Mkuu Kinana kwenda kuhimiza kutekelezwa haraka kwa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ya kuleta meli ili kuwa na usafiri wa uhakika wa mali na wananchi katika eneo hilo.
Kinana alisema ahadi ya meli ya Rais, hiyo ana uhakika itatekelezwa na kufafanua kuwa meli tatu zinatengenezwa Korea Kusini na zitakapokamilika ya Ziwa Nyasa itapelekwa kutoa huduma.
Alisema baada ya Banda kuondoa meli hiyo wananchi wa Mbambabay wanatumia boti dogo kusafirisha abiria na mizigo, hali ambayo inatia shaka.
Kinana alisema amesikia kilio cha Mbunge Komba, kwamba ahadi ya Kikwete itatekelezwa ili kuwapa wananchi usafiri wa meli, ingawa itatumia muda kutokana na kuhitaji muda mwingi kubuni na kutengeneza.

TAARIFA YA ZITTO ZUBERI KABWE (MB) YA LEO KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHADEMA


1. Utangulizi Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 - 22 Novemba 2013, Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. 

Kwa mujibu wa taarifa ya chama iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana kama mkakati wa uchaguzi 2013.
 
 Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha Kamati Kuu . Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. 

Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa Taifa. Nitazianisha tuhuma hizi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vyama.
 
Ninatambua kwamba chama changu kinapita katika wakati mgumu sana sasa hivi. Nataka nitamke mapema sana kwamba mimi Zitto Zuberi Kabwe sitokuwa chanzo cha CHADEMA kuvunjika. 
Hiki ndicho chama kilichonilea na kunifikisha hivi nilivyo. Ningependa chama hiki mtoto wangu atakapokuwa mtu mzima na atakapoamua kujiunga na siasa aingie CHADEMA. 
Bado nina imani kubwa na chama changu na ninaamini ndicho kinachostahili kuendesha nchi jana, leo na kesho. 
 
2. Kuhusu tuhuma mbalimbali zinazo elekezwa kwangu Zipo tuhuma nyingi ambazo zimekuwa zikirudiwarudiwa katika vikao vya chama na nje ya vikao na baadhi ya viongozi wenzangu.
 Tuhuma hizi zinalenga kuonyesha kwamba mimi ni mbinafsi na kwamba ninapokea rushwa ili kukihujumu chama changu. 

Nitazianisha tuhuma kwa kifupi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vya chama. 
 
i) Tuhuma kwamba sikushiriki kumpigia kampeni mgombea wetu wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2010. Ningependa kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:
  • Mimi nilikuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Kaskazini huko Kigoma.
  • Pamoja na kuwa mgombea wa ubunge, nilifanya kampeni katika majimbo mengine 16 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dar es Salaam, Mtwara, Pwani, Shinyanga, Mara na Rukwa. Hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyefanya kampeni katika majimbo mengi kama mimi, ukiacha mgombea urais.
  • Kote nilipopita nilimpigia kampeni wagombea wetu wa udiwani, ubunge na Rais.
  • Katika Mkoa wa Kigoma nilizunguka na mgombea urais katika kata zote za Kigoma Kaskazini na majimbo yote manane ya Mkoa wa Kigoma.

ii) Tuhuma kwamba katika Mkoa wa Kigoma nilishindwa kuwapigia kampeni wagombea wetu kiasi kwamba peke yangu ndiye niliyeshinda katika uchaguzi huo. Ukweli ni kwamba niliwapigia sana kampeni wagombea wetu, na hivyo ndivyo wapiga kura wa Kigoma walivyoamua. 
 
iii) Tuhuma kwamba nilishiriki kuwashawishi wagombea wetu katika baadhi ya majimbo kujitoa katika uchaguzi wa mwaka 2010 ili kuwapisha wagombea wa CCM wapite bila kupingwa kwa njia ya rushwa. Majimbo yanayotajwa ni pamoja na Sumbawanga, Musoma Vijijini na Singida Mjini.
 Kama nilivyokwisha kueleza katika vikao mbalimbali vya chama jambo hili si la kweli na hakuna popote ambapo watoa tuhuma hizi wamewahi kutoa ushahidi kwamba nilifanya jambo hili. 

Nipo tayari kwa uchunguzi ndani ya chama na watoa tuhuma waje na ushahidi bayana wa jambo hili. Si afya kwa chama kuendelea kurudiarudia tuhuma hizi kila mara tangu mwaka 2010 bila uchunguzi wowote kufanyika na jambo hili lifikie mwisho. 
 
iv) Tuhuma kwamba nimekuwa sishiriki katika operesheni mbalimbali za chama: Ukweli ni kwamba nimeshiriki sana katika operesheni mbalimbali za chama ndani na nje ya nchi. Kwa mfano, mwaka 2011 tulikuwa na operesheni kubwa katika mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na nilikwenda katika mikoa yote tuliyotembelea.
 Mwaka 2012 baada ya hoja ya mkonge bungeni nilifanya ziara Mkoa wa Tanga. Mwaka 2012 kulikuwa na operesheni kubwa moja katika mikoa ya kusini ya Mtwara na Lindi. Operesheni hii sikushiriki kwa sababu nilikuwa nchini Marekani kufungua matawi kwa mwaliko wa Watanzania wanaoishi huko. 
 
v) Tuhuma kwamba nimekidhalilisha chama kwa tamko la PAC kwamba Hesabu za Vyama hazijakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG): Katika jambo hili ninatuhumiwa kwamba mimi kama Naibu Katibu nilipaswa kuwasiliana kwanza na viongozi wa chama 'kuwatonya' ili wajiandae. 

Kwamba kutokuwatonya kumekidhalilisha chama na kukiweka kundi moja na CCM na nastahili kuadhibiwa vikali kwa kuwa katika taarifa yangu nilikuwa na nia mbaya na chama chetu. Maelezo yangu niliyoyatoa na ambayo ningependa kuyakariri hapa kuhusu jambo hili ni kama ifuatavyo:
  • Utawala bora hautaki mimi kutumia nafasi yangu ya uenyekiti wa PAC kulinda chama changu na kuonea vyama vingine. Kufanya hivyo ni kuendeleza tabia zile zile ambazo tunazipinga na ambazo tunapigania kuzibadilisha
  • Napenda kusisitiza kwamba hakuna chama ambacho kimewahi kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Natambua kwamba mahesabu ya chama changu yamekuwa yakikaguliwa na wakaguzi wa nje kwa utaratibu tuliojiwekea. Lakini matakwa ya kisheria ni kwamba mahesabu ya vyama vya siasa hayajakaguliwa na CAG, na hili ni kosa la kisheria, bila kujali kosa hili ni la nani.

vi) Tuhuma kwamba mimi ni mnafiki katika kukataa kwangu kuchukua Posho za Vikao Mtakumbuka kwamba mimi nilikataa kuchukua posho tangu mwaka 2011 kama ishara ya kuonyesha kwa vitendo msimamo wa chama chetu wa kupinga posho za kukaa na matumizi mengine yasiyofaa katika fedha za umma kama ilivyoanishwa kwenye Ilani yetu ya mwaka 2010-2015. Mtakumbuka kwamba hivi karibuni Mheshimiwa Lema amenishutumu kwamba kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki kwa sababu ninapokea posho kubwa zaidi katika mashirika ya umma ambapo mimi ni mwenyekiti wa kamati husika. Ninapenda kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:
  • Sipokei posho yeyote ya vikao (sitting allowance) ndani na nje ya Bunge tangu mwaka 2011. Hii ni pamoja na vikao vyote katika Kamati za Bunge ninavyohudhuria. Mtu yeyote mwenye ushahidi vinginevyo auweke hadharani.
  • Swala la kukataa posho (sitting allowance) ni swala la kiilani katika chama chetu, na kwangu ni swala la kimisingi zaidi. Katika Wilaya yangu vifo vya kina mama wajawazito ni 1900 kati ya wanawake 100,000 wenye ujauzito. Vifo hivi vinatokana na ukosefu wa huduma kwa sababu ya bajeti finyu. Ndiyo maana nilifurahi sana kwa chama chetu kuliweka swala la kupunguza matumizi ya Serikali katika Ilani, na kuondoa posho za wabunge, ambao tayari wanapokea mishahara mikubwa, kungesaidia sana kupatikana fedha ambazo zingeokoa vifo vingi vya kina mama.
  • Jambo hili si suala la ugomvi baina yangu na Mheshimiwa Lema. Ni suala la msingi katika chama chetu.

3. Usambazaji wa Ripoti ya Siri kuhusu Zitto Kabwe Hivi karibuni kulisambazwa waraka unaoitwa ripoti ya siri kuhusu mimi ukibeba lundo la tuhuma kwamba nimehongwa fedha nyingi ili kukihujumu chama changu. Waraka huu ulidaiwa kuwa umechomolewa kutoka makao makuu ya CHADEMA. 
Jambo hili pia lilijadiliwa katika kikao cha juzi kwa kifupi, na majibu ya viongozi wa chama ilikuwa ni kwamba waraka huu haukuandaliwa wala kusambazwa na makao makuu. Katika mchango wangu nililalamikia mambo matatu yafuatayo:
  1. Kwamba baadhi ya waliokuwa wanasambaza waraka ule walikuwa ni viongozi wa chama chetu. Bahati mbaya hadi leo hakuna hata mmoja ambaye amekwishachukuliwa hatua za kinidhamu. Ninaamini kwamba kuna siku watu hao watachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za chama chetu.
  2. Kwa kuwa chama kimekana rasmi kuhusika na waraka huu, nitaendelea na taratibu za kisheria ili kuhakikisha kwamba wote waliohusika kutengeneza hekaya ile wanachukuliwa hatua stahiki za kisheria.

4. Hitimisho Ninatambua kwamba kuna watu walitegemea leo ningejibu mapigo na ningewazodoa watu kwa majina kama ilivyo kawaida katika siasa za Tanzania.
 Natambua pia kwamba, kama ilivyo kawaida wakati wa migogoro katika vyama vya siasa hapa Tanzania, kuna watu walitegemea leo ningetangaza 'maamuzi magumu'.

 Natambua kwamba wapo ambao wangependa kupata nafasi ya kuendelea kutumia suala hili katika harakati zao za kudhoofisha mapambano ya demokrasia na uthabiti wa siasa za ushindani nchini mwetu. 

Napenda wanachama wa CHADEMA na wapenda demokrasia na siasa safi wote nchini watambue kwamba mimi bado ni mwanachama mwaminifu wa chama hiki na nitakuwa wa mwisho kutoka kwenye chama hiki kwa hiari yangu. Nitafuata taratibu zote ndani ya chama katika kuhitimisha jambo hili.
 
Naomba wanachama waelewe kwamba mimi kama binadamu ninaumia ninapopigwa. Tuhuma ninazorushiwa ni kubwa na zinanikwaza. Tuache siasa za uzushi ili tujenge chama chetu na nchi yetu, ili hatimaye tuwakomboe Watanzania wenye matarajio na imani kubwa kwa chama chetu.
 
Kama mwanasiasa kijana niliyekaa katika siasa kwa muda sasa yapo mengi mazuri nimeyafanya. Lakini kuna maeneo nilipojikwaa na yapo makosa niliyofanya kisiasa katika maisha yangu ya siasa.
 
Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina, waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka. 
 
Hii ni changamoto kubwa ndani ya chama chetu inayohitaji uongozi shupavu kuikabili. Nitasimama daima upande wa demokrasia. 
Kama alivyopata kunena mmoja ya wanasiasa maarufu, 'kiwango cha juu kabisa cha uzalendo katika nchi ni kukubali kutofautiana kimawazo', na ninatamani huu ndio uwe utamaduni wa chama chetu.
 
Kabwe Zuberi Zitto, Mb Dar es Salaam. 24 Novemba, 2013

KISANGA KISANGANI BLAZA: MBUNGE KAPUYA ADAIWA KUTOWEKA...POLISI WAMSAKA KWA UDI NA UVUMBA.


 
SIKU moja baada ya binti anayedaiwa kubakwa na kutishiwa kuuawa na Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), kufungua jalada polisi dhidi yake, inadaiwa mbunge huyo ametoweka nchini...
 
Vyanzo mbalimbali vilivyo karibu na mbunge huyo, vinadai kuwa amesafiri juzi kwenda nchini Sweden kwa masuala ya kikazi, na kwamba atakuwepo huko kwa muda usiopungua mwezi mmoja.
 
Chanzo kingine kimedokeza kuwa mbunge huyo alidai ametumwa kazi na kigogo mmoja serikalini na atakuwepo nchini Sweden miezi miwili hadi mitatu.
 
Hata hivyo haijajulikana kazi anayokwenda kuifanya Kapuya ingawa kuna taarifa safari hiyo imelenga kumtuliza na upepo mbaya wa kuandamwa na tuhuma za ubakaji ambazo zipo polisi hivi sasa.
 
Wakati Profesa Kapuya anakimbilia nje ya nchi, tayari alishafunguliwa jalada namba OB/RB/21124/13 katika Kituo cha Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam juzi.
 
Mtoa taarifa wetu anasema muda mchache baada ya Kapuya kushindwa kumshawishi binti huyo asimfungulie kesi ya ubakaji, wala kuogopa vitisho vya kuuawa, au kupokea pesa kiasi chochote aondoke nchini, Kapuya mwenyewe alipanga safari ya dharura na kwenda nje ya nchi.
 
Tanzania Daima  lilifanya juhudi za kuwasiliana na ofisi ya Bunge kujua kama wana taarifa zozote za kuondoka kwa mbunge huyo kwenda nje ya nchi na kujua ni sababu zipi hasa zimempeleka huko, lakini simu ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai ilikuwa inaita bila kupokelewa.
 
Katibu wa Bunge, Thomas Kashilila naye hakupatikana baada ya simu yake kuita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) hakuujibu.
 
Hata hivyo, Tanzania Daima Jumapili limedokezwa kuwa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu ambayo Kapuya ni mjumbe wake haina safari ya Sweden.
 
Tangu Tanzania Daima lianze kuandika tuhuma hizi nzito, kumekuwapo na kusuasua kwa mtuhumiwa huyo kutiwa hatiani na Jeshi la Polisi.
 
Harakati za kufungua jalada dhidi ya Kapuya zilianza juzi jioni na kuendelea hadi jana ambapo polisi walitumia zaidi ya saa 12 kumhoji binti huyo anayedaiwa kubakwa ili kupata ukweli wa sakata hilo.
 
Akiwa polisi, binti huyo alikutana na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi ya Oysterbay (OCD) na OC-CID wake na kutoa maelezo ya awali kabla ya viongozi hao kumruhusu ayaweke malalamiko yake katika maandishi kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka.
 
Polisi wanena
Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema watamtafuta Kapuya nchi yoyote atakayokwenda iwapo tuhuma dhidi yake zitathibitika.
 
Alisema Jeshi la Polisi lina mtandao mkubwa ndani na nje ya nchi, hivyo si rahisi kwa mtuhumiwa yeyote kuukwepa mkono wa sheria endapo itahitajika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
 
“Sisi tunashirikiana na polisi wa nchi mbalimbali duniani, ndiyo maana inakuwa rahisi kwa mtuhumiwa aliyetoroka nchi fulani kukamatwa nyingine na kurejeshwa kwao.
 
Nataka niwaondoe hofu wale wote wanaodhani polisi haiwezi kumkamata mtu akikimbia nchini, tuna mkono mrefu sana na hatufanyi kazi kinyume na taratibu zetu,” alisema.
 
Kamanda Wambura pia alikiri polisi kufungua jalada la Kapuya huku akiweka wazi kuwa kinachofanyika hivi sasa ni uchunguzi wa tuhuma zake.
 
Alisema miongoni mwa maeneo wanayoyafanyia uchunguzi ni kubaini kama ujumbe ulio katika simu ya binti anayedai kubakwa na kutishiwa maisha unatoka katika simu ya mbunge huyo.
 
“Tumefungua jalada, lipo kwa ajili ya uchunguzi na tukibaini kuwa ni nani anahusika na tuhuma hizo tutamsaka na kumkamata popote alipo,” alisema Wambura.
   Source: Tanzania Daima