Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Saturday, June 19, 2010

                         MISS TEMEKE JULY 9 (TTC) CHANG"OMBE
     Shindano la kumsaka nkimwana wa vodacom miss Temeke litafanyika july 9 nkatika ukumbi wa sgara (TTC) chang"ombe jijini Dar.
     Ben Kisaka mwanwa shindano hilo amesema mambo yote yamekalika alikadhalika washiriki wamefundwa na kufundishika wapo tayari kwa mchuano huo kuwania tiketi yakwenda miss Tz.

 MISS KINONDONI YAPAMBA MOTO
     Shindano la kumsaka nmlimbende wa Vodacom miss Kinondoni 2010 inatarajiwa july 2 jijini Dar ambapo warembo wqatapanda jukwaani kuwania taji hilo linaloshikiliwa na lulu  Ibrahim miss kinondoni 2009 .
      kambi ya miss kinomdoni imewekwa katika hoteli ya kisasa ya Giraffe ocean view  iliopo jijini Dar es salaam ambapo siku jana vilisakwa vipaji vya IQ,Michael Maulus alikuwa moja ya majaji wa mtanange huo.

 ANNA KIWAMBO AWA MISS TANGA 2010              
       Shindano la kumtafuta Miss Tanga 2010 lilifanyika Tanga Beach,SAHARE ambapo taji la miss tanga lilienda kwa  Anna Kiwambo,nafasi ya pili ilienda kwa  Jari Mure na ya tatu ilienda kwa Zuleha Mrisho.

     YALIOJILI MISS ILALA 2010
       Shindano la kumsaka miss ilala lililofanyioka june 26 ubungo plaza ambapo Bahati Chande alipotwaa taji hilo akilipokea toka kwa silvia shally.
       Mshindi wa pili alikuwa Consolatha lukas na nafasi ya tatu ilienda kwa Salma Mwakaluka.

   REDDS MISS ILALA VIPAJI KUFANYIKA KESHO JUNE 22 LAMADA HOTEL
       Shindano la kumsaka Redds miss ilala vipaji inatarajiwa kufanyika kesho nkatika hotel ya Lamada apartment iliopo maeneo ya msimbazi ambapo kambi ya zone hiyo imewekwa.
       Aidha itapambwa na vijana wa THT na burudani zingine ambapo kwa mwaka jana Redds miss ilala lilienda kwa mshindi wa tatu toka kitongoji cha ukonga(husna).
       Hii ni baada ya kurudi mafunzoni mkoani Tanga na kuudhulia ufunguzi wa mashindano ya magari na Miss tanga 2010.show itaanza saa tatu usiku.

        GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL  YATUNUKIWA  HADHI  YA  NYOTA  NNE(4 STAR)
Wizara ya  Maliasili na Utalii imezipandisha hadhi hoteli 66 katika mikoa wa es salaam na Pwani ambapo hoteli tatu tu zimepata hadhi ya nyota tano.
   Akizitunuku hadhi hoteli hizo jana Waziri wa Maliasili na Utalii Bi. Shamsa Mwangunga alizitaka kutumia mazao na bidhaa zinazozalishwa nchni ili kuzitangaza na kuinua pato la Taifa na kupunguza umasikini kwa wananchi wake.
    Bi Mwangunga aliingia mkataba wa ushirikiano na sekta binafsi katika kuendeleza sekta ya utalii ambapo aliitaka sekta hiyo kukabiliana na changamoto zinayoikabili sekta ya utalii nchini hususani utoaji huduma kwa watalii.
(PICHA1;Mkurugenzi wa giraffe ocean view hotel bwana Charles Bekon akipokea nyota toka kwa Waziri wa maliasili na Utalii Bi.Shamsa Mangunga. PICHA2: Wafanyakazi wa Giraffe hotel wakiwa na nyuso za furaha huku mkurugenzi Bwana Charles Bekon akiwa ameishika nyota hiyo na kulia kwake ni GM,kushot ni Bwana Chama).
    Giraffe ocean view hotel ni moja ya hoteli 66 zilizzopandishwa hadhi na kufikia hadhi ya ya nyota nne katika kutoa huduma,ambapo vigezo vya Afrika mzshariki ndivyo vilivyotumika kuipandisha Giraffe hotel ambapo wataalam waliobobea katika dulu hilo kuona inastaili kupanda hadhi.
    
   Giraffe hotel ni hoteli inayopatikanana Dar es salaam nchini Tanzania pembezoni mwa bahari ya hindi,africana beach off Bagamoyo road,pia ho0teli hii inasifika kutoa misaada ya kijamii kwa wananchi wa Tanzania na kudhamini matukio mbalimbali yanayohusu kutangaza utamaduni wa mtanzania eg;Miss Tanzania event ambayo inatoa ajira kwa vijana wengi pamoja na kulitangaza utalii wa taifa letu kimataifa kila maka.
   Hafla hiyo ilifanyika leo katika ofisi za wizara ya maliasili na utalii jijini Dar es salaam
giraffe@giraffeoceanviewhotel.dom ,p.o.box 33909,mobile +2550784145899,plot No. 169 moduli road.

                                          MISS MWANZA KURINDIMA KANDA YA ZIWA
             Shindano la kumsaka kimwana wa mkoa wa mwanza katika shindano kubwa nchini la Vodacom Miss Tanzania,mkoa wa mwanza imekuwa ni gumzo kwa watanzania wote ikiwa inatizamiwa kama historia itaendelea kuwekwa kwa mara ya tatu mrembo toka mwanza kunyakua miss Tanzania kwa mara ya tatu.
             Washiriki wa mkoa huo wameanza kutambniana kila mmoja akitumaini kuvunja rekodi ya miriam(queen of Tz) kwa mwaka huu ambapo june 25(miss mwanza) katika ukumbi wa yatch atajulikana nani atabeba bendera ya nkoa huo kuelekea Miss lake Zone ambayo itafanyika july 7 mwaka huu katika ukumbi wa yatch club jijini mwanza.
               Kampuni ya sisi Entertainment kupitia mkurugenzi wake bwana John Dotto amesema jumla ya washiriki 18 watapanda jukwaani kuwania taji la mkoa wa mwanza lenye sifa ya aina yake katika medani ya urembo nchini.


No comments: