Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, April 19, 2012

IDDI AZAN AMUUMBUA NAIBU WAZIRI WA MICHEZO

MBUNGE wa Kinondoni, Iddi Azan, (CCM), amemuumbua Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, kutokana na kutoa taarifa za kupotosha bungeni kuhusu timu zilizoshinda katika Kombe la Chalenji na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati.
Akitoa taarifa bungeni jana, mbunge huyo alisema, si kweli kwamba timu ya taifa, ilitwaa kombe hilo mara tano na timu za Simba na Yanga, zilishinda Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati mara moja kwa kila timu.
Azan alisema usahihi ni kwamba, Simba ilishinda kombe hilo mara sita na Yanga mara tano, huku timu ya taifa ilishinda mara tatu Kombe la Chalenji, mwaka 1974, 1994 na mwaka 2011.
“Nimesikitishwa na majibu yaliyotolewa na serikali kuhusu matokeo ya michuano hiyo. Naomba kutoa taarifa Naibu Spika,” alisema Azan.
Katika swali la msingi la Mbunge wa Ziwani, Ahmed Ngwali, aliyetaka kujua ni mafanikio gani ya msingi na ya kujivunia yaliyopatikana kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mpaka sasa.
Akijibu swali hilo, naibu waziri huyo alisema kwa jumla shirikisho hilo limefanikiwa kukuza na kuendeleza mpira wa miguu kila kona ya nchi na kuweka muundo wa utawala katika kila ngazi, kuandaa wataalamu wa fani za ufundishaji, uamuzi, utawala na tiba kwa wanamichezo zaidi ya 10,000 na kuongeza kuwa, wataalamu hao wamepata mafunzo hayo tangu nchi ilipopata Uhuru.
“Shirikisho pia limefanikiwa kuandaa na kuendesha programu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mashindano ya timu za vijana, wanawake na watoto kama sehemu ya kuweka msingi bora wa maendeleo ya mchezo wa soka,” alisema.
Pia alisema timu ya taifa ilifanikiwa kucheza mara moja fainali za Kombe la Afrika na mara moja kwa timu za taifa za wachezaji wa ligi za ndani, (CHAN), pamoja na kujenga na kuimarisha uhusiano mwema kati ya shirikisho na serikali. 

No comments: