Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, September 28, 2012

Tanzania kutangaza mshiriki wa Miss East Africa Oktoba 14


 
Mrembo atakaeiwakilisha Tanzania katika mashindano ya mwaka huu ya urembo ya Miss East Africa atatangazwa rasmi tarehe 14/10/2012 katika hotel ya Serena Jijini Dar es salaam.

Jumla ya warembo 148 wameomba kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss East Africa mwaka huu lakini ni Mrembo mmoja tu atakaechaguliwa kuiwakilisha Nchi katika mashindano hayo makubwa ya urembo katika ukanda huu wa Africa na yanayosubiliwa kwa hamu na wapenzi wa fani hiyo ndani na Nje ya Africa Mashariki 

Aidha maandalizi ya mashindano hayo yanaendelea vizuri ambapo yatafanyika tarehe 07 December, 2012 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam

Wakati huohuo Nchi ya Burundi imebadili mwakilishi wake ambapo sasa itawakilishwa na mrembo Ariella Kaneza (23), Mwanafunzi wa mwaka wa pili wa chuo kikuu cha Universte De Lumiere akichukua Degree ya marketing.

Taarifa kutoka Burundi iliyosainiwa na Mratibu wa Mashindano ya Miss East Africa Nchini humo, Serge Nkurunziza, zimeeleza kwamba Burundi imeamua kubadili mwakilishi wake ili kuhakikisha kwamba Nchi hiyo inashinda Taji hilo kwa mara ya pili tangu mashindano hayo yalipoanzishwa mwaka 1996 baada ya kugundua kwamba mwakilishi wake wa awali anapungukiwa baadhi ya sifa chache za kuweza kunyakua taji hilo. (Burundi imewahi kushinda Taji hilo mara moja mwaka 2008 kupitia kwa mrembo wake Miss Claudia Niyonzima)
Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake na yatashirikisha warembo kutoka Nchi 16 za ukanda wa Afrika Mashariki.

Nchi zilizothibitisha kushiriki mashindano hayo ni wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. Nchi zingine zilizoalikwa kushiriki ni pamoja na Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, Southern Sudan, Malawi, pamoja na visiwa vya Seychelles, Madagascar, Reunion, Comoros, na Mauritius.

Mashindano ya Miss East Africa yanalenga kukuza ushirikiano na kutangaza utamaduni wa Afrika Mashariki, pamoja na kutangaza utalii wa Tanzania kama Nchi wenyeji wa mashindano hayo makubwa katika ukanda huu wa Afrika.

Mashindano ya Miss East Africa yanamilikiwa na kuandaliwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam,.

No comments: