Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, March 20, 2013

JE WAMJUA KING MAJUTO?

Amri Athumani, anayejulikana pia kama King Majuto, amekuwa mwigizaji wa vichekesho kwa miaka 55, Mtanzania huyu mwenye umri wa miaka 65 anaweza kuonekana nchini kwake kote na anatambuliwa kimataifa.
  • Amri Athumani, anayejulikana zaidi kama King Majuto, amekuwa muigizaji wa vichekesho Tanzania kwa miaka 55. [Na Francis Peter Machibya] Amri Athumani, anayejulikana zaidi kama King Majuto, amekuwa muigizaji wa vichekesho Tanzania kwa miaka 55. [Na Francis Peter Machibya]
Zaidi kuhusu kazi yake, King Majuto amelenga katika kutetea amani na kukuza umoja wa taifa. Katika shughuli za umma, vipindi vya redio na sinema ambazo anaonekana, anakuza jamii iliyo salama, utawala bora, heshima ya binadamu na maisha mazuri kwa wote.
King Majuto alizungumza na Sabahi kuhusu mapenzi yake kwa kufanya sanaa na jinsi ya kuimarisha jamii.
Sabahi: Lini ulianza kuigiza?
King Majuto: Nilianza kuigiza mwaka 1958 nikiwa na umri wa miaka 10. Niliuwa katika Shule ya Msingi ya Msembweni, na nilikuwa na uzoefu ambao ulinihamasisha kuwa mwana sanaa.
Mlevi mmoja alikuwa anapita karibu na shule yetu huku akipiga ngoma kwa nguvu huko nje. Mtoto mmoja akajiunga kucheza ngoma kwa sababu yule mtu alikuwa anapiga mdundo mzuri. Mwalimu wetu alikasirika na kumtuma mwanafunzi mwingine kumfukuza yule mtu. Badala ya kumkimbiza, mwanafunzi yule naye akajiunga na ngoma.
Mimi nilikuwa darasa la pili. Mwalimu wetu akatoka nje ya darasa kwa kishindo na kwenda kumfukuza yule mlevi. Sote tulikuwa kimya huku tunamwangalia mwalimu wetu kwa dirishani. Wakati mwalimu alipokuwa anamkaribia [yule mtu], akaanza kutingisha mabega yake kufuatisha mdundo. Kwa mshangao, badala ya kumfukuza mlevi, mwalimu naye akajiunga na ngoma... baada ya muda mfupi, shule nzima ilikuwa inacheza ngoma.
Sabahi: Tena iliishia vipi?
King Majuto: Baada ya saa moja au zaidi ya kucheza ngoma, mwalimu akamshukuru mlevi na kuwaambia wanafunzi umuhimu wa burudani kama kitu cha kuunganisha watu, zana ya kutunza utamaduni na kutunza historia. Kuanzia wakati huo, niliamua kuwa kazi [katika sanaa] inaendana na maslahi yangu. Nikaanza kuifanyia mazoezi, na kujiunga na kwaya ya shule.
Sabahi: Nini kilifuatia baada ya masomo yako?
King Majuto: Mwaka 1966 nilimaliza darasa la nane. Mwaka mmoja baadaye, nilijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa. Tulikuwa tunalipwa shilingi 20. Nilibakia kule kama askari hadi mwaka 1970, lakini mmoja wa viongozi wetu alikuwa ananikera sana. Kila nilipokuwa ninatunga nyimbo au kichekesho, alikuwa ananisumbua. Nikaliona jeshi la kujenga taifa [kuwa] sio bandari ya salama kwangu, kwa hivyo nikaacha kazi.
[Baada ya kufanya kazi kadhaa], mwaka 1976 niliamua kujishughulisha na kazi ya sanaa muda wote. Baada ya hapo, nikaanza kujiingizia hadi shilingi 6,000 kwa mwezi kutokana na kuimba na kuigiza, na nikamudu kujenga nyumba yangu ya mwanzo.
Mwaka 1983 nikajiunga na Bendi ya DDC Kibisa ya Dar es Salaam, na mwaka 1985 nikaenda katika Kikundi cha Utamaduni cha Muungano.
Sabahi: Tuelezee kuhusu Kikundi cha Utamaduni cha Muungano.
King Majuto: Tulikuwa tunatengeneza filamu, Kikundi kikaniteua kama mkuu wa idara ya sinema, ambayo ilikuwa inashughulika na filamu na vichekesho ambavyo vilikuwa vinakuza umoja wa Afrika.
Kile tulichokuwa tunatetea kikawa kweli. Tulikuwa tunaomba uwepo umoja wa Afrika, na sasa tunao Umoja wa Afrika. Hii ni moja ya michango mikubwa kabisa kwa Umoja wa Afrika kupitia sanaa yangu.
Sabahi: Ni katika kampeni gani nyingine ulishiriki?
King Majuto: Nimecheza sehemu ya filamu dhidi ya mauaji ya albino. Katika miaka mitatu iliyopita, nchi yetu imekumbwa na wimbi la mauaji ya kiasi cha albino 57 waliuliwa kutokana na imani za kishirikina kwamba kiungo chochote au mfupa wa albino unaweza kumfanya mtu awe tajiri.
Mwaka 2010 nilianzisha kampeni kubwa katika mikoa ya kanda ya ziwa (Mwanza, Kagera, Kigoma, Shinyanga na Mara) kuhusu suala hili na naamini ujumbe wetu ulifahamika. Mauaji ya albino yamesita. Ujumbe wangu kupitia filamu na vichekesho vifupi ulikua wazi. Ulisema, "huwezi kuwa tajiri kwa kuwaua albino". Ilikuwa kampeni ya miezi sita na ilifanikiwa.
Sabahi: Vipi sanaa inaweza kuleta mabadiliko Tanzania?
King Majuto: Bila ya kazi za sanaa katika nchi hii umoja ungekuwa umeharibiwa muda mrefu uliopita. Naendelea kuwakumbusha Watanzania kuwa umoja wetu, amani na utulivu lazima vibakie kuwa kipaumbele chetu cha kwanza. Naweza kusema kwa kujiamini kuwa filamu na vichekesho vyangu vimesaidia kuiunganisha Tanzania kila wakati nchi ilipoingia [katika mizozo].

No comments: