Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, September 26, 2013

DOLA YAINGILIA KATI NDOA YA BIBI HARUSI MWENYE MIAKA 14

NDOA iliyokuwa tayari kufungwa na shehe kati ya Hamis Ngaumba (35), mkazi wa Bangulo, Ulongoni, Gongo la Mboto, Dar na binti wa miaka 14 anayetajwa kwa jina moja la Zubeda, imesambaratishwa na polisi wa Kituo cha Polisi cha Sitaki-Shari, Dar kutokana na umri wa bi harusi kuwa mdogo, Amani limeidaka hiyo.
Binti wa miaka 14, Zubeda akiwa tayari kufunga ndoa na Hamis (35).
Kizaazaa hicho cha aina yake kilichovuta hisia za wengi kilitokea saa 10:00 jioni, Jumapili iliyopita ambapo Shehe Bakari Mgesa wa Msikiti wa Bangulo alikuwa ameanza kutoa mawaidha ya maandalizi ya kufungisha ndoa hiyo lakini ghafla polisi na mapaparazi waliingia na shughuli kuishia hapo.
ISHU ILIKUWA HIVI
Mapema siku ya tukio, msamaria mwema ambaye hakupendezwa na kitendo hicho alitoa taarifa kwa mapaparazi ambao nao waliwataarifu polisi wa Kituo cha Polisi Sitaki-Shari na kupewa maafande kutoka dawati linaloshughulikia unyanyasaji wa kijinsia na kuambatana nao hadi eneo la tukio.

BREKI YA KWANZA KWA MJUMBE
Kabla ya kufika eneo la tukio, breki ya kwanza ilikuwa ni kwa mjumbe wa eneo hilo Shina Namba 10, Erasto Nyakiege ambaye alikiri kusikia taarifa hizo za mtoto kufungishwa ndoa lakini alizipata muda mfupi kabla polisi na waandishi hao kufika eneo hilo.

No comments: