Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, July 2, 2010

                                   MAFUNDI WANAOMFANYA MUSTAFAH AWE JUU KATIKA ANGA ZA UBUNIFU 
      Baadhi ya mafundi wanafanya kazi katika ofisi za mustafah Hassan Ally ambapo Uniqueentertz ilipotembelea na kujionea mitndo mbalimbali ya nguo inayotengenezwa na vijana hao chini ya boss wao maeneo ya kinondoni jijini Dar.

                                                           MTOKO WA KITAA
  Moja ya mamodo wa mbele akiwa kitaa hana habali na mtu,vazi hili humfanya msichana ajiamini na kutembea kwa madaha zaidi kwa namna yoyote ile lazima aiteke hadhira.kiatu cha ferragamo na kipensi cha madewell

            WASHIRIKI WA MISS TANZANIA KUNOLEWA NA KAMATI 
Mshauri wa Kamati ya Miss Tanzania DK.Raamesh Shah (kulia) akitoa mafunzo kwa warembo wanaoshiriki shindano la Miss Tanzania katika semina inayoendelea katika Hoteli ya Giraffe iliyopo Mbezi Dar es Salaam. jumla ya warembo 31 wapo katika kambi hiyo (wapilI) ni Mwenyeikiti wa kamati ya Miss Tanzania PrashantPateri, Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza.
                        
                                          MICHAL MAURUS AFANYA VIOJA DAR !
                                                                
                                                      Maurus akikuch..kuch..hotahe..
  Moja ya wadau na waandishi wa kutegemewa michael amenaswa na camera zetu akitupa mbichi,yaani mtu mzima akifikisha hisia zake napohusika kwa sisaduu flani hivi,anyways ipotezee......!! hivi ni baadhi ya vituko vya maurus ukimtizama kwa macho ni mpole ila ana mautundu kibaoo..!


                                  WAREMBO WA VODACOM MISS TANZANIA KUINGIA KAMBINI GIRAFFE HOTEL
                                   Hashim Lundenga

Warembo waliofuzu kuingia Fainali za Mashindano ya Urembo ya VODACOM MISS TANZANIA 2010, leo wameingia kambini kwa ajili ya kuanza mchakato wa kumrithi mrembo Miriam Gerald.
                             Washiriki wa Miss Tnzania 2010

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo mchana kabla ya warembo hao kuelekea Kambini, Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga, alisema kuwa “Warembo hao Wakiwa kambini watakuwa na ratiba mbali mbali ikiwa ni pamoja na kufanya kazi za kijamii na kutembelea sehemu mbali mbali za vivutio vya kitalii”

Alizitaja sehemu hizo kuwa siku ya Tarehe 17 / 08 / 2010 warembo watapewa semina maalumu na viongozi wa kamati ya Miss Tanzania pamoja na kusaini mikataba kati yao na waandaaji.

Tarehe 19 / 08 / 2010 waandishi wa habari wote watapata nafasi ya kuongea na washiriki na kupata maoni yao na jinsi walivyojiandaa katika kunyakuwa taji la VODACOM MISS TANZANIA 2010

Mwishoni mwa wiki warembo wote wakiambatana na baadhi ya viongozi wa kamati watasafiri kwenda katika mikoa ya kanda ya kaskazini “KILIMANJARO: na “ARUSHA” kwa ajiri ya kutembelea vivutio vya utalii ili kuvitangaza na kuwahamasisha watanzania ili wajenge utamaduni wa kutembelea, kuvilinda na kuvithamini vivutio vyetu.


H
uu ni mpango tunaoshirikiana na taasisi za serikali yaani ,BODI YA UTALII, TANAPA na NGORONGORO CONCERVATION AREA AUTHORITY.

Huu ni mwaka wa pili taasisi yetu “Miss Tanzania” kushirikiana na taasisi za serikali kuhamasisha watanzania kuthamini na kutembelea vivutio vilivyopo nchini kwetu.

Tunategemea kwenda mbele zaidi kwa kuvitembelea vivutio vya kusini mwa Tanzania, SELOUS, RUAHA NATIONAL PARK, MIKUMI na UDIZUNGWA, katika siku za usoni.


      MISS KILIMANJARO ANAFAGILIA UGALI ILE MBAYA !!! 
                                         prisca akijichana msosi
 Mshindi wa mkoa wa kilimanjaro 2010 na mshindi wa pili kanda ya kaskazini,miss Prisca Mkonyi akipata msosi wa mchana yaani ugali,lost na nyama choma na kati ya vyakula anavyovipenda akiwa anga za home na kitu kingine ambacho hawezi kujizuia kula awapo mahali popote ni chungwa ! 


         MISS EASTERN ZONE 2010 KUAGWA RASMI NA WAANDAJI


               Mrembo Angelina Ngege mshindi wa eastern zone 2010


MKURUGENZI WA KAMPUNI YA KIMKEV ENTERTAINMENT AMBAO NI WAANDAJIWAKONGWE
WA MISS EASTERN ZONE),BW.KIM KIMENYA AKIONGEA NA WAREMBO PAMOJA NA  NA WAGENI WAALIKWA WAKATI AKIWAKARIBISHA DINNER ALIYOWAANDALIA WAREMBO WA EASTERN ZONE KWA AJILI YA KUWAAGA KABLA YA KUJIUNGA NA KAMBI YA MISS VODACOM TANZANIA KWENYE HOTELI YA CITY STYLE SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 14.08.2010.KAMBI YA MISS TANZANIA INAYOAANZA JUMATATU YA 16-8-2010 KATIKA HOTEL YA GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL YA JIJINI DAR.
                         
NNYISHINDANO LA WABUNIFU WA MITINDO LAJA HIHI KARIBUNI KWA MARA NGINE
 Shindano hili linafanyika kwa mwaka wa tatu sasa, halina kikwazo cha umri, na linatoa fursa kwa watu wote wanaoamini kwamba wana kipaji cha ubunifu, na wanataka kuwa wabunifu. Swahili Fashion Week ni jukwaa bora kwa wabunifu kuonyesha uwezo wao wa ubunifu na kuibua sindano la wabunifu wapya, ni jukwaa linalowawezesha watu kufikia malengo yao , aliongeza Mustafa Hassanali, ambaye pia ndiye mwasisi wa Swahili Fashion Week.



Shindano hili linatoa fursa kwa wabunifu kutoka pande zote za Tanzania . Mwisho wa kujisajili ni tarehe 30th ya mwezi wa August 2010. Mwaka 2008 Edwin Musiba alishinda, na mwaka 2009 alishinda 2jenge Afrika Matalay, najiuliza nani atashinda mwaka huu?, alimalizia Hassanali.
                        By Othman.



CAMPBEL"S  TAKE
NAOMI CAMPBELL'S agent has released a statement saying the model "has nothing to gain" by allegedly lying at a war crimes trial. It also declared that although Campbell's comment that the trial was an inconvenience was a bad choice of words, it had been taken out of context

KANYE WEST KUTUMBUIZA MTV VMAs




Us reports that the rapper will perform at this year's awards show, set to air Sept. 12 on MTV. The set will precede West's untitled fifth album, currently slated for a November release.




GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL KUIZAWADIA KAMERA YA KISASA UNIQUEENTERTZ BLOG
Mkurgenzi wa hoteli ya Giraffe Bwana Charles Bekon ameizawadia blog ya uniqueentertz camera ya thamani kubwa akiwa na dhumuni la ki\uipoa nguvu blog hii na kurahisisha upatikanaji wa picha bora kwaajili ya blog
mmliki wa blog hii Bwana Magese atakabidhiwa kesho kamera hiyo na mkurugenzi huyo ambapo camera hiyo itatumikupata matukio mbalimbali wakati kambi ya miss Tanzani ikiwa hotelini hapo na inaanza jumatatu ya 16-8 2010.

LUNDENGA ATANGAZA MAJINA YA WAREMBO WA MISS TANZANIA
Mratibu na mkurugenzi wa Lino Entertainment bw.Hasim Lundenga ametamgaza majina ya warembo waliopita na kupata tiketi yakwenda Vodacom miss Tanzania ambapo kambi inaanza taerhe 16 august 2010 katika hoteli yenye hadhi ya nyota nne Giraffe ocean view hotel
Hashim Lundenga ilitaja majina ya washiriki na sehemu wanazowakilisha kama ifuatavyo Ester Dennis na Gloria (UDSM),Shadia Mohammed, Furaha David na Mary Kagali (Nyanda za Juu Kusini).





 Bahati Chando, Salma Mwakalukwa na Consolata Lukosi (Kanda ya Kati),Flora Florence, Mary Adam na Angelina Ndege (Kanda ya Mashariki), Alice Lushiku, Irene Hezron na Amisuu Malick (Kanda ya Kinondoni), Genevive Emmanuel, Anna Daudi na Britney Urassa (Kanda ya Temeke), Glory Mwanga, Prisca Mkonyi na Jally Murei (Kanda ya Kaskazini).






Wengine ni Gloria Mosha na Christine Justine (Kanda ya Chuo Kikuu Huria), Flora Martin, RachelSindbad na PendoSam (Kanda ya Elimu ya Juu), Fatma Ibrahim, Buduri Ibrahim na Margareth Godson (Kanda ya Ziwa).

                  MAMBO YA LONDON WHITE PARTY WEEKEND HII
Wabongo kadhaa walikuepo kujipangusa na kula bata pande hizo za London

FATMA IBRAHIM AWAVODACOM MISS LAKE ZONE 2010
kinyang"anyiro cha kumsaka mrembo wa kanda ya ziwa kilifanyika jana katika jiji la mwanza ndani ya ukumbi wa Natilo hotel uliopo mjini humo ambapo fatma ibrahim aliibuka mshindi.mgeni rasmi alikuwa waziri wa nishati na madini MH.Wiliam Ngereja

Jumla ya mkoa minne yaani mwanza,kagera,mara na shinyanga ilikusanyika kutafuta watatu watakaoenda moja kwa moja miss Tanzania.
Huu ni mwanzo wa kuanguka kwa umalkia wa miriam gerald ambapo ndiye mshindi wa taji hilo kwa mwaka jana na sasa amebakiza taji moja tu la miss Tz ambapo kambi yake inaanza hivi karibuni.

REDDS FASHION PARTY AT MOVEN PICK 
Jipati lililoandaliwa na kampuni ya TBL kupitia kinywaji cha REDDS original usiku wa jana ilifanyikaa hafla hiyo katika hotel ya moven pick kuwapongeza waandaji wa kanda za Dar es salaam na warembo waliochaguliwa kuingia kambi ya Miss Tanzania kwa mkoa wa Dar es salaam ambapo uniqueentertz ilikuepo kuangaza hili na lile pande hizo
Na hizi ni picha zinazoonyesha how it was !
mc jokate
 
Brand manager wa redds kabula 

Nancy sumari na Irene kiwia walikula tenda
Warembo wa miss Ilala
 
Warembo wa miss temeke

Warembo wa miss kinonondoni
Miriam gerald aliibuka na kivazi cha kufa mtu
Mwisho wa siku warembo wote wote na waswalofika waliruka kwanja la mguu kuinuka kiatu kikabaki chini lililoporomoshwa na Dj makay ambapo Redds ilimwaga vinywaji bure na machop

LIL KIM AJIMWAYAMWAYA NA JUMA NATURE FIESTA
Moja ya staili za kiumeni alizopewa na lil kim na sir nature wakati nature akibambia booty ya  mwanamuziki huyo alieshushwa na clouds kwaajili ya kuburudisha wabongo katika tamasha la fiesta

kanumba sasa amedata kwa movie...yahofiwa kudata kabisa !!


KANYE WEST KUSHUSHA MZIGO NOVEMBA HII
Rapa mahiri katika gemu la hiphop huko majuu kanye west anatarajia kuachia album yake mpya yenye nyimbo kali kama "power" ambayo itadondoka baada ya siku 20 toka aug- 6 na single nyingine kali kama "lost in the world" na "all of the lights" ambazo zitafuatia.
Kanye alitoa ufafanuzi huo akiwa katka ziara za kazi zake nchini korea ambapo watu wa huko walimpokea kwa hamu na msisimko mkubwa kwani anakubalika ile mbaya pande hizo.

NIKKI MINAJ KUIPUA SINGLE MPYA
Mwanadada mahili katika muziki wa kufokafoka huko amerika nikki minaj ameiambia uniqueentertz kuwa anmeshamaliza kuirecord single yake mpya inayokwenda kwa jina la"keep me grounded" ambapo anasubiri taratibu za young money iende hewani.

GABRIEL MOLLEL MBUNIFU WA NGUO ZA KIMASAI
Gabriel ni moja ya wabunifu waliopo nchini Tanzania wakidumisha utamaduni wa mtanzania kupitia vazi la asili ya mmasai anayetoka kaskazini mwa Tabzania.
Ukitaka kuona kazi nyingi za mbunifu huyu tembelea pale sleepway au tembelea tovuti yake ww.tanzaniart.com

VICTORIA BECKHAM  AMFUNDA MUMEWE
            Mke wa mwanasoka maarufu duniani victoria becham ambaye ni mwanamitindo na mdau katika medani hii amemfunda mumewe namna ya kuzndua nguo za kiume zinazotengenezwa na lebo ya mitindo ya nguo za Davd bekham ambazo zinatarajiwa kutoka hivi karibuni.
Nguo hizo ziazotengenezwa na kuzinduliwa kipindi cha joto 2010,becham amepanga kubuni nguo za utamaduni kwa wanaume,suti za kutokea usiku,smart day na Za ufukweni.

MWISHO SHAVU HILO !!
Baada ya mwisho mwambapa ameanza kupata shavu upya baada ya kajiunene flani hivi kupotea ka kile kinachodaiwa alifulia mbaya !!, kwa sasa mwisho anaonekana akiwa na shavu la kutabamu kila wakati kutokana na ndoto alioyoipoteza kumrudia tena kwa mara ya pili.
Mwisho ni kati ya vijana wa kitanzania wenye zali la kuzaliwa ambao wanatembelea nyota bila ndumba wala hilizi,BBA ALL STARS imemrudishia heshma ambapo bado anaonyesha makali yake



SHEREHE ZA KUWAPONGEZA MAWAKALA WA MISS TZ AUG 7
Jipati linaloandaliwa na kampuni ya tbl kupitia kinywaji cha redds original ambae ni mdhamini rasmi wa miss tanzania 2010 imeandaa paty hiyo itakayofanyika katika hoteli ya moven pick august 7 mwaka huu.ambapo waandaji mbalimbali watahudhulia jipati hilo.

MISS LAKE ZONE KUFANYIKA AUGUST 7 JIJINI MWANZA
   ,Shindano la kumsaka mshindi wa kanda ya ziwa katika kupata tiketi ya kwenda miss Tanzania inatarajiwa kufanyika tarehe 7 katika ukumbi wa yatch club uliopo kandokando ya ziwa victoria.
   Jumla ya washiriki kutoka mikoa minne yaani mwanza,mara,kagera na shinyanga wataingia kambini hivi karibuni wiki moja kabla ya shindano.
Wakati huohuo kambi ya Vodacom miss tanzania inategemewa kufunguliwa siku ya tarehe 16 august 2010 katika hoteli ya Giraffe ocean view iliopo pembezoni mwa bahari ya hindi jijini Dar es salaam.

fashion for helth



mojja ya show zilizofanyika hivi karibuni mjini zanzibar kuchangia matibabu ya watoto wenye mtindio wa ubongo katika hospitali iliopo kidongo chekundu mjini unguja ,iliandaliwa na mustafah asanali na kdhaminiwa na vodacon

MAMBO YA WHITE PARTY JIJINI DAR 
Si mchezo jiji la dar ukizubaa umeachwa feri,na hivi ndivyo masistaduu wa hapa wanavyojirusHA.


happy birthday don magese 
on 31 july
 

FROLA MARTINE AWA MISS HIGHER LEARNING 2010
Mlimbewnde msomi ametwaa taji la miss vyuo vikuu katika usiku wa kuamkia ijumaa onyesho lililofanyika katika viwanja vya karimjee jijini Dar es salaam ambapo mshindi wa pili alikuwa ni pendo samweli na wa tatu alikuwa rechel filbert.

RICKY ROSS AJIGAMBA KUMBWAGA EMINEM
Rapper mwenye itikadi za kihasla Ricky ross amejitamba kumuondoa Rminem katika Bilboard top 200 ambapo eminem amekaa kwa takribani wiki nne mfululizo na album yake ya "Ricovery."
Ricky ross ambaye anatmba na album yake mpya inayoitwa "teflon don" anaamini wki ijayo atakuwa yeye namba moja katika Bilboard top 200.

MISS HIGHER lEARNIMG KUFANYIKA USIKU HUU
Kimbembe cha kumtafuta mlimbwene wa vyuo vikuu hapa nchin ampo watatu kati yao wataingia kambi ya miss tanzania iatfanyika leo katika viwanja vya karimjee jijini Dar.

HAPPY BIRTHDAY PRISCA
Mrembo Prisca nkonyi anapongezwa na wadau wote wa tasnia mbalimbali kwani tarehe 26 july anatimiza umri wa miaka 20.
Prisca ambaye ni milimbwende na mshindi wa miss kilimanjaro 2010 pamoja na kshika nafasi ya pili katka mashindano ya miss northern zone kisha kufanikiwa kupata tiketi ya kwenda fainali za miss Tanzania 2010.
UNIQUE ENTERTAINMENT inakutakia maisha marefu na yenye baraka,....happybirthday prisca.....!!!




MWISHO MWAMPAMBA ATINGA BIG BROTHER AFRICA ALL STAR 2010
Mtanzania ailyewahi kuwa mshindi wa big brother namba mbili kwa miaka michache ilyopita amepata tena shavu hilo kurudi kwa mara ya pili.
Toka Tnzania ni Mwisho,Jen toka msumbiji,code toka malawi,Hannington toka Uganda,kaone toka botswana,lerato wa south Africa,merl wa namibia,munya wa zimbabwe,sami toka ghana,uti toka nigeria,sheila toka kenya,jacob wa ethiopia,paloma wa zambia,uti wa nigeria na tatiana wa Angola
Mwanamuziki gwiji la dance hall sean paul alishusha burudani ya aina yake wakati huku tanzania maadhiimisho ya ufunguzi wa uangaliaji rasmi ulifunguliwa na kampuni ya multchoice tz ambapo watu maarufu kama miss tanzania  Miriam Gerald na gwiji la filamu barani afrika steven kanumba walihudhulia hafla hiyo.


GLORY MWANGA AWA MISS NORTHERN ZONE 2010
   Mlimbwende glory mwanga mshindi toka mkoa wa Arusha,usiku wa kuamkia jana july 16 alitawazwa kuwa miss northern zone 2010 baada ya kushika nafasi ya kwanza katika shindano hilo.
   Prisca nkonyi mrembo toka mkoa wa kilimanjaro aliibuka kidedea na kushika nafasi ya pili wakati nafasi ya pili ilienda kwa mshindi toka mkoa wa Tanga jally Morray.
sindano hili iliandaliwa na vigezo kati ya prisca au glory nani kuwa mshindi.kampuni ya Crown International Entertainment chini ya bwana Erasto Jones ya mjini Aarusha.

HAPPY BIRTHDAY MANDELA KUFIKIA MIAKA 92
Uniqueentertz inatoa salamu za kumpongeza Rasi wa kwanza wa Afrika kusini na mkombozi wa nchi nhiyo dhidi ya ubaguzi wa rangi,na hivi ndivyo ilivyokuwa huko johannesburg nyumbani kwao.


TATOO GAL
Rose moja ya model wa video nchini tanzania akichora tatoo kuongeza mvuto.
 


KWA WALE WAPENZI WA HABARI ZA KIAFRIKA
karibuni mumtembelee bwana Godfrey kaswalala katika blog yake


  WIKI YA HAILE SELASSIE KUANZA JUMATATU
   Mwanaharakati hayati haile selassie ambaye ni muasisi wa OAU  na mtu anayeheshimika sna kwa marastafari na watu wenye imani kama hiyo,wiki ya kumkumbuka shujaa huyo toka Ethiopia ambaye ana asili ya ukoo mfalme suleimani na malkia wa sheba.
   Haile selasie alizaliwa 23 july 1892 na kuawa 28 august 1975 huko Addis ababa Ethiopia,hivyo ikumbukew kwa kumuenzi mwanaharakati nhuyu ambaye yuko katika historia ya dunia.AMINA

WASHIRIKI MISS NORTHERN ZONE KUTEMBELEA OFISI ZA VODACOM NA TBL MJINI ARUSHA
          Washiriki wa shindano la kumsaka mlimbwende kwa kanda ya kaskazini leo wametembelea ofasa za vodacom na TBL hususani depertment ya Redds original ambao ni mdhamini. wa shindano hilo.
         Akizungumza na UNIQUEENTERTZ,bwana Erasto Jones ambaye ni mratibu wa shindano hilo kuwa amefurahishwa na makampuni hayo kuwa mstari wa mbele kiudhamini katika shindano lake.
        Baada ya kutoka katika ofisi hzo walielekea city garden ambako nako kulikua na mengi ya kujifunza kwa warebo hao,ambapo ijumaa hii atajulikana malikia wa zone hiyo kwa mwaka 2010.
Erasto amesema mshindi wa kwanza atapata kitita cha milioni moja,kozi ya utalii miaka miwili toka chuo cha taifa cha utalii Arusha na vocha ya manunuzi ya Tsh laki moja kwa ajili ya shoping.
       kiingilio ni 30,000 kwa v.i.p na 20,000 kwa viti vya kawaida ndani ya Naura spring hotel mjuini Arusha.NYOTE MNAKARIBISHWA

LONDON"S LINE UP
The londoni fashion week schedule is in;micheal van dar ham,mary katrantzone,david koma and holly fulton will make their catwalk debuts on september,while Swedish fashoin hose acne will also show in london.

london fashion week

KUMBE  LIL WYNE  SIO  MTU  WA  KAWAIDA
Gwiji la muziki wa kufokafoka(hip hop) lili wyne anatarajia kushusha bonge la ngoma linaloitwa"am not a human being"kutoka kaenye albam yake mpya ambapo siku ya birthday yake septemba 27 ndipo ataachia jigoma hilo.
kwa mijibu wa meneja wake ngoma hii itakuwa mahususi kwaajili ya birthday yake ambapo lili wayne akiwa jela kwa tuhuma za kukutwa na silaha katika bus ambapo ni kinyume na mujibu wa sheria za usa.
Wyne alifungwa toka mwezi march kwa kifungo cha mwaka mmoja akiwa katika gerza la rickers island nchini marekani amekuwa akiwamiss sana washabiki wake ambao anawasiliana nao kwa njia ya email tu,mama yake na watatoto wake ambao amekuwa akiwasiliana nao kwa njia ya simu.pia amewasifu Drake na nNikk minaj kuedndeleza lebo ya young money wakati boss wao yuko kifungoni

KATY PERRY ATAMBA NA CALFORNIA GURL
Mwanadada katy perry ameendelea kutesa katika chati mbalimbali za muziki zmbapo kibao chake cha calfornia guls kinaongoza kuchezwa mara nyingi katika vituo vya radio na television.
Katy kwa sasa anaongoza namba moja katka chati za muziki duniani bilbord katka zile hot 100 akifatiwa na eminem.
Kushika namba moja katika chati hizi si lelemama kwani mwaka jana ilimshangaza snoop dogg kwa soulja boy kuingia mpaka namba nne katika chati hizo wakati wakongwe wengi hawajawai kushika namba moja pamoja na umaarufu wao. 
Wakati huohuo eminemu naye anaongoza katika hot 200 za bilboad

SILVIA SHALLY ALIJIA JUU GAZETI LA UDAKU
     Mrembo silvia shally miss ilala 2009\2010 ameipigia simu blog hii ya urembo na mitindo akilaumu gazeti la ... toleo la jumatatu july 12 2010 kuchapisha habari ambazo hazina ukweli wowote kuwa ameachana na muigizaji maarufu wa filamu steven kanumba na sasa yuko na bwana wa kiarabu ambae amempa makazi na gari la kifahali.
Silvia amekanusha vikali kuwa hana uhusiano na huyo bwana wa kiarabu kama inavyodaiwa na vyombo vya habari,"nampenda kanumba kwa dhati toka moyoni na ndiye mume wangu mtarajiwa,nataka ulimwengu wote uje nampenda kanumba peke yake" aliongea kwa majonzi mrembo huyo. 
   Akiwa zanzibar Kanumba alikuwa wa kwanza kuisoma habari hii ndipo alipoamua kuinua simu na kumuuliza mwandani wake silvia je yalioandikwa ni kweli?.silvia alikanusha habari hizo na kudai ni mbinu za kuyachafua mapenzi yao,hata hivyo kanumba alikuwa mtulivu na mwenye hekima kwa swala ambalo limemuingia rohoni The great. 
  Mrembo silvia alishindwa jizuia kutoa machozi wakati akitoa habari hizi ambapo alishidwa kuendelea kuwa kazini akitigwa na mawazo kuhusu kashfa hii wakati yeye amekolea na hana choice nyingine ila ni kwa celebrity huyo maarufu barani Africa 

KUMEKUCHA KAMBI YA MISS NORTHERN ZONE 2010.
   Mbio za kuelekea kinya'anyiro cha kumsaka mlimbwende wa kanda ya kaskazini imezidi kupamba moto ambapo inajuisha mikoa minne kilimanjaro,Tanga,Manyara na Arusha.
     Siku ya kumaliza gumzo hili ni siku ya ijumaa july 16 ambapo jumla ya washiriki wote watapanda jukwaani katika ukumbi wa hoteli ya kitalii ya Naura spring iliyopo jijini Arusha.
Kambi ya warembo hao imewekwa katika hoteli ya city link iliyopo nje kidogo ya mji ambako wanajifua vilivyo huku kila mmoja akimtambia mwenzake chini ya mwalimu waDance Bob richie.
Erasto jones ambaye ni mkurugenzi wa mashindano haya kupitia kampuni ya crown internationa Entertainment amesema wapenzi wa burudani ya urembo wasubiri kupata burudani ya namna yake toka kwa wasanii wa bongo flava MARLAW ,PETER MSECHU ,HOT STONE NA B-BOYS toka Atown watabamba vilivyo.
Erasto aliongeza kuwa washindi watatu watapatatiketi ya kuingia kinyang"anyiro cha miss Tz ambapo kiingilio cha Miss Northern zone itakuwa ni 20,000/= kwa vit vya kwaida na 30,000/= kwa viti vya VIP.
Miss Northern zone 2010 Imedhaminiwa na VODACOM,TANZANIA ONE,REDDS original.NAURA SPRING HOTEL, PSI, JJ BLACK,CITY LINK HOTEL,CHUO CHA UTALII KAMPASI YA ARUSHA,SKY ,ARTIFUL PHOTO GRAPHIC,EDTIONS SENZIA FASHION,SUPREME POWER FENCE NA CHUO CHA LUGHA YA KIFARANSA(ALLIANCE FRANCEISE)


SUGAR MINOTT AFARIKI DUNIA
mwanzmuziki wa regga mwenye sauti nyororo na producer aliesaidia kuinua muziki wa ragger amefariki akiwa na umri wa miaka 54.
Minott(MY-natt) alikufa jumamosi akiwa katika hospital ya ya The West Indies nchini jamaica katika mji mkuu wa nchi hiyo Kingstone.aidha mkewe marehemu sugar minott maxime stowe amesema bado hajui sababu iliyomuua mumewe.

GENEVIVA EMANUEL ATWAA TAJI LA REDDS MISS TEMEKE 2010
    Mlimbwende Geneviva Emanuel ameibuka kidedea baada ya kuibuka mshindi wa shindano la kumtafuta Redds miss temeke 2010 kwa ngazi ya kanda ikiwa amepata mtiketi yakwenda Miss Tz.
   Mshindi wa pili alikuwa Anna Daud(kulia) na nafasi ya tatu nilienda kwa Pendo Urassa(kushoto) ambapo mtanange huo ulifanyika katika ukumbi wa TTC sigara chang'ombe.
    Kwa upande wa majajin walikua ni Hashim Lundenga(kulia),pashant patel(kati) na Bosco majaliwa(kushoto).

KAMBI YA VODACOM  MISS NORTHERN ZONE YAANZA JULY  9
Baadhi nya washiriki wanaowania taji la miss north zone ambao ni washindi wa mikoa yao ya Tanga,kilimanjaro,manyara na Arusha wameanza kuingia kambini usiku wa jana wakitokea mikoani mwao.
Kambi hiyo ya warembo wanaotikisa na kuleta msisimko katika shindano la Miss Tanzania mwaka huu.
City link hotel ya arusha mjini imedhamini kuwaweka warembo hao hapo hotelini kwa muda wote wa wiki moja ambapo fainali zitakua july 16 jijini Arusha.

ALICIA NKEYS ASHIKA  No 1 CHART ZA BILBOARD {hip hop/r&b}
Kibao kipya cha Alicia keys kiitwacho "un thinkable'(am red) kimeshika namba moja katika chati kubwa za muziki duniani,alicia anategemewa kuuza mamilioni ya copy kwa ubora wa album yake hii mpya ambayo inatikisa anga za muziki barani America na Ulaya.
The element of freedom ndiyo jina la album ambayo inamrudisha keys kwenye chati upya mpaka kushika nafasi ya kwanza katika nyimbo 100 bora za bilboard za r&b na hip hop..

MEL GIBSON ACCUED TO HIT HIS EX-GIRLFRIEND
More rumous are circulated inhollywood today after emerged that mel gibson allegegly hit his ex girl friend  twice while  she was holding their seven-month-old doughter"what kind of a man is that who would hit a woman when she is holding a child iin er hand,hit her twice in the face?"
Mel's Lawyer said that he did not hit Osaka,they just had an argument,where as osaka claimed in an emergency restrain order filling that she was left bloodied,bruised and without her two front teeth after hight.

KANUMBA ATUA DAR TOKA SOUTH.
 iambako alienda kiziara ambako alitembelea ofisi za MNET  na  sehemu mbalimbali za utamaduni wa nchi hiyo ambayo ina kiasi cha wageni wengi kwa sasa waliofika kushuhudia kombe la Dunia.
The Great K aliweza kuhudhulia mechi kati ya ghana na uruguay akiwa south Africa.

CATCH NEW STYLE 

RECOVERY YA EMINEM YAZIDI KUTAMBA UK
Album ya mwana hip hop mahili toka usa inayokwenda kwa jina "recovery" yenye songi la"love yhe way you lie" alichomshirikihsha Rihanna imetikisa chart za Uk ikishika nafasi ya kwanza kwa majuma mawili mfululizo ikifatiwa na kibao cha "calfornia gurl" cha katy perry,recovery ambayo imevunja record ya album yake iliyopita.

MISS&MR EAST AFRICA UK WATOKEA ELTREA NA ETHIOPIA
Moja ya mashindano makubwa ya urembo duniani yalifanyika hivi karibuni mjini londoni ambapo mshindi ni mueltrea ambapo mshindi wa MR.East africa ametokea ethiopia anaenda kwa jina Dawggie.


   REDDS  MISS  TEMEKE 2010 YAZIDI PAMBA MOTO
   Joto limezidi kupanda kwa washiriki wa kanda ya temeke ambapo mtanange utafanyika july 9 katika ukumbi wa tcc sigara chang"ombe.
    Imebaki siku tu ambapo watajulikana ni akina nani wataendelea na mchakato wa Miss tanzania kutoka kanda ya Temeke.

ALICE LUSHIKU AWA REDDS  MISS KINONDONI 2010
   Mnyange Alice lushiku usiku wa kuamkia leo ameibuka kidedea baada ya kuibuka mshindi toka kanda ya kinondoni ambapo mtanange huo ulifanyika katika ukumbi wa mlimani city jijini.
   Mshindi wa pili alikuwa Amisuu malik na watatu alikuwa Irene Hezron ambapo Giraffe ocean view hotel ilitoa zawadi kwa mshindi wa kwanza na pia ndipo kambi ya miss kinondoni ilikaa kwa muda wote wa maandalizi.

   PRISCA NKONYI TEGEMEO LA WAKAZI WA KILIMANJARO MISS TANZANIA
  Mshindi wa mkoa wa kilimanjaro mrembo Prisca amegeuka tegemeo la wadau na mashabiki wa urembo mkoani humo kwakua ndiye anayetgemewa zaidi kufanya maajabu kama aliyofanya Miriam Gerald  mwaka jana.
  Prisca alikuwa jijini Dar hivi karibuni akifanya shopping yakufa mtu ikiwa ni maandalizi ya kwenda ngazi ya kanda ambako ameaidi kuwatoa jasho washiriki wenzake kama alivyofanya kwenye miss kilimanjaro.
  Mtanange wa kumsaka miss kanda kaskazini,kambi inaanza july 9 ambapo siku ya fainali steji itachimbika high hills kubaki stejini.kila laheri prisca.

  UNIQUE WEEKEND TOP TEN
   *1:-calfornia Gurl  by katy perry  ft  snoop dogg.
   *2;-Love the way you lie  by  Eminem  ft Rihanna
   *3:-O.M.G  by  Usher raymond  ft  wil.i.am
   *4:-Airplane  by  B.O.B   ft Hayley wiliam
   *5:-Bilionaire  by  Travie mc coy ft  Bruno mars
   *6:-Find your love  by  DRAKE
   *7:-Cooler than me  by  MIKE POSHER
   *8:-Your love is my drug  by  ke$ha
   *9:-Alejandro   by  lady gaga
   *10:-Riding  by Jason Derula

   DRAKE AHAILISHA  EUROPEAN TOUR
            Mwanamziki anaekuja kwa kasi ya ya ajabu katika fani ya muziki wa majuu(rap) Drake toka YUNG MONEY amgailisha tour yake barani ulaya kwa kuwa mama yake mzazi ni mgonjwa na anataji upasuaji mdogo.
           Msemaji wa Drake aliimbia moja ya radio mjini toronto usa kuwa drake amejitadi kujishauri kwenda ila ameshindwa kutokana na mama yake kuitaji sapoti ya mwanae akiwa mgonjwa,hivyoTour hiyo imesogezwa Mbele.
   Mkoa wa manyara haukubahatika kupeleka mshiriki yoyote katika fainali za shindano la kumtafuta miss tanzania.
   Uniqueentertz inawapongeza Glory,prisca na Jally kwani toka wanaingia kambini blog hii imekuwa mstari wa mbele kuandika habari za shindano hili ambapo upinzani wa mashabiki walikuwa apigia kura washiriki wawili ambao wanafanana

No comments: