Mkurugenzi wa  Tanzania One Thetre (TOT) ambaye pia ni Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba akizunguma na waandishi wa habari nyumbani kwake, Mbezi Tangi Bovu, Kawe, Dar es Salaam, leo  wakati
 akizungumzia hali ya afya yake baada ya kurejea nchini akitoka nchini 
India alikokwenda kufanyiwa upasuaji. Kushoto ni Mkewe, Salome Andrew 
Komba. 
**********************************
NA BASHIR NKOROMO
MKURUGENZI
 wa Kundi la Tanzania One Theatre (TOT) ambaye pia ni Mbunge wa Mbinga 
Magharibi, John Komba amerejea kutoka India ambako amefanyiwa upasuaji 
kumtibu ugonjwa wa nyonga ulilokuwa ukimsumbua upande wa mguu wake wa 
kulia.
Akizungumza
 na waandishi wa habari, jana Julai 27, 2012, nyumbani kwake Mbezi kwa 
Komba, mjini Dar es Salaam, Komba alisema amerejea nchini,  Juzi,  baada
 ya kupatiwa matibabu hayo kwenye hospitali ya Appolo iliyopo Hydrabad 
nchini India tangu mwanzoni mwa wezi huu.
Alisema,
 aliondoka nchini, Julai 2, 2012, baada ya kupelekwa na serikali kwa 
maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete, Spika wa Bunge Anna Makinda na Katibu 
wa Bunge John Kashilila na kwamba alikwenda baada ya kukosa matibabu 
hapa nchini kwa sababu ya mgomo wa madaktari.
"Siku
 napelekwa Muhimbili tu, tayari madaktari walikuwa wameanza siku ya 
kwanza ya mgomo wao, nikawa sina namna ila kuujulisha uongozi wa Bunge 
na kisha nikamuomba Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, naye kwa 
mamlaka yake akanisaidia haraka kama ambavyo huwasaidia wengine kwenda 
kutibiwa nje", alisema Komba.
Alisema,
 uzito ulichangia sana kusababisha mifupa kusagana kwenye nyonga upande 
wa mguu wa kulia, ambapo hadi anakwenda India alikuwa na uzindo wa kilo 
138 wakati wastani wa uzito aliotakuwa kuwa nao kulingana na ukumbwa wa 
mwili wake ni kilo 90 au 100 tu.
"Amesema,
 baada ya matibabu amerejea nchini akiwa na uzito wa kilo 128 ambao hata
 hivyo ametakiwa kuudhibiti na kuupunguza katika siku hizi ambazo 
atalazimika kupumzika nyumbani kabla ya kuanza kazi, Mwezi Septemba 
mwaka huu kama alivyoelekezwa na madaktari.
Akizungumzia
 upasuaji ulivyoendeshwa, Komba alisema, ulichukua saa tano na 
kukamilika bila matatizo katika upasuaji huo ambao alisema sehemu 
iliyopasuliwa ni ya ukumbwa wa futi moja.
Alisema,
 hata hivyo baada ya upasuaji huo, hakuweza kurejea katika wodi ya 
kawaida, kwa sababu majongwa kadhaa yaliibuka ikiwemo homa kali, presha,
 hivyo akalazimika kulazwa katika wodi ya wagonjwa waliopo kwenye 
uangalizi maalum (ICU) kwa siku tano.
"Sasa
 nimerejea nikiwa mzima, kwa sasa natumia fimbo hii, ili kuwezesha uzito
 uzilemee upande wa kulia nilikopanyiwa upasuaji, lakini sijambo 
kabisa", alisema Komba.
Komba
 alilaani baadhi ya vyombo vya habari ambavyo viliripoti kwamba katika 
kuugua kwake alikuwa mahututi na kwamba alikuwa anaugua figo.
"Jamani
 ninyi waandishi wa habari, jizoesheni kuandika habari zilizokamilika 
siyo kurashia-rashia tu na kuzusha uongo, mfano gazeti moja liliandika 
eti naugua figo nipo mahututi, wakati si kweli kabisa, ilikuwa jambo 
rahisi tu, kuja hapa nyumbani na kuniuliza au kuuliza mke wangu 
lingepata kwa uhakika ninachoumwa", alisema Komba.