Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Saturday, September 14, 2013

MBONGO ATIWA MBARONI BAADA YA KUFUMWA AKILIWA URODA NA MZUNGU

MDOSI au Kanjibai aliyefahamika kwa jina moja la Milah ambaye ni bosi wa kampuni moja ya ujenzi yenye makao yake Mwenge jijini Dar alinaswa chooni akiwa na mfanyakazi wake, John Carlos ‘Shabani’ (watu walimpachika jina la Shabani kutokana na Kanjibai wa kwenye Komedi) ikidaiwa walikuwa katika mazingira ya ulawiti...
Ishu hiyo nzito ilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo wawili hao walikuwa chooni humo kwa zaidi ya nusu saa na kuwasababishia usumbufu watu waliokuwa wakitaka kutumia choo hicho.
   KISA KILIPOANZA
Siku hiyo ya tukio, mtu mwenye sauti ya kiume alipiga simu kwenye chumba cha habari , Mwenge jijini Dar na kupasha juu ya tukio hilo. Alisema:


Mtoa habari huyo alikwenda mbele zaidi kwa kuwaambiwa waandishi wetu waliompokelea simu wachukue Bajaj au Bodaboda ili kuwahi.
 
Sosi huyo kabla ya kukata simu aliweka wazi ramani ya kufika kwenye choo hicho na kusisitiza kwamba muhimu kuwahi kwa sababu huenda wanagombana.

Kufuatia msisitizo huo, waandishi  wetu makini  waliwasha pikipiki zao, kila mmoja na yake na kushika njia kuelekea eneo la tukio.
 
Hata hivyo, kwa kuamini wanaweza kukutana na lolote, waliona ni vyema kwanza kwenda kutoa taarifa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi cha Mwenge ambapo walipewa askari wawili kuelekea eneo la tukio.

ENEO LA TUKIO SASA
Timu hiyo iliwasili kwenye eneo la tukio. Mlango wa choo hicho ulikuwa umefungwa lakini kwa mara moja tu haikuwa rahisi kugundua kama ulifungwa kwa funguo au kawaida tu.
 
 Afande mmoja alijitolea kugonga mlango wa choo hicho ili kupima ushirikiano utakaotolewa na wawili hao au mmoja wao.
 
Sauti iliyoonekana ni ya Kanjibai kutokana na kushindwa unyoofu wa lugha ya Kiswahili ilisikika ikiuliza:
“Nani wewee… taka nini huku?”
Afande: Sisi ni askari polisi, fungua haraka tunajua mko wawili humo ndani, fungua.

Kanjibai: Subiri kidogo.
Baada ya dakika kadhaa ,  mdosi huyo alifungua mlango na kukutwa akiwa na ‘Shabani’.
WALICHOKUWA WAKIKIFANYA CHOONI
Katika maswali ya harakaharaka nje ya choo hicho kila mmoja alisema la kwake ambalo aliliamini linaweza kumchomoa kwenye skendo hiyo mbaya.
 
‘Shabani’ alisema yeye aliingia kwenye choo hicho baada ya kuitwa na bosi wake huyo ambapo alishindwa kumkatalia kwa kuogopa kupoteza ajira yake na kama inavyojulikana maisha ya Dar bila kazi ni ngumu kuyamudu.
 
Alipoulizwa walichokuwa wakikifanya ndani ya choo hicho, Shabani alibaki akiwatumbulia macho maafande.
 
Kwa upande wake Kanjibai alipotakiwa kujieleza kisa cha kuingia chooni na mfanyakazi wake, alisema alimuomba wazame humo ili akamnyoe. Yaani Kanjibai alitaka kunyolewa.

IKAFIKA ZAMU YA KUPELEKWA KITUONI
Afande mmoja aliamuru wawili hao wapelekwe kituo cha polisi, lakini kabla ya kuanza safari, mdosi huyo aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali na kutoa vitu vyake kadhaa na kuwakabidhi wadosi wenzake waliofika ‘kumsaidia’ muda mfupi baada ya kunaswa.
 
Halafu aliingiza mkono kwenye mfuko mwingine na kutoa mafuta aina ya KY ambayo mtaani hujulikana sana kwa jina la ‘mlainisho’ lakini askari alimwambia mafuta hayo yanatakiwa kituoni kwa ajili ya ushahidi hivyo asiwape nduguze.

Breki ya kwanza ilikuwa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi Mwenge ambapo baada ya mahojiano mafupi walihamishiwa Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’ ambapo walihojiwa zaidi kuhusiana na tukio hilo.

No comments: