Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Sunday, September 8, 2013

MTOTO WA KIGOGO ASHTUKIWA KWA DAWA ZA KULEVYA AIRPORT

Mfanyabiashara maarufu na msanii nyota wa bongo muvi ambae ni mtoto wa Waziri Mkuu mstaafua aliyefahamika kwa jina la Libart Msuya katika ya wiki hii alionja joto ya jiwe baada ya kuhenyeshwa masaa kadhaa kwa kupekuliwa alipokuwa anareja toka nchini Uingereza huku msanii mwenzake Manaiki Sanga akihangaika kumnusuru.

Habari za uhakika zilizonaswa na Xdjz ambayo ilikuwepo kwenye viwanja hivyo kwa ajili ya kumpokea mzanii Azonto ambapo Libart alisafiri ndege moja na Azonto wakitokea Uingereza ilishuhudia jambajamba hiyo aliyokuwa akipewa Libert kwenye sehemu ya kutokea wageni wanaokuwa wanawasili.

Libert Msuya ambae ana uaraia wa Ungereza licha ya kwamba ni mtanzani siku za hivi karibuni alikuwa nchini huko ndio familia yake ilipo na siku hiyo ya tukio alikuwa anarejea Tanzani huku akiwa na mabegi kibao na baada ya kufika Air Port ya Dar mabegi hayo alifanyiwa uchunguzi mkubwa kiasi cha kusababisha askari wote kumzunguka.
Hata hivyo hali hiyo iliyodumu kwa dakika 40 ilimlazimu rafiki wa karibu na mtoto huyo Manaiki Sanga “The Don” kuanza kuchanganyikiwa akizani labda huenda ni kweli rafiki yake huyo alikuwa na mzigo.

Aidha baada ya kuachiwa huru Libert alitoka nje huku akipokelewa na Manaiki, hata hivyo mwandishi wetu alifanikiwa kuongea na Libert ambae alisema “ Ni utaratibu ambao upo kila nchi wa kusachiwa hivyo mimi sikuona tatizo pele na wala mimi sijihusishi na biashara yoyote haramu” Alisema Libert

Hata hivyo nae msanii Manaiki Sanga” The Done” aliiambia blog hii kuwa biashara ya madawa sio rahisi kama inafanywa na watu wenye mioyo migumu huku wakiwa wamekula viapo kwamba lolote litakalotokea poa na sio kazi rahisi ni kama sanaa wanayoifanya wasanii wote.

No comments: