Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Saturday, September 14, 2013

YALIOJILI FIESTA 2013 DODOMA

Haaaa haaaa...ukitaka kubana pua kabane nyumbani kwenu,hapa ni hip hop tuuu.....Msanii wa Bongofleva Ney wa Mitego wakioneshana umahiri umwamba wa jukwaani na msanii mwenzake  Dimond  kupitia wimbo wa Muziki Gani.

 Mmoja wa wasanii wanaokuja kwa kasi kwenye anga ya muziki wa Bongofleva a.k.a hip hop,Stamina akiwaimbisha wakazi wa Dodoma na vitongoji vyake waliojitokeza kwa wingi usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri,wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea.
 Msanii mahiri ambaye kwa sasa anasumbua vilivyo anga ya muziki wa Bongofleva,Diamond akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,linalofanyika usiku huu kwenye uwanja wa Jamuhuri.
 Sehemu ya mashabiki wakishangweka vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2013.
Mmoja wa wakongwe wa muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la Wateule Skwadi,atambulikae kwa jia la kisanii Mchizi Mox akiimba jukwaani usiku huu.  
Maelfu ya Watu wakiwa kwenye uwanja wa jamuhuri,usiku huu wakishangweka na tamasha la Serengeti Fiesta 2013.
Mkali mwingine wa Bongofleva,Dullysykes akiimba jukwaani usiku huu wakati tamasha la Serengeti fiesta likiendelea.
 Young Killer na Stamina  kama kawaida yao wakilishambulia jukwaa la fiesta usiku huu,huku maelfu ya watu wakiwa ndani ya uwanja wa Jamuhuri,mkoani 
 Ni burudani murua kabisa usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri,wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea. 
 Mwanadada ambaye wengi wanadai amerithi viuno na sauti kutoka mwanamuziki Ray C,anaitwa Rachael kutoka nyumba ya vipaji a.k.a THT akiimba jukwaani huku akionesha umahiri wake wa kukata mauno.
Mkongwe wa muziki wa kizaz kipya a.k.a Bongofleva Afande Sele a.k.a Baba Tunda a.k.a Simba Mzee akidhihirisha ukongwe juu ya steji ya tamasha la Serengeti linalofanyika usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri mkoani Dodoma,ambapo maelfu ya watu washabiki wamejitokeza kushuhudia tamasha hilo ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka.
 Makamuzi yakiendelea usiku huu
CLICK OLDER POST KWA HABARI ZAIDI

No comments: