Miss
  Morogoro 2012 Joyce Baluhi katikati akiwa na washindi wenzake, Salvina
  Kibona mshindi wa pili kushoto na Irene Thomas mshindi wa tatu. 
Warembo  hawa ni miomngoni mwa wanaoingia Kamoni hii leo. 
******* 
JUMLA
  ya warembo 14 wanaotaraji kuwania taji la Miss Redd's Kanda ya  
Mashariki 2012 Wanataraji kuiongia kambini mjini Morogoro jioni ya leo  
tayari kwa maandalizi ya shindano hilo.
Shindano
  la Redds Miss Kanda ya Mashariki 2012 linataraji kufanyika Septemba 1,
  2012 katika Hoteli ya Kisasa ya Nashera iliyopo mjini Morogoro.
Aidha wanyange hao walichelewa kunza kambi yao kupisha warembo hao kuhesabiwa makwao kabla ya kuingia kambini. 
Akizungumza
  na Father Kidevu Blog, mratibu wa shindano hilo Alexander Nikitas  
alisema warembo hao pia walishiriki kuhamasisha zoezi la sensa katika  
maeneo mbalimbali wanayotoka Huku wale wa Mkoa wa Morogoro wakihamasisha
  mjini hapo watu kushiriki kuhesabiwa. 
Kanda
  ya Mashariki inaundwa mna mikoa mine katika shindano hilo dogo la Miss
  Tanzania 2012 ambayo ni mikoa ya Morogoro, Lindi, Mtwara na Pwani.
Nikitas
  aliwataja washiriki watakao ripoti kambini katika Lodge ya Usambara  
Safari Resort iliyopo nane nan mkoani Morogoro kuwa ni Zuhura Gora,Alice
  Adam na Shakila Hassan kutoka Mtwara.
Wengine
  mikoa yao kwenye mabano ni Maria Peter,Irene Mweleko na Rose  
Lucas(Pwani) Irene Veda,Stella Bartazary na Darina Athumani(Lindi)  
na kutoka Morogoro ni pamoja na Salvana Kibano,Joyce George,Irene  
Thomas,Betina Msofe,na Nafia waziri.
Taji
  la Miss Kanda ya Mashariki linashikiliwa na Loveness Flavian ambaye 
pia  ni Miss Sport Woman wa Miss Tanzania 2011. Warembo hao watakuwa 
chini  ya Mwalimu Asha Salehe Miss Eastern Zone namba tatu. 
Kwa
  mujibu wa Nikitas wadhamini wa shindano hilo Mbunge wa Kilosa Mustafa 
 Mkulo,Redd's, Dodoma wine, Father Kidevu Blog, Auckland Travel Safairi 
 Tour, Clouds Fm, Usambara Safari Lodge, Chilakale Resort, Endepa Event 
 Planner, Jambo Leo, Kitwe General Traders na Simple Easy Car Renta

No comments:
Post a Comment