Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, September 10, 2013

MZOZO WA USHURU MPAKANI MWA RWANDA NA TANZANIA NGOMA BADO MBICHI

Taharuki imeibuka katika mpaka wa Tanzania na Rwanda wakati madereva wa malori kutoka nchini wakihaha kuvuka kuingia Rwanda kabla ya kuanza kutumika kwa ushuru mpya wa barabara ambao unaanza kutumika tena leo kwa upande wa Rwanda ukilenga magari kutoka Tanzania tu.  
Rwanda iliongeza ushuru kwa zaidi asilimia 229 dhidi ya magari ya mizigo ya Tanzania tu kutoka viwango vya zamani vya Dola za Marekani 152 hadi Dola 500 kwa madai ya kutaka usawa na Tanzania.
 
Ushuru huo ambao ulianza kutumika rasmi Septemba mosi mwaka huu kisha kusitishwa kwa muda, unatarajiwa kurejeshwa tena leo kulingana na tangazo la Rwanda mpakani Rusumo.
Kadhia hiyo imesababisha msururu mrefu wa malori yanayoingia Rwanda kutoka Tanzania kuanzia jana ambayo ilikuwa siku ya mwisho kabla ushuri huo wa kutoka Dola za Marekani 152 hadi 500 kuanza kutozwa tena kuanzia leo.
Kaimu Ofisa Mwandamizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kituo cha Rusumo, Sure Mohamed, jana alilithibitisha NIPASHE kwamba wiki moja iliyopita serikali ya Rwanda iliweka ongezeko la ghafla la ushuru wa barabara kutoka Dola 152 hadi Dola 500 za Marekani.
  Alisema hali hiyo ilisababisha msururu mrefu wa magari umbali wa zaidi ya kilometa 20 kwa kuwa madereva wengi hawakuwa na taarifa za ongezeko hilo, hali iliyowalazimu kuwasiliana na waajiri wao ili wawatumie fedha za ziada.
Hata hivyo, alisema ongezeko hilo la ushuru lililodumu kwa takribani wiki moja inakadiriwa magari zaidi ya 200 yalitozwa ushuru mpya wa Dola 500 kabla serikali ya Tanzania kufanya mazungumzo na serikali ya Rwanda na kufikia mwafaka wa kurejesha ushuru wa zamani wa Dola 152.
 
Alisema ingawa serikali ya Rwanda ilikubali kurejesha ushuru wa zamani, lakini baadaye iliweka bango mpakani upande wake lililosema tozo hiyo ya zamani ingedumu hadi jana na baada ya hapo malori yatatakiwa kulipa Dola 500.
“Ni kweli kulitokea ongezeko la ghafla la road toll (ushuru wa barabara) kwa upande wa wenzetu kutoka Dola 152 hadi Dola 500.

 
Tulipouliza kwa nini wamefanya hivyo tena ghafla, walidai wanataka kuwa na kiwango sawa na cha kwetu,” alisema.

Aliongeza kwamba kimsingi, madai hayo ya Rwanda kwamba wanataka kuwa na kiwango cha tozo sawa na cha Tanzania hayana ukweli wowote kwa sababu hapa nchini ushuru wa barabara unatozwa kulingana na umbali ambao gari linasafiri.
 
“Sisi hapa nchini tunatoza ushuru wa barabara kwa kuangalia kilometa, hiyo Dola 500 wanayodai tunatoza ni umbali wa kutoka hapa Rusumo hadi Dar es Salaam ambao ni zaidi ya kilometa 1,800,” alisema Mohamed.
Aliongeza kwamba kwa magari yanayoishia Isaka wilayani Kahama yanayotozwa Dola 110 tu, tofauti na Rwanda ambao wao kiwango chao ni kimoja hata kama gari litasafiri umbali wa nusu kilometa.

No comments: