Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, September 1, 2014

DIAMOND PLATNUMZ AZUA TAFLANI HUKO STUTTGART UJERUMANI. WATU WAANZA KURUSHA CHUPA, WENGINE WAZIMIA

Polisi nchini Ujerumani wamemnusuru Diamond kutoka kwenye mikono ya mashabiki wenye hasira waliochukizwa na kitendo cha mwimbaji huyo kufika ukumbini saa kumi alfajiri badala ya saa nne usiku kama walivyotarajia, wikendi iliyopita.
Kwa mujibu wa habari kutoka Ujerumani, mashabiki hao waliokuwa na hasira za kusubiri usiku mzima ujio wa Diamond jukwaani waligeuka mbogo alipoingia ukumbini hapo akiwa na promota M-nigeria aliyempeleka na hivyo wakaavamia jukwaa na kuanza kutembeza kipigo kizito kwa ma-DJ na baadhi ya watu waliokuwa wanahusika.

Hali ilivyokuwa ndani ya ukumbi baada ya vurugu
Taarifa hizo zinaeleza kuwa DJ Drazee alipewa kipigo kikali na kupelekwa na kupelekwa hospitali pamoja na DJ mwingine wa kike ‘DJ Flor’ ambaye alipata mshituko wa moyo.
Mashabiki hao walivunja vitu mbalimbali katika ukumbi huo ikiwa ni pamoja na vyombo vya muziki ambavyo vinaelezwa kuwa vilikuwa vibovu (havina ubora).
Polisi wanamsaka muandaaji wa show hiyo huku wakiendelea kuchunguza thamani ya hasara zilizosababishwa na vurugu hizo lakini pia watamfungulia mashtaka promota Britts ambaye ni raia wa Nigeria.

Polisi wakiwa nje ya ukumbi
Kupitia Instagram, Diamond ameandika ujumbe kuhusu tukio hilo na kulitolea ufafanuzi.
“kiukweli nimesikitishwa sana na uandaaji wa kampuni hii ya BRITTS EVENTS iliyoandaa show ya Stuttgart Germany, Promoter anatupeleka kwenye show saa kumi alfajiri. Naomba mtambue halikua kosa langu, mimi ni mgeni tu na ninafata maelekezo ya Promoter hivyo nisingeweza kujiamulia kuja muda ninaotaka mimi.

No comments: