Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, June 26, 2013

ATEKETEZA NYUMBA KUKIWA NA WATOTO WA JIRANI KISA MAPENZI.


MWANAMKE mmoja anayefahamika kwa jina la Taraji Muenzi, 31, mkazi wa kijiji cha Mwatasi, wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, anashikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo kwa kosa la kuichoma nyumba ya jirani yake na kuwateketeza watoto wawili waliokuwa ndani mwake pamoja na vitu vyote katika nyumba hiyo kwa kilichoelezwa wivu wa mapenzi.

Habari kutoka mkoani humo zinasema watoto walioteketezwa wakiwa ndani ya nyuma hiyo ni Faraji, 6 na Jacob, 3 ambao walikuwa watoto pekee wa Subira Kisitu aliyekuwa akituhumiwa na mtuhumiwa huyo kuwa anatembea na mumewe.

Inaelezwa kuwa Taraji kwa muda mrefu alikuwa akimtuhumu jirani yake kumuibia mume na kumchimba mkwara kwamba atamfanyizia, kiasi cha uongozi wa eneo lao kuitisha kikao na kumtwanga faini ya Sh 10,000 aliotakiwa kuilipa juzi, Juni 22 siku aliyofanya tukio hilo.Inaelezwa uongozi wa kitongoji hicho kiliamua kumtoza faini baada ya wiki iliyopita kumvamia jirani yake nyumbani kwake na kumwagia mboga na kusisitiza kuwa kuna kitu atakachomfanyia ambacho hatasahau maishani kama siyo kwa kumuua kwa sumu basi kwa kumchomea moto nyumba yake.

Hata hivyo inaelezwa kuwa jana juzi usiku akiamini kuwa jirani yake yupo ndani na wanawe aliamua kuichoma moto nyumba hiyo, ila kwa bahati mbaya jirani zake alikuwa klabuni akipata kinywaji na hivyo watoto pekee waliokuwa wamelala ndani ndiyo waliougua na kufa pamoja na mali zote.

Kamanda wa Polisi wa Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza wanamshikilia mwanamke huyo ili kumfikisha mahakamani kwa kitendo alichokmifanya ambacho kimeacha gumzo kijiji cha Mwatasi, huku familia ya watoto ikiwa katika majonzi makubwa ya kupoteza watoto wao.
chanzo:.

No comments: