Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, September 24, 2013

SPECIAL KWA WANANDOA TU

Mimi nimeoa na ndoa yangu ina miaka 7 sasa na tuna watoto wa 2. Nlimuoa mwanamke aliyekuwa kamaliza degree ambaye alikuwa home tu at the time anatafuta ajira. Toka nimuoe hajawahi kufanya kazi yoyote ile yaani Goalkeeper mpaka leo na kutafuta kazi alisha acha. Mpaka leo hii mke wangu hajabadilika. Namlipa mshahara mwisho wa mwezi ambao ni sawa na kama 10k per day yaani (300k). Kila ninapojaribu kumtafutia kazi anafanya kidogo tu anaacha. Huwezi amini hata umlazimishe vipi ajishughulishe mzito ile mbaya. Mi ni mfanyabiashara(Magari Makubwa) nimemuanzishia vimiradi through the years vyote kala mtaji. Kuna kipindi alijaribu kusoma masters ya bussiness administration nkamlipia ada, nunua vitabu vyote alafu yeye akaamua kuacha baada ya mwezi tu Eti kuamka alfajiri hawezi. Nkaja nkamuomba basi asome chuo ambacho atakuwa anaingia mchana nacho alishindwa.
Tatizo rafiki yake mkubwa ni mama yangu mzazi hivo kuna kipindi nlikata mshahara wake ili kumlazimisha afanye kazi akakimbilia kulia manyanyaso nikalazimishwa hela yake isiguswe na wazazi wangu. Nkienda kazini namuacha nyumbani na home kwenyewe hafanyi chochote anaita tu housegirl. Yaani yupo yupo tu siku hadi siku. Nifanyaje ili hata nikianguka leo au kesho awe ni mama atakayeweza kusomesha watoto.
Alafu matumizi yake ya hela mabaya yaani hela yake mwenyewe ukimpa mwanzo wa mwezi kwenye tarehe 1 hiv basi ikifika tarehe 8 ujue alikuwa anaumwa. Ila ni hela yake na hainunui hata nguo ya mtoto hivyo hainihusu.

No comments: