Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akielezea kufurahishwa
 kwake na Serikali Tanzania kwa kupigia hatua katika kutoa ajira nyingi 
kwa walimu kwenye mkutano huo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa 
Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez 
akizungumza na waandishi wa habari wa Zanzibar kwenye ofisi ndogo za 
mashirika ya Umoja wa Mataifa visiwani Zanzibar kuhusiana na mafanikio 
ya mradi wa kusaidia maendeleo nchini Tanzania (UNDAP) ulioanza mwaka 
2011 na sasa ukiwa ukingoni. Kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la 
Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) 
Tanzania, Zulmira Rodrigues na kushoto ni Mtaalam wa Mahusiano na 
Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu.
 **********
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
Zaidi
 ya watoto 3000 waliokuwa wakikabiliwa na utapiamlo nchini Zanzibar sasa
 wapo katika hali nzuri baada ya Umoja wa Mataifa (UN)kwa kushirikiana 
na wadau wengine kufanikisha programu ya kusaidia kukabili utapiamlo 
mkali kwa watoto hao.
kauli
 hiyo imetolewa katika mkutano wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
waandishi wa habari uliofanyika hivi karibuni ambapo UN ilielezea 
mafanikio ya mradi wa kusaidia maendeleo nchini Tanzania (UNDAP) 
ulioanza mwaka 2011 na sasa ukiwa ukingoni.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez alisema 
kwamba Umoja huo ukiadhimisha miaka 69 ya uwepo wake imefurahishwa na 
maendeleo yaliyopatikana katika maeneo ambayo ilikuwa imejikita kusaidia
 kukabili umaskini,kuhakikisha utawala bora na kusaidia jamii.
 
 
No comments:
Post a Comment