Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, December 3, 2012

KAJALA KAFUTUKA FUTUUH GEREZANI..!!


MSANII wa filamu Bongo ambaye yuko nyuma ya nondo Gereza la Segerea, Dar es Salaam kwa mashitaka ya kuuza nyumba iliyowekewa kizuizi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Kajala Masanja anaweza kupata gonjwa la moyo kufuatia kunenepa sana akiwa gerezani humo.
Kajala Masanja wakati akipandishwa katika Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam Jumatatu wiki hii. Kajala aliyepandishwa katika Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam Jumatatu iliyopita, muonekano wake kwa sasa uliwashangaza watu katika mahakama hiyo baada ya kuonekana amenenepa sana kuliko alivyokuwa uraiani.
Baadhi ya watu walisikika wakihojiana wenyewe kwa wenyewe kama kuishi gerezani kwa muda mrefu kunasababisha mtu kunenepeana kama yeye.
“Hivi kumbe gerezani kunaweza kumnenepesha mtu jamani? Kajala shavu dodo,” alisema mwanamke mmoja ambaye mwenzake alikuwa kinyume naye.
Mwenzake: “Ila kunenepa kwa aina hii halafu unakaa kwa muda mrefu kuna hatari ya kupata magonjwa ya moyo. Unajua uraiani chakula kinachukuliwa na kazi za siku nzima, gerezani muda mwingi ni kukaa tu, inabidi afanye mazoezi ya kupungua.”

Kajala akionekana kanenepa kuliko alivyokuwa uraiani. Mwingine: “Dah! Hebu mcheki kwanza, yaani anazidi kuwa bomba kila kukicha, sasa hivi amekuwa shavu dodo kuliko hata alivyokuwa uraiani! Tusidanganyane jamani, piga ua kutakuwa na mtu anamtunza huyu hukohuko aliko si bure. ”
Hata hivyo, miongoni mwa waliodatishwa na muonekano wa Kajala ni msanii mwenzake, Mahsein Awadh ‘Dokta Cheni’ ambaye alimsogelea na kutaka kumkumbatia lakini alizuiliwa na askari waliokuwa wakimlinda.

...akiwa na sura ya tabasamu.

No comments: