Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, March 22, 2012

BASATA KUVIJADILI VIKUNDI VYA UNENGUAJI VINAVYOKIUKA MAADILI

PRESS RELEASE
KUWEPO KWA VIKUNDI VYA WANENGUAJI NA BENDI ZINAZOKIUKA MAADILI YA KITANZANIA
Katika siku za karibuni kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa maadili kupitia maonyesho ya majukwaani na kazi mbalimbali za Sanaa.
Kutokana na hali hii, Baraza la Sanaa la Taifa kupitia programu ya Jukwaa la Sanaa Jumatatu ya Tarehe 26/03/2012 litakuwa na mada maalum ya Unenguaji na Maleba Katika Muziki.
Mada hii itakayowasilishwa na Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (CHAMUDATA) na asasi ya Sanaa ya Binti Leo pamoja na mambo mengine itaangalia hali halisi ya Sanaa ya unenguaji, maleba na matatizo yaliyopo na hatua zinazopaswa kuchukuliwa.
BASATA inatoa wito kwa wadau wote wa Sanaa na wapenzi wa Utamaduni wan nchi yetu kujitokeza kwa wingi siku hiyo kushiriki kuchangia mwelekeo mpya wenye maadili sahihi ya kitanzania.
Sanaa ni Kazi Kwa Pamoja Tuikuze na Kuithamini.
Ghonche Materego
KATIBU MTENDAJI, BASATA

No comments: