Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, April 19, 2012

ZITTO KABWE AZILIPUA TANESCO NA ATCL


Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imependekeza kwa serikali iwakamate na kuwafikisha mahakamani maofisa wa serikali walioingia mkataba wa ukodishaji wa ndege ya ATCL, Air Bus 420-214, mwaka 2007.

Hali kadhalika, kamati hiyo imelishutumu Shirika la Umeme nchini (Tenesco), kwa kufanya manunuzi ya Sh. bilioni 600 bila kufuata sheria za manunuzi.

Hayo yalisemwa bungeni jana na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe, wakati akiwasilisha taarifa yake, kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2010.

Zitto alisema fedha hizo ni nyingi hivyo ni muhimu msisitizo na hatua za kisheria zitaendelea kuchukuliwa kwa taasisi zote ambazo zinakiuka sheria za manunuzi ya umma  kuisababishia serikali hasara kubwa.

No comments: