Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, January 9, 2013

MWANDISHI WA HABARI APIGWA RISASI NA KUNYOGWA HADI KUFA MKOANI KIGOMA

Mwansidhi wa Habari wa Kituo cha Redio Kwizera wilayani Kakonko, Mkoa wa Kigoma, Issa Ngumba (45) enzi za uhai wake.
 MWANDISHI wa Habari wa Kituo cha Redio Kwizera wilayani Kakonko, Mkoa wa Kigoma, Issa Ngumba (45), ameuawa kwa kupigwa risasi na kunyongwa na watu wasiofahamika.

Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa mwili wa mwandishi huyo ulikutwa porini, siku tatu tangu alipotoweka nyumbani kwake katika mazingira ya kutatanisha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Frasser Kashai alithibitisha tukio hilo, lakini akasema asingeweza kulizungumzia kwa undani kwa kuwa polisi walikuwa bado eneo la tukio.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwandishi huyo alikutwa jana akiwa amekufa, huku mwili wake ukiwa na majeraha ya risasi na ukiwa umenyongwa na pembeni yake kulikuwa bastola iliyokuwa imetelekezwa pamoja na simu zake mbili za mkononi.

“Mwili wake ulipatikana jana katika Pori la Mlima Kajuluheta ulioko katika Kijiji cha Muhange, Kakonko asubuhi baada ya wananchi kufanya msako wa siku tatu tangu Jumapili iliyopita ikiwa ni siku moja baada ya kupotea katika mazingira ya kutatanisha,” alisema mmoja wa  mashuhuda hao.

Imeelezwa kuwa pamoja  na vifaa hivyo, pia katika eneo hilo la tukio kulikutwa risasi tano na katika mfuko mmoja wa suruali ya marehemu, kulikuwa na noti moja ya Sh10,000.

Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Kigoma (KPC) Deogratius Nsokolo alisema: “Sisi ndiyo kwanza tunaelekea eneo la tukio, lakini waandishi wa Wilaya ya Kibondo ambao waliwahi kufika eneo la tukio na kushuhudia uchunguzi wa daktari, wameeleza kuwa marehemu amekufa kwa kunyongwa na kupigwa risasi mkono wa kushoto.”

“Tunaelekea Wilaya ya Kakonko kutoka Kigoma Mjini, lakini daktari amesema maiti inaonekana kunyongwa shingo na kupigwa risasi mkononi.”

Alisema mwili huo ulifanyiwa uchunguzi na daktari Primus Ijumaa wa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo.

Kamanda Kashai alisema jeshi lake linasubiri taarifa ya daktari aliyefanya uchunguzi wa mwili wa marehemu pamoja na taarifa za awali za uchunguzi kabla ya kutoa taarifa kamili kwa waandishi wa habari.

Naibu Mhariri wa Kituo cha Redio Kwizera kinachorusha matangazo yake kutoka wilayani Ngara mkoani Kagera, Seifu Upupu alisema mwandishi huyo alipotea tangu Januari 5, mwaka huu saa kumi na moja jioni.

“Simu zake zilikuwa zikiita bila kupokewa kwa muda wote na hadi jana (juzi) zikawa hazipatikani kabisa,’ alisema Upupu na kuongeza:

No comments: