Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, January 3, 2011


MAJINA MATATU YAINGIA FAINALI “TUZO YA SHUJAA WA SAFARI LAGER”.



MAJINA MATATU YAINGIA FAINALI
TUZO YA SHUJAA WA SAFARI LAGER”.
Dar es Salaam, Jumatatu 03, 2011: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager na ushirikiano wa kituo cha ITV na Radio One, leo wameweka hadharani majina matatu yaliyofanikiwa kuingia fainali za tuzo ya “Shujaa wa Safari Lager”. Majina ya mashujaa hao ambao wanawania tuzo ya hiyo maalum ni:-
A. MERCY SHAYO – BOMANG’OMBE, KILIMANJARO
B. PAUL LUVINGA – SINZA E, DAR ES SALAAM
C. LEONARD MTEPA – MWANANYAMALA A, DAR ES SALAAM
Akitangaza majina hayo, Meneja wa Bia ya Safari Lager Fimbo Butallah alisema; “Tulipokea mapendekezo mengi toka kwa wananchi wakipendekeza mashujaa wao na mambo waliyofanya kwa jamii, kazi iliyofuata ilikuwa ni kupitia na kuchambua mapendekezo hayo kwa kuangalia vigezo muhimu, ili kuweza kupata majina matatu yatakayoingia fainali. Hatua inayofuata ni kuchapisha mambo waliyofanya mashujaa hawa watatu katika magazeti na kutangaza katika Televisheni na Redio ili wananchi wote waelewe na kisha waweze kupiga kura ili kuchagua shujaa wanaetaka atwae tuzo hii ya “Shujaa wa Safari Lager 2010”.
Tunapenda kuwakumbusha wananchi wote kuwa mshindi wa tuzo hii ya Shujaa wa Safari atajinyakulia kitita cha shilingi milioni 7, pia kutakuwa na shilingi milioni 3 ambazo zitasaidia shughuli yoyote ya kijamii atakayopendekeza shujaa huyo mahali anakotoka. Mashujaa wawili waliobaki wao watapata kifuta jasho cha shilingi milioni 1 kila mmoja.





 GIRAFfE UNIQUE MODEL 2010

                                                     Katikati ni mshindi wa (asia dachi)UNIQUE MODELOF YEAR 2010,WPILI ALIKUWA DIANA HAMSON KULIA NA MARIAM RABII WATATU
                                       

                                       Tano bora ya GIRRAF UNIQUE MODEL.diana hamsin,caroline mwakasaka,mariam rabii,asia dachi na bilkis suleiman

CHINA YAAHIDI KUSAIDIA SEKTA YA SANAA NCHINI

 Balozi muambata wa utamaduni wa China, Liu Dong akifafanua jambo wakati alipomtembelea Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego (Kulia) ofisini kwake Ilala,Sharif Shamba wiki hii.Katikati ni wakurugenzi idara mbalimbali za BASATA              
Katibu Mtendaji wa BASATA,Bw.Materego akisisitiza juu ya uimarishaji wa uhusiano wa kitamaduni kati ya China na Tanzania wakati alipopokea ugeni wa maafisa watatu kutoka Ubalozi wa China ukiongozwa Balozi muambata wa utamaduni Bw.Liu.
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeingia kweye makubaliano na ubalozi wa China nchini ya kubadilishana kazi za sanaa na wasanii mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha mashirikiano ya kiutamaduni na kukuza sekta hiyo nchini.

Akiwa katika ziara yake BASATA ambayo aliambatana na maofisa wawili wa ubalozi wake Huang Wei na Wang Hong,Balozi muambata wa utamaduni kutoka China,Liu Dong amesema kwamba nchi yake imejipanga kusaidia sekta ya utamaduni nchini kwa kuwashirikisha watanzania kwenye matamasha mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ikiwa ni pamoja na kujenga miundombinu ya sekta hiyo.

Bw.Liu alikubaliana kimsingi na BASATA katika kuimarisha mahusiano ya kiutamaduni ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati ya kuwezesha ubadilishanaji wa kazi za sanaa na wasanii ili wapate fursa za kuuza kazi zao, kujitangaza na kushiriki katika matamasha mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

“China kwa sasa inaweka nguvu kwenye suala la kubadilishana utamaduni baina ya mataifa haya mawili.Tunategemea kuwashirikisha wasanii wa Tanzania katika matamasha mbalimbali tutakayoyaandaa pamoja na kuwapeleka nchini China kwa ajili ya kuongeza na kubadilishana ujuzi” alisisitiza Liu huku akitaja sanaa za uchongaji, filamu, uchoraji, ngoma za asili, sarakasi na nyinginezo kuwa watazipa msisitizo.

Kwa kuanzia Balozi huyo wa China alisema kwamba,wasanii wa Tanzania watapata nafasi ya kushiriki matamasha na maonesho ya kuazimisha mwaka wa China ambayo yanatazamiwa kuanza mwishoni mwa Februari mwaka 2011 ambapo pamoja na wasanii kutoka Tanzania watakuwepo pia magwiji wa tasnia hiyo kutoka China pamoja na waandishi wa habari maarufu.

Kwa upande wake,Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego alisema kwamba, ziara hiyo ya maofisa wa ubalozi wa China ambayo imekuja baada ya ile ya awali ya maofisa wa Baraza ubalozini kwao ni yenye manufaa makubwa na italeta tija kubwa katika tasnia ya sanaa na utamaduni kwa ujumla hasa ukizingatia wasanii wamekuwa na uhitaji mkubwa wa maonyesho na masoko ya kazi zao.

Alingeza kwamba,BASATA iko tayari kusaidiana na China katika masuala mbalimbali ya ukuzaji wa sekta ya sanaa huku akiweka wazi kwamba,uhusiano wa China na Tanzania ni wa muda mrefu sana hivyo kuna kila sababu ya kuuendeleza na kuuimarisha zaidi.

“Kama kuna suala lolote mtakalohitaji tuwasaidie katika kukuza ushirikiano wa kiutamaduni sisi tuko tayari na milango iko wazi.Bila shaka eneo hili la mashirikiano ya kiutamaduni ni nyeti sana na hatuna budi kulipa msukumo wa kipekee” alisisitiza Materego

No comments: