Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, January 31, 2011

   VURUGU ZA MACHINGA NA POLISI JIJINI MWANZA

JIJI la Mwanza jana lilikumbwa na machafuko baada ya machinga kufanya vurugu na kuandamana wakipinga kuondolewa kufanya biashara katika maeneo ya mjini kati. Vurugu hizo zilisababisha kufungwa kwa maduka katika maeneo mbalimbali mjini hapa, kuvunjwa vioo vya magari, maduka na baadhi ya barabara kutopitika kwa muda huku kituo kidogo cha Polisi Pamba, kikinusurika kuvamiwa na kuchomwa moto.MKUU WA MKOA WA MWANZA ABBAS KANDORO AKIZUNGUMZA NA WAANDAMANAJI HAO KUPITIA GARI LA FFU, KULIA MWENYE SHATI YA BLUE NI MWENYEKITI WA WAMACHINGA MZ.
Pamoja na vurugu hizo, serikali mkoani Mwanza imewataka wafanyabiashara hao kuheshimu sheria na kanuni za mipango miji zilizowekwa pia maafikiano yaliyofikiwa baina ya viongozi wao, uongozi wa mkoa na halmashauri ya jiji hilo .

Vurugu hizo zilizodumu kwa zaidi ya saa sita, zilianza saa tatu asubuhi baada ya mgambo wa jiji na askari wa kutuliza ghasia kuwatawanya wafanyabiashara hao katika maeneo ya Makoroboi, Mission na Soko Kuu. 
Nje ya jengo hilo , waliweka vizuizi vya mawe katika barabara zote zinazoingia jiji na kulazimisha pikipiki na magari yaliyokuwa yakipita kurudi yalikotoka huku wakiwa na chupa za maji ya kunawa kwa ajili ya kujikinga na moshi wa mabomu iwapo polisi wangewafyatulia mabomu ya machozi.
Hali hiyo ilisababisha polisi wa kutuliza ghasia na makachero kuweka ulinzi mkali katika lango kuu la kuingilia jiji hadi viongozi akiwemo Mkurugenzi wa jiji Wilson Kabwe na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro walipofika na kufanya mazungumzo na viongozi wa machinga hao.

Baada ya mazungumzo hayo, Kandoro aliwaambia machinga kuwa hapingani na sheria na kanuni za mipango miji kwa kuruhusu machinga wafanye biashara katika maeneo waliyoruhusiwa, isipokuwa wafuate masharti waliyopewa katika maeneo ya Makoroboi, Mirongo, Vitunguu Soko Kuu na Mlango Mmoja.

AJALI KATIKA PILIKA ZA KUNUSURU BIASHARA.
Baada ya kuondoka katika ofisi za halmashauri hiyo, machinga waliingia mitaani tena na kuanza vurugu wakivamia maduka na kuvunja vioo kwa madai kwa wafanyabishara wengine, hawatafanya biashara.

No comments: