Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, December 4, 2013

PENZI LA CHUCHU LANOGEA RAY ATAKA KUOA KABISA

Akizungumza wikiendi iliyopita katika Viwanja vya TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam ambapo kulikuwa na mechi kati ya wasanii wa Bongo Fleva na Bongo Muvi, Ray aliwashangaa waandishi kwa kumshambulia kutoka kimapenzi na Chuchu.

Mwandishi alianza kwa kumwuliza: “Ray magazeti yanaandika kuhusu wewe kutoka na Chuchu Hans ambaye ni mke wa mtu. Mainda amezungumza mengi. Kukaa kwako kimya bila kufafanua chochote siyo kitu kizuri. Tafadhali, hebu zungumza japo kidogo kuhusu madai ya Mainda.”

RAY: Sikia nikuambie, huyo Mainda utoto unamsumbua. Haniumizi kichwa kabisa. Kuhusu Chuchu... si mmeshaandika? Endeleeni kuandika lakini soon mtashuhudia kitu kikubwa sana.
RISASI: Ni kitu gani hicho?

RAY: Niacheni na Chuchu wangu.... kifupi ndiye mke wangu na itawashangaza wengi. Halafu mimi nawashangaa sana. Yaani mimi kutoka na Chuchu mnakuzaaaa... mbona alivyokuwa na ma-boyfriend zake wengine hamkuandika? Kwa sababu ni Ray basi mkaona ni habari. Mimi ninavyojua Chuchu siyo mke wa mtu.
Kwanza mimi sijamchukua kutoka mikononi mwa mumewe kama mnavyosema. Chuchu tayari alikuwa na maisha yake mapya. Nilimchukua kutoka kwa Libert (hajafafanua zaidi ni nani). Mbona alivyokuwa na huyo Libert  hamkuandika? Kifupi niacheni na maisha yangu.

RISASI: Vipi kuhusu Johari?
 

RAY: (Huku akikimbia kuingia uwanjani) Tena huyo mama yako (akimuonesha mwandishi Johari) anakuja.
Mwandishi wetu aliachana na Ray aliyekuwa akiingia uwanjani na kumfuata Johari lakini hakuwa tayari kusema chochote achilia mbali hata kumsikiliza mwandishi wetu!

No comments: