Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, May 19, 2011

BREAKING NEWS..!! OSAMA ACHEZA FILAMU YA NGONO..!!

0518_oooohsama_hustler_ex_tmz
        It's called "This Ain't Osama bin Laden XXX" -- and the porn studio claims Osama's secret porn stash was a major inspiration ... telling us, "We're pretty sure from what we've heard that bin Laden was a big fan of Hustler. He was looking at porn, now porn is looking at him."


T-PAIN AMZIMIA KESHA INOMA NOMA..!!

Msanii Tallahassee Pain "T-Pain" na Mkali wa Pop/Female Rapper Ke$ha wameonekana wamepiga picha ya kimahaba  na kwa sasa kuna uvumi kuwa wanatupa mbicji
T-Pain na Ke$ha walionekana jijini Las Vegas,na walikuatana weekend moja kwenye show ya Wango Tango na T-Pain na kuanza kumfukuzia.
  kutupia kwenye Twitter T-pain alisema “Usiku wa jana nilimzimia sana Ke$ha,wala siku-share nae mapenzi,ila namzimia coz anajua kutupia akitaka kufanya showz” na baadaye Ke$ha naye akajibu “hata mimi nakuzimia T-Pain,usikonde wala nini” na baadaye kwenye tweeter zikatupiwa picha zao zilizoandikwa K-Pain aka Ke$ha-Pain.


HALI TETE KWA WILLIAM LUKUVI NA CYRIL CHAMI
Mh.William Lukuvi
Kwa mara nyingine,KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amewataja vigogo na watendaji wa serikali wakiwamo mawaziri wawili na wabunge akiwatuhumu kufanya ufisadi wa kujigawia vitalu vya uvunaji magogo katika msitu wa taifa uliopo Mufindi mkoani Iringa.
Miongoni mwa aliowataja ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami, huku akisisitiza kuwa wamepata vitalu hivyo ‘kifisadi’.
Dk. Slaa aliwataja mawaziri hao na watuhumiwa wengine wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Mafinga katika mfululizo wa mikutano ya hadhara na maandamano ya chama hicho yaliyoingia mkoani hapa jana.
Alisema hatua ya mawaziri hao kumiliki vitalu hivyo si haki, kwani inasababisha kuwapo mgongano wa kimasilahi baina yao na msitu huo ambao kwa nafasi zao kama viongozi wa kiserikali walipaswa kuusimamia kwa haki na uwazi ili uwanufaishe wananchi, hususan wakazi wa Mufindi.
Akifafanua hoja yake hiyo, Dk. Slaa alisema Dk. Chami kwa nafasi yake kama Waziri wa Viwanda na Biashara, ndiye mwenye jukumu la moja kwa moja kusimamia haki kwenye msitu huo unaotumiwa pia na Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi Paper Mills, lakini naye amechukua vitalu tena katika utaratibu aliosema si wa wazi.
Alisema mwaka jana waziri huyo akiwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ndiye aliyeongoza kamati maalumu ya serikali iliyokwenda Mufindi kuchunguza mgogoro wa kiwanda hicho pamoja na msitu kinaoutumia, lakini kinyume cha kanuni za kibunge, kiongozi huyo wa serikali sawa na wenzake akiwamo William Lukuvi aliowataja, hawakusema wazi kama wana masilahi katika msitu huo.
“Naitaka serikali ieleze ugawaji huu wa vitalu vya msitu wa Mufindi ulitangazwa lini na utaratibu gani wa uwazi ulitumika ili kila Mtanzania wakiwamo wananchi wenyewe wa Mufindi wawe na haki ya kushindania vitalu hivyo.
“Pili, namtaka Chami na viongozi wengine wa kiserikali waliochukua vitalu vya msitu huo wajieleze kwa nini wasiwajibishwe kwa kumiliki vitalu vya msitu bila kutangaza wazi masilahi waliyonayo ya kiuongozi katika msitu huo.
“Tutawasha moto bungeni mpaka haki ya wananchi na msitu wao ipatikane, hawa ni mafisadi. Wakituzidi kwa wingi wao bungeni, basi tutafanya maandamano yasiyokoma nchi nzima hadi mafisadi hawa wawajibishwe na haki za wananchi zitimizwe,” alisema Dk. Slaa na kushangiliwa na umati wa watu.


Mkuu wa IMF Ajiuzulu

Dominique Strauss-Kahn
Mkuu wa IMF Dominique Strauss-Kahn mahakamani
Mkuu wa shirika la fedha duniani, Dominique Strauss Kahn amejiuzulu.
Taarifa hiyo ya kujiuzulu kwa Strauss Kahn imechapishwa katika wavuti wa shirika hilo.
Anasema amejiuzulu ili atumie muda uliobakia kujitea katika kesi inayomkabili ya kujaribu kumbaka mwanamke mmoja mjini New York.
Strauss Kahn ametuma taarifa yake kwa bodi ya shirika hilo. Amesema kuwa anakanusha mashtaka yote dhidi yake na amesikitishwa na kisa hicho kilichomkabili.
Shirika hilo limesema kuwa litatangaza hivi karibuni utaratibu wa kumteua mkurugenzi mpya. Kwa sasa John Lipsky ataendelea kuwa kaimu Mkurugenzi mkuu wa IMF.
Awali waziri wa fedha wa Marekani amesema kuwa mkuu wa shirika la fedha duniani (IMF), Dominique Strauss-Kahn, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya kujaribu kumbaka mhudumu wa hoteli, hawezi tena kuendesha shughuli za shirika hilo.
Timothy Geithner ametoa wito kwa IMF kumteua rasmi kaimu mkuu wa shirika hilo.
Bwana Strauss-Kahn anazuiliwa katika jela moja mjini New York baada ya kukamatwa hapo jumamosi kwa kosa la kujaribu kumbaka mhudumu wa hoteli moja.
Strauss-kahn ambaye amezuiliwa katika gereza la wafungwa sugu la Rikers Islands mjini New York yupo chini ya ulinzi mkali kuchunga asijiue. Hii ni baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
Wakili wa mwanamke huyo kutoka Guinea, Afrika Magharibi, anayemtuhumu Strauss-Kahn, amesema mteja wake amepata mshutuko ambao sio wakawaida.
Wakili huyo ameongeza kuwa kwa sasa yupo mafichoni na kwamba anajihisi ''Yuko pekee duniani''.
Strauss-Kahn, mwenye umri wa miaka 62, anakabiliwa na mashtaka saba dhidi yake na iwapo atapatikana na hatia, atahukumiwa kifungo cha hadi miaka 25 jela.


 AMBER ROSE NA MAUZO YA FRONT PAGE
Amber rose amepata shavu la kuuza front page katika jarida la king kwa mara nyingine.

No comments: