Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, June 2, 2011

MISS UTALII YAWEKWA KITIMOTO NA BASATA

Rais wa Miss Utalii ambaye pia ni muandaaji wa Shindano la urembo la utalii,Bw.Chipungahelo akitoa maelezo kuhusu shindano lake kwenye kikao hicho cha tathimini.Kushoto kwake ni Bi.Shalua.

Baadhi ya waliokuwa washiriki wa shindano la Miss Utalii lililopita wakifuatilia kikao cha tathimin. 
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha kikao maalum cha kutathimini shindano la urembo la utalii (miss utalii) linalofanyika kila mwaka ambapo wito umetolewa kwa waandaaji wa shindano hilo kufuata kanuni na taratibu zilizopo.
Akizungumza kwenye kikao hicho kilichofanyika wiki hii kwenye Ukumbi wa BASATA,Mkurugenzi wa Idara ya ukuzaji Sanaa wa baraza hilo,Bi Vivian Shalua alisema kwamba,shindano la miss utalii limebeba utambulisho wa taifa hivyo waandaaji hawana budi kujipanga na kufanyia kazi mapungufu yote yanayokuwa yanajitokeza

 

Misri na Cameroon njia panda kufuzu

Misri na Cameroon zina kibarua licha ya ushindi wa Kombe la Mataifa mara kumi na moja baina yao. Timu hizi zina shughuli pevu kuvuka michuano ya kufuzu kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2012.
Misri yasherehekea kombe la Mataifa ya Afrika
Misri yasherehekea kombe la Mataifa ya Afrika

Misri iliyo katika chungu chenye moto inahitaji ushindi dhidi ya Bafana bafana mjini Cairo siku ya jumapili vinginevyo itaondolewa kwenye mashindano iliyoyatawala na kushinda mara saba ikiwa ni mara tatu mfululizo hadi sasa.
Endapo Cameroon itashindwa ugenini Senegal siku ya jumamosi huenda tukawakosa wachezaji kama Samuel Eto'o wa Inter Milan na Alex Song wa Arsenal.

Michael Essien anatarajiwa kurejea uwanjani kwa mara ya kwanza kuinua matumaini ya Ghana baada ya kukaa nje ya mechi za kimataifa kwa zaidi ya mwaka mzima Black stars itakapochuana na Jamhuri ya Congo.
Timu zitakazomaliza kwa pointi bora katika nafasi ya pili zitafuzu timu 12 zilizofuzu moja kwa moja kujiunga na mwenyeji wa mashindano haya Gabon na Equatorial Guinea. Hata hivyo Misri na Cameroon hazijaonyesha kiwango cha hata kufuzu kupitia mlango wa nyuma.
Timu hizi zinakabiliana na timu zilizowararua dakika ya mwisho wakati wa michuano ya awali.
Misri inaburura mkia wa kundi G na itakosa kufuzu tangu mwaka kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1978 endapo watachapwa na Bafana Bafana na kisha Niger iliyo katika nafasi ya pili ishinde mechi yake dhidi ya Sierra Leone.
Tayari mechi hiyo iliyopigiwa debe vilivyo imehamishiwa uwanja wa kijeshi badala ya uwanja mkubwa wa Kimataifa kwa hofu ya mashabiki wake kuzusha ghasia endapo matokeo yatakwenda kinyume na matarajio yao.
Cameroon ilipoteza mecji yake dhidi ya viongozi wa kundi E Senegal ambapo Simba hao wa nyika wanajikuta mkiani mwa kundi hilo kwa pointi tano.

No comments: