
Takriban wafungwa 300 wameuwawa katika moto ulioteketeza jela moja nchini Honduras kwa mujibu wa maafisa wa serikali.

Wengi wao waliteketea au kukosa hewa katika seli zao za jela ya Comayagua, kaskazini mwa mji mkuu Tegucigalpa.
Maafisa wa serikali wanasema imethibitishwa takriban 300 wamekufa lakini wengine 56 kati ya wafungwa 853 katika gereza hilo hawajapatikana na inadhaniwa wameteketezwa.


Rais Lobo wa Honduras ameahidi uchunguzi kamili ulio wazi na kusema hillo ni janga lisilokubalika.
Alisema wakuu wa magereza wa kitaifa na wa eneo la moto huo watasimamishwa kazi wakati uchunguzi ukiendelea.
No comments:
Post a Comment