MAMBO YA KIDOSI NA UFUGAJI WA DHATI


TAMKO LANGU KUHUSU MOVIE YA FAMILY DISASTER

Kipindi cha tangu kuzaliwa mwana mpaka kufikia umri wa kwenda shule, huwa ni kipindi cha matunzo kwa mwana; anatunzwa kwa ajili ya kufikia utu uzima aweze kujitegemea akiwa katika afya njema tayari kukabiliana na majukumu ya utu uzima.Kwa upande mwingine, kipindi cha malezi huanza pale watoto wanapofikia umri wa miaka kumi na ziada,kwani hapo mtoto anakuwa tayari kwa maandalizi ya kuwa mtu mzima. Kipindi hiki huwa kinamfanya mtoto kuwa mdadisi mno kwa kila kitu anachokiona hususani yale yanayohusiana na mambo ya kimahusiano; kipindi hiki ni kipindi muhimu sana kwa wazazi na watoto kwani inatakiwa kuwa karibu sana kuliko kipindi chochote kwani watoto wana matarajio makubwa sana kutoka kwa wazazi wao kwa kila wanachohitaji kukijua,na kwa kuwa wazazi tayari wameshashuhudia kipindi kama hicho inakuwa rahisi kwao kuwaelekeza,kinyume chake mambo yatakuwa mabaya kuliko inavyofikiriwa.
FAMILY DISASTER ni kisa kinachoonesha jinsi wazazi wanaposhindwa kukubali kuyatwaa majukumu yao na kuharibu kabisa ustawi wa familia zao.Wazazi kwa kuthamini sana nafsi zao kuliko za watoto wao,wanajikuta wakivutana badala ya kuwalea watoto wao,kitu ambacho kinasababisha watoto hao kukosa kupata malezi ya mambo muhimu na kujikuta wakiiga tabia mabya kutoka kwa majirani,marafiki na watu wengine wasio na maadili, kwasababu ustawi wa familia haupo.Sina maana mbaya kutengeneza filamu hii, Maana yangu ni nzuri tu nia ni kuelimisha jamii .Kuhusu kuvaa nguo fupi ni jinsi story inavyotaka maana hawa watoto wameigiza kama watukutu waliokosa maadili.Wadau nisimalize uhondo nataka mtambue kitu kimoja katika maisha kuwa huwezi kujifunza kitu bila kukosea .Nina uhakika tena mkubwa sana filamu hii itakuwa fundisho kubwa kwa wazazi na watoto wote wasiokuwa na maadili. Naomba tusubiri wadau.
Taylor Swift's Ex-Manager Sues for Millions
EXCLUSIVE: Did Taylor Swift's father conspire to cheat her former manager out of millions of dollars earned by launching the Grammy-winning country star?

No comments:
Post a Comment