Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, December 2, 2011

BREAKING NEWS: MR.EBBO AFARIKI DUNIA

                                                       Ndugu wenzangu usiku wa jana, kuna ujumbe wa kusikitisha sana ya kwamba Abel Motika a.k.a Mr. Ebbo ambae ni msanii na pia ni producer wa muziki katika studio yake ya Motika Records mjini Tanga ameaga duniani,taarifa zilizopatikana kwa jirani yake wa Mr.Ebbo amesema kuwa alikuwa anaumwa na alikuwa amelazwa hospitali ya Mount Meru na  usiku ndipo alifunga ukrasa wake wa maisha na safari yake ya kuishia ndio ulifika mwishoni mwa jana saa 5 usiku.


WAZIRI MWANDOSYA AREJEA NYUMBANI
Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya, aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Apollo, nchini India, kwa takriban miezi minane, amerejea nchini, baada ya afya yake kuimarika. Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam zilizothibitishwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Gerson Lwenge, Profesa Mwandosya alirejea nchini juzi. Mwingine aliyethibitisha jana kurejea kwa waziri huyo mwandamizi, ni mkewe, Lucy Mwandosya. Hata hivyo, Mhandisi Lwenge, ambaye alizungumza na jana, alipotakiwa kueleza maendeleo ya afya ya Waziri Mwandosya, alijibu: “Sijamuona, ndio naenda. Ukinitafuta baadaye nitakwambia.” Awali, Mhandisi Lwenge, alipoulizwa kama Waziri Mwandosya amerejea nchini, alijibu: “Ndio amerudi” na alipotakiwa kueleza lini alirejea, alijibu: “Jana (juzi).” Baadaye, majira ya saa 11.05 jioni jana, ilimtafuta Profesa Mwandosya kwa simu yake ya mkononi, ambayo ilipokelewa na mkewe, Lucy. Baada ya mwandishi kujitambulisha na kueleza shida yake ya kutaka kuzungumza na Profesa Mwandosya, Lucy, alisema muda huo waziri asingeweza kuzungumza kwa vile alikuwa anapumzika.

MILIONI 55 ZAKUSANYWA RED RIBBON FASHION SHOW


WAKATI jumla ya sh. Milioni 55 zimechangishwa katika maonyesho ya mitindo kwa ajili ya kuadhimisha siku ya ugonjwa hatari wa UKIMWI duniani (Red Ribbon Fashion Gala), mwanamuziki nyota nchini, Diamond aling’ara vilivyo kwa kuonyesha kipaji kingine cha maonyesho ya mavazi.
Fedha hizo zilipatikana kwa njia ya mnada wa vitu mbali mbali na nyingine zikitolewa kwa njia ya udhamini wa shughuli hiyo iliyotumika pia kuadhimisha siku ya ugonjwa hatari wa Ukimwi Duniani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Mitindo House (TMH), Khadija Mwanamboka aliwashukuru wadau wa maonyesho ya mavazi kwa kujitolea kufanikisha kupatikana kwa fedha hizo ambazo zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mafunzo ya fani mbali mbali kwa watoto yatima wanaoishi na virusi vya Ukimwi.
Mwanamboka alisema kuwa kituo hicho kitajengwa jijini na kitatoa mafunzo ya njia mbali mbali za kupambana na maisha, Ujasiliamali, Ushonaji nguo, mafunzo ya kompyuta na jinsi ya ubinifu wa mitindo au mavazi. Alisema kuwa jumla ya watoto yatima 100 watakuwa wanapata mafunzo katika kituo hicho kila mwaka.
Baadhi ya wadhamini waliochangia kufanikisha kwa fedha hizo ni kampuni ya simu ya mkononi, Vodacom Tanzania na wadau wa maonyesho ya mavazi ambao walichangia kimya kimya katika maonyesho hayo yaliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree.
Katika maonyesho hayo, mkali wa miondoko ya Bongo Fleva nchini, Diamond naye alifanya vitu vyake jukwaani kwa kuvaa nguo aina ya Kidoti iliyobuniwa na mbunifu chipukizi, Jokate Mwegelo.
Wengine walioonyesha mavazi jukwani ni Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Production, Ritha Poulsen ambaye baadaye nguo yake iliunuliwa na mcheza filamu maarufu nchini, Steven Kanumba.
Wabunifu mbali mbali akiwemo Doreen Estazia nao walionyesha mavazi yao, Doreeen alionyesha mitindo yake maarufu ya Eskado Bird. Wabunufu wengine waliotamba katika maonyesho hayo ni Ali Rhemtullah, Diana Magese, Mollel na Zamda.
Wadhamini wengine wa shughuli iyo walikuwa Redds, Clouds Entertainment, Kiondo Communications, I_View Media team na Hall Neel Production. Wengine waliosaidia maonyesho hayo ya mavazi ni Amaya Beauty Saloon and SPA, Bank M Tanzaniia, Stanbic Bank, Mimis collections, Kidoti By Jokate Mwegelo, Bongo Real Mamaz na Bluecherriemoe.
Wadau wengine ni Flaviana Matata Foundation, Amina Design, Jenifa Pemba, FM Express events and services ltd, Ernst &Young, ,LR Creations, Millen Magese Foundation Tiffex, Cool Blue Iku Lazaro, Miraj Kikwete, Halima Kamus, Mabibo Beer Wines nd Spirits Ltd, and World Link Travel and Tours ltd.

No comments: