

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuanzia tarehe 1, Januari 2012 inaanza rasmi kushughulikia marejesho ya kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa wasafiri wakigeni wanaondoka kwenda nchi za nje kwa mujibu wa sheria ya kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Fedha TRA, Saleh B. Mashoro, alisema utaratibu huu wa kukusanya VAT umekuwa ukitumika na nchi mbalimbali duniani kutokana na ukweli kuwa VAT ni kodi inayotokana na matumizi.
No comments:
Post a Comment