Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, June 27, 2013

RAIS OBAMA ATUA SENEGAL KWAAA ZIARA YA AFRIKA


Rais Barack Obama amewasili Senegal katika ziara yake ya wiki moja barani Afrika na anatarajia kuzuru Afrika Kusini na Tanzania akilenga kustawisha demokrasia na masuala ya uchumi.
Hii ni ziara ya pili ya Obama barani Afrika tangu achaguliwe Rais mwaka 2008.
Hata hivyo ziara yake inatarajiwa kufifishwa na hali mbaya ya afya inayomkabili aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela. Ikulu ya white house imesema kuwa itategemea uamuzi wa familia ya Bwana Mandela iwapo Rais Obama anaweza kumtembelea hospitalini.
Katika mkutano wake wa leo na rais wa nchi hiyo, Mackey Sall, Rais Obama anatajiriwa kuipa heko Senegal kwa rekodi yake nzuri ya uthabiti ikizingatiwa iko kwenya kanda yenya misukosuko ya kisiasa.
Maafisa wa Marekani wanasema kuwa muhimu katika ziara ya Obama ni kustawisha demokarsia na nchi zote tatu anazotembelea ziko na demokasria thabiti.
Ni ziara ya pili ya Obama katika bara la Afrika tangu kuwa rais wa Marekani mwaka 2008.

No comments: