Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, October 10, 2014

Mashauzi kuwarusha roho mashabiki Swahili Carnival

Maandandalizi ya tamasha kubwa la utamaduni wa mshwahili, Swahili Carnical yanendelea vizuri baada ya wasanii wa muziki kuendekea kuongezeka siku hadi siku.
Kati ya wasanii ambao watatoa burudani siku ya tamasha hilo litakalolofanyika kwenye viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaama ni pamoja na mkali wa muziki wa Taarb nchini, Isha Mashauzi akiwa na bendi yake ya Mashauzi Clasic.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Mratibu wa tamasha hilo la siku tatu, Ahadi Kakore alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na kwamba Isha ni miongoni mwa wasanii wa taarab ambao watakata kiu ya wapenzi wa muziki Tanzania hasa muziki wa taarab.
"Tunashukuru Mungu kwamba kila kitu kinakwenda sawa licha  ya changamoto zilizopo lakini tunaendelea mbele.
"Kwa upande wa burudani tumeweza kufanikiwa kumalilisha kumpaga gwiji wa muziki wa taarab Tanzania, Isha Mashauzi ambaye ataungana na bendi nyingine ikiwemo Yamoto Band katika kuhakikisha watakaokuwepo kwenye tamasha hilo wanapata burudani mwanzo mwisho," alisema Kakore.
Burudani zitakazokuwepo kwenye tamasha hilo ni moja na muziki, mchezo wa soka kwa madiwani, michezo ya jadi,  filamu za Kiswahili, maonyesho ya mavazi, bidhaa za Wajasiliamali na michezo ya watoto.
Tamasha la Swahili Carnival litafanyika kuanzia Novemba 28 hadi 30 kwenye viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam ambapo milango itakuywa wazi kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana.

No comments: