Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Zanzibar, Hamad Masoud (pichani) amejiuzulu kufuatia shinikizo za za watu na maandamano.
Kumekuwa
 na msukumo kutoka kwa makundi mbali mbali ya kutaka waziri huyo 
ang'atuke kufuatia kuongezeka kwa ajali za baharini kati Hatua hii 
imekuja kufuatia madai ya wananchi kuwa ajali za meli zimekuwa 
zikiongezeka mjini Zanzibar bila yeye kuchukua hatua yeyote.
Mbali
 na kujiuzulu kwa Hamad kama Waziri, Rais wa Zanzibar Ali Mohammed Shein
 ameunda Tume ya kuchunguza kiiina cha Meli hiyo ya MV Skagit kuzama na 
kuuwa watu.
Mwenyekiti
 wa tume hiyo atakuwa Jaji Abdulhakim Ameir Issa, wanachama watukiwa 
Meja Jenerali S.S. Omar, Komanda Hassan Mussa Mzee, Kapteni Abdulla 
Yussuf Jumbe, Kaptein Abdulla Juma Abdulla, Salum Taoufiq,Kaptein Hatibu
 Katandula, Bi. Mkali Fauster Ngowo, Ali Omar Chengo na Shaaban Ramadhan
 Abdalla Katibu wa Tume.
Kufuatia shinikizo hizo Siku ya Ijumaa ,tarehe 20 Julai ,Hamad Masoud alimuandikia barua rais wa Zanzibar kumuomba kujiuzu.
Kwa
 mujibu wa taarifa kutoka chama tawala cha CCM, Rais wa Zanzibar Ali 
Mohammed Shein amekubali ombi la Waziri Hamad Masoud kujiuzulu.
Kufuatia
 kujiuzulu kwa waziri huyo, Rais ,Dk Shein amemteua Mbunge wa Jimbo la 
Ziwani Rashid Seif Suleiman kuwa Waziri mpya wa Miundombinu na 
Mawasiliano.
Taarifa kutoka ikulu zinasemna kuwa uteuzi wa Bwana Rashid Seif Suleimna utaanza mara moja

No comments:
Post a Comment