Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, February 18, 2011

RAIS WA TUNISIA YUKO MAHUTUTI KITANDANI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRnUqi0GoROcs6amUXxoBeyk-rKwYIj6yBakDj8fBJ1FQAI73YWAaB6pZZjginFEj-JMMF5i9kzw4fmhFgNW1uWIXxvD0hEkrOd7jp73zR-ky8WSEz1EnMxe54c37Qp1fQJ9Ef2_GstBJF/s1600/BEN+ALI_1.jpg
Aliyekuwa Rais wa Tunisia Zine al-Abidine Ben Ali anaumwa sana na amelazwa katika hospitali ya Saudi Arabia.
Mtu wa karibu wa familia yake ameliambia shirika la habari la AFP, Bw Ben Ali, aliyeondolewa wakati wa ghasia zilizoibuka mwezi uliopita, amepata kiharusi.
Bw Ali mwenye umri wa miaka 74 alikimbilia Saudi Arabia na familia yake baada ya kuwepo maandamano makubwa kwa wiki kadhaa juu ya ukosefu wa ajira na umaskini.
Tunisia kwa sasa ina serikali ya mpito inayoiandaa nchi kwa uchaguzi mkuu.
Jamaa huyo, ambaye jina lake halikutajwa, alisema aliyekuwa Rais yupo "kwenye hali ya kuzimia" katika hospitali moja mjini Jeddah.
Alisema, "alipata kiharusi , na hali yake ni mbaya sana."
Gazeti la Tunisia liitwalo Le Quotidien pia liliripoti siku ya Alhamis kwamba Bw Ben Ali amepata kiharusi.
Wakati huo huo, chanzo cha Saudi Arabia kilichonukuliwa na shirika la habari la Reuters limesema Bw Ben Ali alikuwa "katika hali mbaya."
Awali, msemaji wa serikali ya mpito ya Tunisia amekataa kuthibitisha au kukubali taarifa zozote kuwa Ben Ali yuko hospitali.


 VODACOM YATOA MSAADA KWA WAHANGA WA MABOMU

Mkurugenzi wa mahusiano wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba akiwa amebeba  kapu lenye mikate kwa ajili ya waadhirika wa janga la ulipukaji wa mabomu Gongo la mboto waliopo katika kiwanja cha uhuru,Vodacom Foundation ilitoa misaada mbalimbali .

  LAMPARD AIONYA CHELSEA
Frank Lampard amekiri itakuwa "maafa" iwapo Chelsea itashindwa kufuzu Ligi ya Ubingwa wa Ulaya msimu ujao.
Frank Lampard
Frank Lampard
Sare ya kutofungana dhidi ya Fulham siku ya Jumatatu, imewafanya mabingwa hao watetezi kusalia nafasi ya tano ya msimamo Ligi Kuu ya soka ya England.
Chelsea kwa sasa wapo nyuma kwa pointi 12 ya vinara wa ligi hiyo, Manchester United.
Akizungumza katika uzinduzi wa Wakfu wa Wacheza Soka wa England, Lampard ameiambia BBC kitengo cha michezo : "Hatuna budi kumaliza katika timu nne za juu na kamwe hatupaswi kupoteza michezo zaidi, itakuwa "maafa" iwapo hatutafaulu."
Chelsea siku ya Jumamosi itakabiliana na Everton katika mzunguko wa nne wa hekaheka za kuwania Kombe la FA na watapepetana na FC Copenhagen katika mchezo wa kwanza wa mtoano wa Ligi ya Ubingwa wa Ulaya siku tatu baadae.
Na Lampard amekiri mashindano hayo mawili ni muhimu sana kwa klabu yao.
Msambuliaji aliyesajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 50 na Chelsea, Fernando Torres ameshindwa kufunga katika mechi mbili alizocheza. Torres alinyakuliwa kwa kitita hicho kutoka Liverpool, lakini Lampard amemtetea nyota huyo wa Hispania katika klabu yake mpya.
Kuhusu mlinzi Luiz aliyesajiliwa kwa paundi milioni 25, Lampard amesema amefurahishwa na usajili walioufanya katika dirisha dogo la usajili mwezi wa Januari, ambapo klabu hiyo imetumia paundi milioni 75.


 MTOKO WA JUSTINE BIEBER TOKA KWA D&G
WE caught up with Stefano Gabbana and Domenico Dolce this morning, as they prepare for their Milan show, to see how the designers feel about being the label of choice for the most Googled person on the planet: Justin Bieber. The 16-year-old singer wore a D&G waist coat, bow tie, shirt and jeans as he arrived at the O2 Arena for the premiere his biopic, Never Say Never, where hoards of screaming tweens took part in scenes of mania not seen since the days of The Beatles.
"Justin represents the epitome of the new generation of music talents," Stefano Gabbana told us. "We are fascinated by his capability of communicating with his music to a wide variety of audiences, from the teenagers to a more adult public."

No comments: