Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, February 22, 2011

WAZIRI MAGUFULI ACHARUKA!!

                                                        
AGIZO la Waziri wa Ujenzi John Magufuli la kuweka alama za x mabango yote yaliyoko kandokando ya barabara na kutaka yaondolewe imepingwa vikali na halmashauri zote za jiji na kuamua kulifikisha suala hilo katika ofisi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Raphael Ndunguru, alisema wanajaribu kuangalia suala hilo kisheria ili kuona waliotekeleza hayo wana mamlaka yapi.
Alisema walikutana katika kikao cha pamoja na manispaa za Ilala na Temeke na kuzungumzia chanzo hicho cha mapato kwa halmashauri na yamewekwa kwa kuzingatia kanuni na taratibu.
Ndunguru alisema mwanzoni mwa wiki iliyopita waliamua kulifikisha suala hilo kwa Waziri Mkuu kwa kuwa halmashauri hizo ni sehemu ya serikali hivyo walistahili kukutana na wizara hiyo ili kujadiliana.
“Hatukutendewa sawa mabango yale hayawezi kuchangia kutokea kwa ajali wala si uchafu bali yanapendezesha mji …..lakini kitendo cha kuyaweka alama ya x ndicho kilichosababisha uchafu na tumekubaliana kutoyaondoa kabisa,” alisema.
Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda, alisema wanatarajia kutoa tamko kwa kuwa si kitendo cha kiungwana kilichofanywa cha kuweka alama ya x, kwani mabango hayo ndicho chanzo kikuu cha mapato.
“Kama kulikuwa na tatizo basi sisi ni sehemu ya idara ya serikali tungekaa na kujadiliana na si kuweka uchafu kama walivyofanya,” alisema.
Pia Mkurugenzi Mtendaji wa ZEK Group International, Edwin Sannda, wa kampuni zinazojihusisha na uwekaji mabango ya matangazo nchini, amemshauri Waziri Magufuli kusitisha agizo lake la kutaka mabango yaliyoko kandokando ya barabara kuong’olewa badala yake akutane na wadau wote ili kujadiliana juu ya mfumo unaofaa kwa nia ya kuepuka usumbufu na athari ambazo zimeanza kujitokeza.
Mwishoni mwa mwaka jana, Dk. Magufuli alitoa maelekezo kuwa hataki kuona katika hifadhi ya barabara mabango ya matangazo kwa madai kuwa ni chanzo cha ajali.
Agizo hilo lilifuatiwa na uwekaji alama ya X kwenye mabango na mengine kuondolewa au kuharibiwa bila wahusika kupewa notisi au kushirikishwa.


WATU 65 WAUWAWA KWA TETEMEKO NEW ZEALAND


A 6.3-magnitude earthquake rocked the southern New Zealand city of Christchurch Tuesday, killing dozens, collapsing buildings and cracking streets.
Prime Minister John Key said at least 65 had died as a result of the disaster and told reporters  that the death toll was expected to rise further. "It is a just a scene of utter devastation," he added.
Television footage showed streets strewn with bricks and shattered concrete. Sidewalks and roads were cracked and split, and hundreds of dazed, screaming and crying residents wandered as sirens blared throughout the city.
Bodies were being pulled from rubble, others lay in the streets. Water mains burst, causing extensive flooding

6 wauwa katika vurugu Ivory Coast


Vurugu imekuwa ikishuhudiwa nchini Ivory Coast tangu mwaka uliopita.
Takriban watu sita wameripotiwa kufa nchini Ivory Coast Jumatatu iliyopita wakati wanajeshi waliwafyatulia risasi waandamanaji katika mji mkubwa zaidi, Abidjan.
Walioshuhudia wanasema wanajeshi watiifu kwa kiongozi aliye madarakani, Laurent Gbagbo, waliwapiga risasi wafuasi wa Alassane Ouattara, kiongozi wa upinzani anayetambulika na jamii ya kimataifa kama aliyeshinda uchaguzi wa urais wa mwaka uliopita.
Ujumbe wa Muungano wa Afrika unaozuru Ivory Coast unatarajiwa kurudia matakwa yao kumtaka Bw Gbagbo ajiuzulu.Ivory



              WAKE WA VIGOGO  WATEMBELEA WAHANGA WA MABOMU


MKE WA WAZIRI MKUU Mama Tunu Pinda jana mchana (Jumatatu, Februari 21, 2011) amewaongoza wake wa viongozi mbalimbali wa kitaifa kutoa msaada kwa watu waliopata maafa kutokana na mlipuko wa mabomu ya Gongo la Mboto, wilayani Ilala jijini Dar es Salaam. 

Akitoa taarifa kwa niaba ya akinamama hao 26 walioambatana naye, Mama Pinda alisema wao kwa niaba ya wake wengine wa viongozi ambao wameshindwa kufika kutokana na majukumu mengine, wameguswa na tukio hilo na wanawapa pole waathirika wote kwa maafa yaliyowapata.

“Tunatambua kuwa kuwa wako waliofariki, waliopoteza wapendwa wao na waliopata ulemavu na wengine waliopoteza mali katika tukio hili... wote tunawapa pole na kumuomba Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki kigumu,“ alisema.

Alisema wanatoa pole kwa wote lakini zaidi kwa akinamama kwa sababu wao ndiyo wanahangaika zaidi majanga yanapotokea ikiwemo kukimbia na watoto au ndugu wasiojiweza.

Misaada iliyotolewa ni kilo 200 za mchele, kilo 100 za sukari, kilo 500 za unga wa mahindi, mafuta ya kujipaka katoni moja, sabuni za kufulia katoni moja, dawa za meno katoni moja, doti za khanga 55 ambayo ina thamani ya sh. milioni 1.5/-. Pia walitoa mabegi matatu ya nguo za wakubwa na watoto ambazo thamani yake haikuweza kupatikana mara moja.

Akipokea misaada hiyo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Meck Sadick, aliwashukuru viongozi hao na kuwaahidi kuwa itakabidhiwa kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ambayo itavigawa vifaa hivyo kwa wahusika.

Wake hao wa viongozi walitembelea pia Hospitali ya Wilaya ya Temeke ambako Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Mariam Malliwa aliwaeleza kwamba hivi sasa wamebaki wagonjwa wawili tu ambao wanaendelea vizuri. Alisema mlipuko ulipotokea walipokea wagonjwa 139, ambao sita walipelekwa Muhimbili, 129 walitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani lakini wawili walifariki.

No comments: