Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, March 24, 2011

Happy Birthday to theUNIQUEENTERTZ.BLOGSPOT.COM


 TUNAYO FURAHA KUWAJULISHA WASOMAJI WA BLOGU HII KUWA APRIL1,2010 TUNATIMIZA MWAKA MMOJA TOKA TUWE HEWANI,TUTUMIE SALAMU ZA BIRTHDAY TUTAZIWEKA HEWANI.kupitia uniqueentertz@yahoo.com, facebook: magese unique (am nothing without my funs)

 

RAIS JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA WIZARA YA MAJI

Rais Jakaya Kikwete, akisisitiza jambo kuhusu upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama nchini kwa Waziri wa Maji Prof. Mark Mwandosya, baada ya kuzungumza na viongozi na wafanyakazi wa Wizara, Idara, Taasisi na Wakala wa Wizara hiyo leo jijini Dar es salam. 

Gaddafi ashambulia miji muhimu ya waasi


Libya
Mapigano baina ya waasi na majeshi yanayomtii kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi yamekuwa yakiendelea katika miji muhimu baada ya mashambulio ya anga yanayoendelea kwa mfululizo wa siku ya tano sasa yanayofanywa na majeshi ya kimataifa.
Milio mingi ya milipuko ilisikika usiku kwenye mji mkuu wa Tripoli.
Katika mji unaoshikiliwa na waasi Misrata, mashariki mwa Tripoli, vifaru vya serikali vimekuwa vikishambulia eneo karibu na hospitali.
Kumekuwa pia na ripoti juu ya mapigano makali baina ya waasi na majeshi yanayomwuunga mkono Gaddafi mjini Ajdabiya.
Wakazi waliokimbia mji huo wameelezea kuwepo kwa makombora, milio ya risasi na nyumba kuwashwa moto.

Mashambulio ya anga

Kulingana na vyanzo vya jeshi vya Libya na vyombo vya habari vimesema, kuna ripoti za kuwepo mashambulio ya anga yaliyofanywa na nchi za magharibi kwenye mji wa Tajura.
Na jeshi la Ufaransa limesema mashambulio ya anga yaliyofanywa na Ufaransa yamelenga kituo cha anga cha Libya ndani ya nchi hiyo nyakati za usiku.
Siku ya Alhamis, ndege za kijeshi za nchi za magharibi zimeripotiwa kushambulia mji wa Sebha kusini mwa Libya, kulingana na wakazi na taarifa kutoka vyombo vya habari.
Sebha, uliopo kilomita 750 kusini mwa Tripoli, ni eneo lililodhibitiwa vilivyo na ni kitovu cha kijeshi cha Kanali Gaddafi.
Pia kumeripotiwa kuwepo kwa mlipuko nyakati za usiku kwenye kituo cha kijeshi eneo la Tajura mashariki mwa Tripoli.


UVAAJI WA SHANGA NI RUKSA KILA MAHALI?
Hivi ndivyo kizazi cha wasichana wa siku hizi wanavyo vaa na kuweka mambo yao ya falagha hadharani, zamani ilikuwa ni nandra kumuona mwananke akiwa amevaa shanga "chachandu" nje namna hii. Na vitu hivi hupaswa kuvaliwa kwa heshima. Je hii ndo kwenda na fasheni au tunawafundisha nini watoto wetu? . Picha hii imepigwa jijini Dar es Salaam katika daladala msichana huyu akiteremka kituoni.

Polisi wa Uganda rawamani kwa utesaji raia

Kulingana na ripoti iliyotolewa na shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch HRW, kitengo maalum cha polisi cha Uganda kimefanya utesaji, kutumia nguvu kupita kiasi na mauaji holela.
Ripoti hiyo imesema maafisa wa kikosi maalum cha polisi huwapiga watu mara kwa mara na vifaa kama marungu, chupa na vyuma.
Imesema katika matukio mengine walikuwa wakiwaingizia pini chini ya kucha za washukiwa.
Msemaji wa polisi wa Uganda alisema kumekuwa na ripoti za utesaji, lakini idadi yao imepungua.
Ripoti hiyo yenye kurasa 59 imetolewa kutokana na ushahidi wa zaidi ya watu 100 na waliokuwa washukiwa, familia zao, na waliokuwa kwenye kikosi cha polisi pamoja na ambao bado wapo kwenye nafasi hizo.

R.I.P MUIGIZAJI LIZ TAYLOR


Actress maarufu wa filamu duniani,Elizabeth Rosemond Taylor aka Liz Taylor amefariki dunia Jumatano ya tarehe 23 March,2011 akiwa na miaka 79,baada ya kulazwa kwa muda wa wiki 6 kwenye hospitali ya Cedars-Sinai Medical Center jijini Los Angeles-Marekani

Liz Taylor alizaliwa London tarehe 27 February 1932,alianza kuugua ugonjwa wa moyo tangu mwaka 2004 na enzi za uhai wake aliwahi ku-act movie zaidi ya 50 na kuwahi kuolewa zaidi ya mara 8 na waume tofauti,na mpaka anafariki ameacha watoto 4,wajukuu 10 na vitukuu 4

No comments: