Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, March 10, 2011

MUSTAFA HASSANALI AALIKWA KWENYE ONYESHO LA MAVAZILA ‘ARISE MAGAZINE FASHION WEEK’NIGERIA


Nigerian Model Sola in Mustafa HassanaliNigerian Supermodel



OLUCHI OMWEAGBA In A mustafa Hassanali.

Baada tu ya kuzindua kwa toleo la kiafrika ndani ya Movenpick jijini Dar es salaam, mbunifu wa kipekee wa kiafrika toka Tanzania Mustafa Hassanali amealikwa kushiriki katika maonyesho ya mavazi yanayojulikana kama ‘Arise Magazine Fashion Week’ yanayotarajiwa kufanyika tarehe 10 hadi 13 Machi 2011 ndani ya jiji la Lagos Nigeria.


‘Arise Magazine Fashion Week iliyoandaliwa na Nigeria’s this Day, inanatarajiwa kukusanya wabunifu mahiri wa Afrika wa ndani na waishio nje ya mipaka ya Afrika watakaoonyesha ubunifu wao, huku wakisindikizwa na wasanii maarufu wa muziki kama vile Dbanj, Keri Hilson, and Estelle.


Akizungumzia akiwa ndani ya jiji la Lagos Nigeria, Mustafa Hassanali alinukuliwa akisema kuwa “nimefarijika na kufurahishwa sana kuwa mmoja wa washiriki wa onyesho hili la ‘Arise Magazine’. Kuwa kwangu wa kwanza kwa mara nyingine tena kualikwa katika onyesho hili la wana wa Afrika kunaonyesha kukubalika kwangu kama mbunifu katika jamii ya mitindo kimataifa” alisema Mustafa Hassanali.


Mustafa Hassanali ataonyesha mavazi yake ya kiafrika yaliozinduliwa Dar es salaam tarehe 4 March katika onyesho la Mamma MIA kwa msaada wa Utepe Mweupe, toleo ambalo lililosanifiwa na uzuri wa Bara la Afrika, mg’ao wa miale ya asubuhi ya jua na machweo yake, ukarimu na ucheshi wa watu wake.


“kama hujapendeza, gauni lako halijameremeta, na halina mkia, hilo si gauni la Mustafa Hassanali, kama toleo langu hili nimetumia uhalisia wa kitanzania, khanga na kupambwa kwa thamani na hariri za hadhi.” alijigamba Mustafa Hassanali.


Arise Magazine Fashion Week’ itafanyika katika hoteli ya Federal Palace Ijumaa ya tarehe 11 Machi saa 9 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
 


HATMA YA IVORY COAST ITAJULIKANA LEO
wafuasi wa outarra
visa vya ghasia kati ya wafuasi wa viongozi hawa wawili vinaongezeka mjini Abidjan

Baada tu ya kuzindua kwa toleo la kiafrika ndani ya Movenpick jijini Dar es salaam, mbunifu wa kipekee wa kiafrika toka Tanzania Mustafa Hassanali amealikwa kushiriki katika maonyesho ya mavazi yanayojulikana kama ‘Arise Magazine Fashion Week’ yanayotarajiwa kufanyika tarehe 10 hadi 13 Machi 2011 ndani ya jiji la Lagos Nigeria.

‘Arise Magazine Fashion Week iliyoandaliwa na Nigeria’s this Day, inanatarajiwa kukusanya wabunifu mahiri wa Afrika wa ndani na waishio nje ya mipaka ya Afrika watakaoonyesha ubunifu wao, huku wakisindikizwa na wasanii maarufu wa muziki kama vile Dbanj, Keri Hilson, and Estelle.

Akizungumzia akiwa ndani ya jiji la Lagos Nigeria, Mustafa Hassanali alinukuliwa akisema kuwa “nimefarijika na kufurahishwa sana kuwa mmoja wa washiriki wa onyesho hili la ‘Arise Magazine’. Kuwa kwangu wa kwanza kwa mara nyingine tena kualikwa katika onyesho hili la wana wa Afrika kunaonyesha kukubalika kwangu kama mbunifu katika jamii ya mitindo kimataifa” alisema Mustafa Hassanali.

Mustafa Hassanali ataonyesha mavazi yake ya kiafrika yaliozinduliwa Dar es salaam tarehe 4 March katika onyesho la Mamma MIA kwa msaada wa Utepe Mweupe, toleo ambalo lililosanifiwa na uzuri wa Bara la Afrika,  mg’ao wa miale ya asubuhi ya jua na machweo yake, ukarimu na ucheshi wa watu wake.

“kama hujapendeza, gauni lako halijameremeta, na halina mkia, hilo si gauni la Mustafa Hassanali, kama toleo langu hili nimetumia uhalisia wa kitanzania, khanga na kupambwa kwa thamani na hariri za hadhi.” alijigamba Mustafa Hassanali.

Arise Magazine Fashion Week’  itafanyika katika hoteli ya Federal Palace Ijumaa ya tarehe 11 Machi saa 9 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Baraza la usalama la Umoja wa Afrika linakutana mjini Addis Ababa, Ethiopia kujadili hatua za kuchukuliwa baada ya juhudi za upatanishi nchini Ivory Coast kushindikana kwa mara nyingine.
Bw Alassane Outarra ambaye anatambulika kama mshindi wa uchaguzi uliofanyika Novemba mwaka jana, kwa mara ya kwanza amesafiri kutoka nchini humo kuhudhuria mkutano huo.
Lakini Rais Laurent Gbagbo ameususia na badala yake amemtuma kiongozi wa chama chake Bw Pascal Affi N'Guessan.
Baraza hilo litajadili ripoti ya jopo la viongozi watano walioteuliwa na Umoja huo kuongoza duru hii ya upatanishi kabla ya kutoa uamuzi wa hatua za kuchukuliwa kusuluhisha mzozo huo.
Jopo hilo linaongogzwa na Rais wa Mauritania Mohammed Ould Abdel Aziz. Wengine ni Jakaya Kikwete wa Tanzania, Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Idriss Deby wa Chad na Blaise Compaore wa Burkina Faso.
Awali Umoja wa Afrika,ulitishia kutumia nguvu za kijeshi kumondoa Bw Gbagbo ambaye amekataa kuachia wadhifa wa urais.
Athari za vikwazo vya kiuchumi vilivyowekewa utawala wa Gbagbo zimeanza kusikika. Duru zinasema serikali sasa imeshindwa kulipa mishahara ya watumishi wa umma wakiwemo wanajeshi.

Uefa yawashitaki Wenger na Samir Nasri

Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger pamoja na mshambuliaji wa pembeni wa timu hiyo Samir Nasri, wameshtakiwa na Shirikisho la soka barani Ulaya- Uefa kutokana na matamshi yao makali dhidi ya mwamuzi baada ya kufungwa na Barcelona usiku wa Jumanne.

Arsene Wenger akibishana na mwamuzi Massimo Busacca
Arsene Wenger akibishana na mwamuzi Massimo Busacca

Msemaji wa Uefa amesema shauri hili linahusu mwenendo mbaya wa kocha na mchezaji.
Samir Nasri
Samir Nasri


Wanashtakiwa kwa kutumia "lugha mbaya" kwa mwamuzi Massimo Busacca baada ya mpambano wa usiku wa kuwania ubingwa wa Ulaya dhidi ya Barcelona.
Wenger alirushiana maneno makali na Massimo Busacca baada ya kichapo cha 3-1 na kutolewa kwenye mashindano ya Ligi ya Ubingwa wa Ulaya.
Wenger alikasirishwa na uamuzi wa kutolewa nje mshambuliaji wao Robin van Persie kwa kuoneshwa kadi ya manjano ya pili, wakati huo timu hizo mbili zilipokuwa nguvu sawa kwa kufungana 1-1 katika dakika ya 56.

Paris Fashion Week Round Up

While we’re all set for Lakme Fashion Week to kick start tonight, we’re also still excited about howthe last of the international fashion weeks on a high – with Kate Moss no less.  The leggy British model walked the ramp for Louis Vuitton, while Galliano surprised the world by showcasing his collection amidst all the controversy.

From Chanel’s array of constructed looks to Yves Saint Laurent’s fluid ensembles and Alexander McQueen Ice Queen collection - Paris was high octane glamour at its best.

ENZI ZA UHAI WA PENZI LA CHISS BIZZ NA RIHANNA
Batailikuwa kila sehemu leo hii wamekuwa paka na chui wanatundikiana mapicha ya utupu mitandaoni. 
picha hii rihana alipiga kwa raha zake ila leo imekuwa kilio kwake

Congo ya ruhusu uchimbaji wa madini

Joseph Kabila
Waasi mashariki mwa nchi hiyo wanatumia faida ya madini kufadhili shughuli zao
Utawala wa Rais Joseph Kabila umeruhusu tena shughuli za kuchimba madini mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya kipindi cha miezi sita.
Rais Kabila aliweka marufuku hiyo ili kudhibiti biashara ya magendo ambayo imesababisha serikali kukosa kipato kutoka utajiri wake wa madini.
Uchimbaji na mauzo haramu ya madini hayo pia umekuwa ukichochea utovu wa usalama katika mikoa ya Kivu kaskazini na Kusini.
Waziri wa madini nchini humo, Martin Kabwelulu amesema kuwa harakati za kuwadhibiti waasi katika eneo hilo na mikakati ya serikali ya kuimarisha usimamizi wa shughuli za kuchimba madini ndio zimechangia marufuku hiyo kuondolewa.
Viongozi katika maeneo husika wameshirikishwa katika mikakati hiyo kuhakikisha kuwa utawala wa mikoa pia unafaidi kutoka kwa wawekezaji watakao sajiliwa kuchimba madini nchini humo.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inautajiri mkubwa wa madini yakiwemo, dhahabu, almasi na Kobalti yenye thamani kubwa kwenye soko la kimataifa.
Wiki iliopita Rais Kabila na mwenzake wa Kenya Mwai Kibaki walizindua tume ya pamoja itakayo endesha harakati za kudhibiti biashara ya magendo ya dhahabu.
Uchunguzi umeonyesha kuwa mtandao wa biashara hiyo ya magendo unaendesha shughuli zake nchini Kenya.

Serikali Yampiga 'Stop' Babu Wa Loliondo


WAZIRI wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdori Shirima kuzuia haraka matibabu ya magonjwa sugu yanayoendeshwa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la KKKT, Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa Sale, Loliondo.

Dk Mponda alisema hayo jana alipokuwa akijibu swali la waandishi wa habari baada ya kumaliza kuzindua matumizi ya Bajaji kwa ajili ya kusafirishia wagonjwa. Alisema amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kumzuia mchungaji huyo kuendelea na utoaji wa dawa mpaka serikali itakapojiridhisha na hali ya usalama pamoja na uwezo wa dawa hiyo.

“Kutokana na hali halisi ya usalama wa kiafya kwa sasa katika eneo hilo, kuna hatari ya kuwepo kwa milipuko ya magonjwa kwa kuwa idadi ya watu inazidi kuongezeka,” alisema Dk Mponda.

No comments: