Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, March 1, 2011

KIKWETE-TANZANIA HAITOISHA MATATIZO

Kauli ya mh.jk akitoa katika hotuba ya mwisho wa mwezi kwa vyombo vya habari kuwa yeye hawezi kuyamaliza matatizo yote ya nchi hii kwani waliomtangulia hawakuyamaliza,apewe muda.   Baba wa taifa alitawala miaka 23 na hakuyamaliza, mzee mwinyi na mzee mkapa walitawala miaka kumikumi na hawakuyamaliza matatizo yote ya nchi hii,je yeye atawezaje kuyamaliza kwa miaka mitano tu.
   wachambuzi wa mambo ya kisiasa nchini Tanzania wamesema serikari ya ccm ina hofu kubwa ikiwa nguvu ya umma kwa kushawishiwa na chadema itaenda kama chadema walivyopanga kuleta mageuzi ya uongozi.


Twanga Pepeta kufanya onyesho maalum la kuchangia walioathirika na Mabomu ya Gongo la Mboto


Bendi ya African Stars "Twanga Pepeta" Ijumaa ijayo inataraji kufanya onyesho maalum la kuchangia walioathirika na Mabomu ya Gongo la Mboto.
Onyesho hilo linataraji kufanyika katika ukumbi wa Zhonghua Garden uliopo maeneo ya Victoria siku ya ijumaa tarehe 4-02-2011 na linataraji kuanza saa tatu za usiku. 

MODEL ZUHRA
A model from Tanzania contact her  +255 714883703

Maafisa wa UM washambuliwa Ivory Coast

Umoja wa Mataifa umesema maafisa wake walishambuliwa nchini Ivory Coast walipokuwa wakipeleleza taarifa za ukiukaji wa sheria za vikwazo vya silaha vilivyowekewa nchi hiyo.
Kikosi cha Umoja wa Mataifa likishika doria nchini Ivory Coast
Kikosi cha Umoja wa Mataifa likishika doria nchini Ivory Coast
Maafisa hao walishambuliwa wakiwa katika mji mkuu wa Yamoussoukro.
Walikuwa wakichunguza ripoti kwamba Belarus ilitoa helikopta kuwafadhili wafuasi wa Laurent Gbagbo ambaye amekataa kuachia madaraka.
Umoja huo umesema haujafanikiwa kuthibitisha taarifa kuhusu shehena hiyo lakini maafisa wake wataendelea kufuatilia hali nchini humo.
Mkutano ulioandaliwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili ripoti hiyo imefutwa.
Wakati huo huo, waasi wa zamani wa Ivory Coast walisema wako tayari kujihami na kupambana dhidi ya Bw Gbagbo.
Msemaji wa kundi hilo la New Forces, Cisee Sindou, aliiambia BBC kwamba iwapo mtafaruku utaendelea baina ya wafuasi wa Bw Gbagbo na hasimu wake Alassane Ouattara, kundi hilo litachukua hatua.
Lakini Bw Sindoue alisema kuwa hakuna operesheni ya kivita iliyopangwa.
Bw Ouattara anatambuliwa na wengi kama mshindi wa uchaguzi wa urais wa Novemba mwaka jana.
Bw Gbagbo na Bw Ouattara hawajatoa kauli yoyote kuhusiana na ilani aliyotoa msemaji huo wa waasi.


 MENGI AFANYA KUFURU GONGO LA MBOTO
Tajiri mashuhuri afrika mashariki na kati Bw.Regnald Mengi ametoa tani 18 za chakula kwa wahanga wa mabomu na fidia ya laki tano kwa kila kaya iliyopatwa na majanga ya mabomu ya gongo la mboto.



CHADEMA WAITEKA SHINYANGA
Viongozi wa Chadema na wabunge wa chama hicho wakiwa wanaandamana mkoani Shinyanga huku akiwa ametanguliwa na vijana wa chama hicho Redbriged.

Wanafunzi wa shule ya msingi Jomu wakiwa katika maandamamo ya Chama cha Demokaria na Maendeleo yaliofanyika mjini Shinyanga jana huku wakiwa wameshikana na kuonesha alama ya Vidole viwili.
Mwenyekiti wa Chadema taifa Freeman Mbowe akisisitiza kuendelea na maandamano kumjibu Rais Jakaya Kikwete.

Aliyekuwa Mgombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini Shilembi Magadula Shilembi ambaye kutotangazwa kakwe mshindi kulisababisha vulugu kubwa katika mji wa Shinyanga na kuchomwa moto kwa ofisi za Halmashauri.

Mabango mbalimbali ya waandamanaji wa mkoa wa Shinyanga yakionekana kuwa na ujumbe mbalimbali kwa rais Kikwete.

FA ya Misri yapunguzia mishahara

Chama cha soka nchini Misri (EFA) kimetangaza kitapunguza mishahara ya wafanyakazi wake.
Wachezaji wa timu ya taifa ya Misri
Wachezaji wa timu ya taifa ya Misri


Wachezaji wa timu ya taifa nao huenda mishahara yao ikipunguzwa.
Taarifa iliyotolewa kupitia mtandao wa EFA imeeleza hakuna mfanyakazi yeyote ndani ya chama hicho atakayepokea mshahara unaozidi dola 2,500, wakati mshahara wa kima cha chini utakuwa ni kiasi cha dola 250.
Hivi karibuni Misri ilikumbwa na tafrani za kisiasa, hali iliyosababisha kusimamishwa shughuli za soka nchini humo kiasi mapato yamepungua.
Taarifa hiyo imeendelea kueleza uamuzi huo "unakwenda sambamba na hisia za mapinduzi".
EFA pia wamesema watakutana na vilabu vya soka nchini humo kukubaliana taratibu za fidia kwa wachezaji watakaoitwa katika timu ya taifa.

MASHINDANO YA NGUMI TAIFA YAMEFUNGULIWA

Bondia wa Mkoa wa Ilala Edward Jackson (kulia) akioneshana kiwango cha kutupa masumbwi na Mohamedi Abdalah wa Arusha wakati wa mashindano ya klabu bingwa taifa yanayofanyika uwanja wa ndani wa taifa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

FINAL TOUCH OF MUSTAFA HASSANALI COLLECTION, READY FOR MAMMA MIA CHARITY FASHION SHOW 4TH - 5TH MARCH

     Mustafa Hassanali puts the final touch of his collection that will be shown at Mamma MIA Charity Fashion show on 4th -5th March
            Mustafa Hassanali, on the last minutes preparation of his collection for Mamma MIA
The renowned Tanzania Pan African Designer Mustafa Hassanali work on his collection for the Mamma MIA Charity Fashion show, 4th - 5th March
 
 

 MGOMO WA MADENTI WA IFM
Mmoja kati ya viongozi wa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM, aliyetambulika kwa jina moja la Moses, akiwafafanulia jambo wanafunzi wenzake wakati walipogoma kuingia madarasani leo asubuhi, wakidai haki zao.
Madenti hawa wamegomea kuhusu kuzuiwa wenzao wasio maliza kulipa ada wafanye pepa  


SALAMU ZENU WADAU!!
 WELCOME BACK, Ndugu msomaji usisahau kuclick older post kwa habari kemmem zilizopita katika blogu hii hapo chini.

No comments: