Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, July 19, 2013

CHRISTIANABELLA MSANGI SPECIAL NIGHT


Biharusi Mtarajiwa, Christabella Msangi akipunga mkono kusalimia wageni waalikwa katika tafrija yake ya kukata na shoka iliyofanyika ukumbi wa Lion Hotel Sinza jijini Dar es Salaam usiku wa Julai 18, 2013 sambamba na Siku ya Kimataifa ya Mandela.

Chritabella anataraji kufunga ndoa Julai 20, 2013 na Bwana Norbert Kinyaia kanisa Katoliki Parokia ya Segerea jijini Dar es Salaam.

Production by: MD Digital Company - +255 755 373 999 au +255 717 002 303 WatsApp - +255 788207274.

Bi Harusi mtarajiwa Chritabella akiwa na mpambe wake Mrs Eliflorida Mbazi.
Bi harusi mtarajiwa, Christabella akikata keki yake.
 Huyu ndiye kijana Mtanashati, Norbert Kinyaiya ambaye ama kwa hakika alikuwa akimyima usingizi Bi. Christabella na akaamua kuwaambia wazazi wake yupo tayari sasa kuambatana nae na Mungu akijalia Jumamosi Julai 20, 2013 watapata Baraka za Mungu kuwa mwili mmoja na kuambatana vyema kila mmoja akiachana na wazazi wake.
 Mama Msangi akilamba picha na Binti zake.
 Mzee Msangi nae akipiga picha na vito vya thamani kutoka katika uzao wake.
 Hii sasa ndio familia kamili ya Mzee Msangi ikiwa katika picha ya pamoja.
 Kakaz na dadaz wa Bi harusi wakimwagia mafweza Christabella.
 Mambo yalipendeza hapa ni mashangazi wakipaa vyao huku wakiangalia kwa namna tafrija inavyoenda.
 wacha weeeeeeeeee...!!! Raha ya sherehe ni kucheza na kupiga menu! hapa mambo yalinoga.
 Wengine walishindwa kusimama lakini walionesha umahiri wao hapo hapo vitini walipoketi.
Waalikwa ....
Pozi zilikuwepo kupata taswira za kuvutia....
 Wageni waalikwa mbalimbali walikuwepo Ukumbini hapo...
 hapana chezea familia ya Msangi wewe.

 Christabella anaolewa uchagani na hapa akipata staili ya uchezaji wa watani zake.. kwa kushikana mikono ili wasije fanyiana ndivyo sivyo watu wakakosa nauri.
Yap! Yap huu nao ni mmoja ya uchezaji ...

No comments: