Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, May 25, 2011

RYAN GIGGS NA SKENDO YA KUHUJUIMU NDOA YAKE

Pamekuwa na minong'ono kwamba mchezaji wa Man United ya Uingereza,Ryan Joseph Giggs ametembea na mmoja wa aliyekuwa mshiriki katika kipindi cha televisheni cha Big Brother,Imogen Thomas

IMOGEN THOMAS
Tuhuma hizo za muda mrefu na kabla ilipitishwa sheria mahsusi kuwalinda watu maarufu kutotolewa hadharani mambo yao ya siri kwa sababu wanazozifahamu wao wenyewe.Lakini ghafla bin vuu, mbunge kwa tiketi ya chama cha Liberal,John Hemming,akiwa bungeni akateleza ulimi na kumtaja mchezaji huyo anayelindwa na sheria hiyo kuwa ni Ryan Giggs wa Man United, na amekuwa mmoja wa wanaharakati ambaye amekuwa akipinga kwa mchezaji huyu kulindwa na sheria hiyo. Huku wakati huo huo watumiaji wa mtandao wa Twitter ambao walikuwa wameshalinyaka jina hilo na kuanza kumegeana ndogo ndogo kwa sasa Giggs yuko kwenye wakati mgumu sana hasa ndoa yake na kwa sasa habari hiyo imeshaenea duniani kote...!

  

Nato yaishambulia Libya usiku kucha


Mashambulio ya anga Libya
Takriban milipuko mikubwa mitano imeitikisa Tripoli usiku kucha, wakati harakati za majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato zikiendelea kwenye mji mkuu wa Libya.
Kwa usiku wa pili, mashambulio ya anga yalilenga ngome ya Bab al-Aziziya ya Kanali Muammar Gaddafi.
Nato inatekeleza azimio la umoja wa mataifa la kulinda raia wa Libya, kufuatia maandamano dhidi ya uongozi wa Kanali Gaddafi.
Lakini Urusi, ambayo haikuunga mkono azimio hilo, imesema uvamizi huo ni ukiukwaji wa umoja huo.
Mwandishi wa BBC Andrew North mjini Tripoli alisema mashambulio ya Jumanne usiku si makubwa kama yaliyofanyika Jumatatu usiku, lakini bado yalitikisa majengo eneo kubwa.
Moshi ulionekana kutanda kwenye mji huo.
Nato ilisema ngome hiyo ya Bab al-Aziziya imekuwa ikitumika kama kituo cha majeshi na magari ya kijeshi yaliyotumika kushambulia raia.
Lakini serikali ya Libya imesema Nato inajaribu kumwuua Kanali Gaddafi na mashambulio ya usiku yanawatisha raia wa Tripoli

No comments: