Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, February 8, 2012

WANAHARAKATI WAANDAMANA KUSHINIKIZA SERIKALI ICHUKUE HATUA JUU YA MGOMO WA MADAKTARI WA MUHIMBILI

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba akizungumza na waandishi wa habari katika maeneo ya Salender Brige, kuelezea maadamano ya wanaharakati hao ya kuishinikiza serikali kuchukua hatua na kutatua mgogoro wa mgomo wa Madaktari wa Hospitali ya Muhimbili, ulioanza hivi karibuni na ambao bado unaendelea. Ameongeza kwamba hali ya wagonjwa inaendelea kuwa mbaya zaidi kwa sababu ya mgomo huo, Dk Hellen Kijo-Bisimba mara baada ya kumalizika kwa maandamano hayo yaliyofanyika leo.
Mkurugenzi wa TAMWA, Analilea Nkya akiwa ameshikilia bango lake wakati wa maandamano hayo jijini Dar es salaam leo.
Polisi wakiwaamuru waandamanaji watawanyike mara baada ya kufika katika eneo la Salender Brige jijini Dar es salaam leo.
Mkurugenzi wa TAMWA,Mama Ananilea Nkya (kulia) akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari mbalimbali kuhusiana na maandamano yao yaliyodumu kwa muda wa masaa mawili hivi kwa ajili ya kuishinikiza Serikali ikae meza moja na madaktari na kuhakikisha mgomo wao unakoma mara moja na kuhakikisha shughuli za matibabu hospitali ya Muhimbili na nyinginezo zinaendelea kama kawaida.
Amri ikitolewa kuwataka wanaharakati kuondoka eneo hilo,kwani ilielezwa kuwa maandamano hayo yamefanyika bila kubarikiwa.
Askari wakiwa eneo la tukio mapema leo jioni.
Ujumbe kutoka kwa wanaharakati hao.
Mwanaharakati akiwa na ujumbe wake.

No comments: