Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, July 4, 2013

MCHEZEAJI FACEBOOK A/C YA JOKATE ATIWA MBARONI

 Hapa ni wakati Jokate alipoamua kukaa na Mpeka kistaarabu kuongea nae kabla ya hatua za kisheria

 Message  alizotumia watu kwenye facebook na msg za simu za mkononi.
 
Aliyefanikisha huyu jamaa kukamatwa ni mrembo mmoja model Blessing ambae alishiriki Miss Morogoro 2013 ambapo namkariri akisema:

“Wiki mbili zilizopita nilipata msg kwamba Kidoti hair na Mzinga Planet wanahitaji mamodo kwa ajili ya kutengeneza matangazo kwa ajili ya nywele za kidoti, tulikua Morogoro kwa ajili ya Miss Morogoro tukaja Dar mpaka Mzalendo Pub msg ilipotuelekeza lakini nilivyoingia sikuona mtu ambae anahusiana na Jokate, niliona watu ambao nawajua lakini sio kuhusu nywele.


"Nikampigia kaka mmoja anaitwa Johnson kwa sababu najua anafahamiana na Jokate, nikampigia kumfokea kumwambia nyinyi vipi mbona mmetangaza audition alafu sioni hata mtu mmoja ambae anahusika? naona watu ambao kampuni zao zipo majumbani kwao? 

"Baada ya dakika zaidi ya 10 kina Jokate wakawa wameshafika japo baadhi ya mamodo wengine walikua wameshaondoka lakini baadhi ya viongozi kama Majaji wa kike walikuwepo na walipoulizwa wakasema tumsubiri Mpeka ambae ndio muhusika na pia Mkurugenzi wa Mzinga Planet” – Blessing


Baada ya kina Jokate kufika Mpeka alipigiwa simu ili arudi Mzalendo Pub, japo alisita sana mtuhumiwa huyu alikuja kwenye eneo la tukio na kukutana uso kwa uso na Jokate na timu yake, baada ya hapo akaanza kusingizia kwamba yeye hahuusiki ila kuna watu wengine ndio wanahusika ila alipotoa namba zao wakapigiwa simu, kila mmoja alionekana kutaharuki kwa sababu hawajui chochote kuhusu hiyo Mzinga Planet.
Baada ya Jokate na timu yake kukaa na Mpeka na kumuuliza kistaarabu bila kutoa ushirikiano wa kutosha, uamuzi ulitoka kwamba apelekwe Polisi Osterbay ili kuendelea na taratibu nyingine za kisheria.

Mpeka alikua anaonekana analia wakati mwingie na hiyo ilikua ni baada ya kumpiga huyu msichana shuhuda aitwae Blessing kwa sababu alimchomea mpaka akakamtwa.

No comments: